Mishahara ya SUMATRA kufuru

Mishahara ya SUMATRA kufuru

Huo ni mshahara mdogo sana,nilitaka kuona labda Mil 9 hivi gross salary,
 
Baada ya makato anabakia na 954,000. Je huo unauona ni mshahara wa kufuru.
Huyu inabidi apande basi ili aweze kusave hela nyingi.

Huu ni mshahara wa kawaida sana
Hata mimi naona ni mkubwa, maana mimi take home yangu ni nusu ya take home uliyoiweka hapo. Lkn haina noma,yote maisha.
 
Mleta maada yuko sahihi,naweza kumwelewa kwani hata kwenye sector binafsi hususani benki za kigeni ni tatizo sana
Mfano mimi mwenyew binafsi nina shahada ya uhasibu nasimamishwa dirishani tangu saa 8:30 hadi saa 06:00 nakula vumbi la hela naishia kuambulia 450k per month,hapo lazima 1.53m nione kufuru
 
HHAHAHA WE JAMAA NI MPUUZI KWELI NI KATI YA WATU MNAORUDISHA NYUMA MAENDELEO.

YAANI MSHAHARA WA M 1.5 NI MKUBWA?? NI WASTAN WA 50K TU PER DAY..

HV UNAJUA KUNA WAKURUGENZ WANAJILIPA M.40 KWA MWEZ? WASTANI WA M 1.1 PER DAY.. NA WANAPEWA USAFIRI, NYUMBA BURE..

EWURA WALIPELEKA MAPENDEKEZO YA MISHAHAHARA YAO NAKUMBUKA KIMA CHA CHINI NI 5M

BADALA YA KUTAKA SERIKALI ISHUSHE MISHAHARA NI VEMA KUISHAWISH IPANDISHE NA KUPUNGUZA GAPE.
 
Mkuu mimi binafisi kwa ufundi wangu ukinilipa 2m kwa mwezi siwezi njoo kwenye ujasiriamali mkuu hoyo pesa utaona kawaida sanaaaaaa..
 
Millioni 1.35 ni mshahara wa kufuru? Kweli tunatofautiana.watu wanalipwa dola 25000 ambayo ni kama millioni 40 kwa mwezi endelea kulalamika na vyeti vyako
Ila sio kwa serikali ya Tz mkuu
 
Mleta maada yuko sahihi,naweza kumwelewa kwani hata kwenye sector binafsi hususani benki za kigeni ni tatizo sana
Mfano mimi mwenyew binafsi nina shahada ya uhasibu nasimamishwa dirishani tangu saa 8:30 hadi saa 06:00 nakula vumbi la hela naishia kuambulia 450k per month,hapo lazima 1.53m nione kufuru
Pole chief
Pambana na hali yako...
 
Wakuu, hii mamlaka ya serikali inayoendeshwa kwa kodi za wavuja jasho ina unyeti sana kiasi cha watumishi wake kuenjoy pepo duniani?

Cjajua Taasisi zingine kama TRA mishahara yao ikoje ila nimeijua mishahara ya SUMATRA hadi nimeshangaa. Huenda sijafahamu unyeti wa mamlaka hii ila wanaoijua watatueleza.

Rafiki yangu amemaliza pale IFM akichukua Accouting, amepata ajira mwanzoni mwa mwaka huu katka mamlaka ya SUMATRA na kwa macho yangu amenionyesha Salary Slip yake daah, ni Milioni 1.53 kwa mwezi.

Wakuu hii mishahara inapangwa na ofisi ya utumishi au wanajipangia wafanyakazi wenyewe wa Mamlaka?

Mkuuu nina hitaji kijana kama ww mwenye mawazo hayo nikuajiri, nitumie CV yako.
 
Wakuu, hii mamlaka ya serikali inayoendeshwa kwa kodi za wavuja jasho ina unyeti sana kiasi cha watumishi wake kuenjoy pepo duniani?

Cjajua Taasisi zingine kama TRA mishahara yao ikoje ila nimeijua mishahara ya SUMATRA hadi nimeshangaa. Huenda sijafahamu unyeti wa mamlaka hii ila wanaoijua watatueleza.

Rafiki yangu amemaliza pale IFM akichukua Accouting, amepata ajira mwanzoni mwa mwaka huu katka mamlaka ya SUMATRA na kwa macho yangu amenionyesha Salary Slip yake daah, ni Milioni 1.53 kwa mwezi.

Wakuu hii mishahara inapangwa na ofisi ya utumishi au wanajipangia wafanyakazi wenyewe wa Mamlaka?
hiyo pesa ya kawaida kwa agency nyingi za serikali sumatra, tanroads, nssf, tbs na nyingine afu hiyo pesa si kubwa ingawa pia si haba hata kidogo...
 
Yan M ndio mshahara kufuru, watu mnapenda kupunjwa daaah, me nawajua watu wanalipwa mpaka 15 M na ni wabongo hapa hapa...


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Huo mshahara mbona mdogo sana kwa mamlaka kama hiyo ila kwa jobless ni mkubwa sana.
 
Back
Top Bottom