Mishahara ya SUMATRA kufuru

Mimi napata 6m kwa mwezi wewe unasema 1m?

hakuna aliekuuliza mshahara wako ni kiasi gani, na hiyo haituhusu. Soma uzi kwa umakini ujue lengo lake ni nini?
Naona wewe na wengi wa wachangiaji hapa mna tatizo la kukurupuka, kwa mtazamo wangu hapa jamaa anajaribu kuikosoa serikali kwa kupendelea baadhi ya taasisi kimaslahi. Inawezekana sumatra wanamaslahi mazuri zaidi ya taasisi alieko yeye, wakati wote wanaelimu sawa na mwajiri wao ni mmoja. Sidhani kama jamaa anashangaa hizo 1.53m au hata hizo chenji zako 6m.
Tujifunze kutokukurupuka tunapochangia, after all you have an ample time to think before start writing!!
 
kaka mbona hata sisi wa Halmashauri tunapaswa kulipwa mishahara zaidi ya hiyo sema basi tu hatujengi hoja nzuri Serikalini,nimewahi kusikia NSSF kwa anayeanza na kazi anachukua around 2.4M kwa graduate,hiyo ni kwa kuwa wamejenga hoja
 
co tatzo lake ndo katoka chuo jaman bado yuko polin na rambo ya nguo
 
hahahahaha kaazi kweli,mie ukiniita kwenye usahili ukaniuliza mshahara huwa naanzia milioni 7 halafu nakuonesha kwanini iwe milioni 7!
nadhani baada ya muda itakuwa zaidi ya hapo.
Sasa we jamaa utakufa kwa presha,huo mshahara ni mdogo sana labda kama haujui unachokifanya kwenye kazi yako
 
watu unamshambulia mtoa.mada ila point yake ni utofauti wa mIshahara baina ya watumishi wa umaa..wote elimu sawa ila Huyo wa Sumatra analipwa 1.53mil wakati mhasibu wa halimashauri ana TGS D 625,000 yaani hata nusu hajamfikia..hata kama tofauti ilitakiwa iwepo ila si kwa kiwango hicho..ikiwa wote wanalipwa kwa pesa ya Kodi.
 
Mimi nakumbuka nilikosa kazinbaada ya kutaja mshahara mdogo
 
 
Huo ni mshahara kwa wafanyakazi wa
kawaida wa Bakhresa Group of Company.(azam)
Hivyo basi kwa mamlaka kama hiyo wanastahili kuongezewa zaidi.
 
Anatakiwa aongezewe
lakini sio mtu anaelipwa zaidi asimangwe.
Nchi kama Tanzania ina uwezo, ni Taifa lisilofilisika.
 

Uko sahihi kabisa mantiki ya mtoa mada naamini ilikuwa ndo hiyo
 
Mbona mshahara mdogo sana huo.

Kuna watu nchi hii wanapokea milioni 40 kwa mwezi wameajiriwa.


Hao wanaolipwa 40 millions kwa mwezi wana sifa zinazofanana na huyu rafiki wa mtoa mada?? Yaan wameajiriwa mwanzoni mwa mwaka huu, wana bachelor degree kama huyu na wanafanya kazi kwenye taasisi za umma kama huyu???
 


Well said!!
 
Labda yupo kijijini jamani msishangae kule shs 500/-bado ina sound ukiwa na note ya alfu 10 unaangaliwa mara 2/2
 
Nikupe tu tuisheni kidogo. Unaposema mshahara mkubwa lazima useme relative to wapi maana hata miashahara ya TRA umesema huijui. Leta comparison ambayo ipo relativbe na mamlaka zingine za serikali ndo utaeleweka zaidi. Mishahara ya mamlaka zote za serikali na taasisi za serikali kwa kawaida ndo huanzia range hizo. Mishahara yao ipo tofauti na Central Government. Mhasibu wa hazina anapokea mshahara mdogo zaidi ya mhasibu wa TRA. Kwa hiyo bado sijaona point ya post yako:biggrin1:
 
Muache kushabikia vitu kosiasa mm sumatra na dactari yupi wa muhimu ???ujinga ujinga tuuu
 
Nawasiwasi na taarifa hii,sidhani kama SUMATRA wako vizuri kuliko TPDC labda huyo jamaa ana miaka kadhaa kazini au cheo chake ni kuanzia Afisa Mwandamizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…