Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
Kila Kona ya nchi Sasa ni mtetemo na mtikisiko ikienda sambamba na tabasamu la kumalizika Kwa miradi iliyoanzishwa wakati wa utawala wa Hayati Magufuli. Ni juzi tumeambiwa mtambo namba 8 wa kuzalisha umeme katika bwawa la JNHPP umewashwa na kuwashwa huko tatizo la umeme litapungua Kwa 85% ,hii ni habari njema na ya matumaini makubwa. Hamu inaendelea kuwa kubwa endapo mitambo yote 9 ikiwashwa na kuanza kuzalisha umeme ,Je matokeo yake yatakuwaje?
Hilo likiwa halijakauka ,habari njema zaidi ni kuanza Kwa majaribio ya SGR kutoka Dar mpaka Moro, majaribio ambayo yamefanyika Kwa mafanikio. Kuanza kufanya kazi Kwa SGR uchumi wa Tanzania utafunguka Kwa kiwango kikubwa.
Miradi hii ,wa kufua umeme na SGR ni pigo litakaloikumba upinzani na Kwa sababu hawaoni wataendelea kuona watanzania wanataka maandamano. Watanzania wanataka maendeleo na maendeleo yanayoletwa na Serikali ya CCM ni ya vizazi Kwa vizazi.
Miradi mikubwa yote ambayo hapo kabla ili " white elephant projects" na wapinzani Sasa imekuwa miradi yenye matokeo mazuri kwenye uchumi. Miradi hiyo itautesa upinzani Kwa miaka mingi sana na kama upinzani wataendelea kuzurura bila ajenda ,sioni mwisho kwao.
Mwenyezi Mungu mpe pumziko jema mja wako , matokeo ya kazi ngumu Kwa nchi hii tumeanza kuyaona Sasa.
Hilo likiwa halijakauka ,habari njema zaidi ni kuanza Kwa majaribio ya SGR kutoka Dar mpaka Moro, majaribio ambayo yamefanyika Kwa mafanikio. Kuanza kufanya kazi Kwa SGR uchumi wa Tanzania utafunguka Kwa kiwango kikubwa.
Miradi hii ,wa kufua umeme na SGR ni pigo litakaloikumba upinzani na Kwa sababu hawaoni wataendelea kuona watanzania wanataka maandamano. Watanzania wanataka maendeleo na maendeleo yanayoletwa na Serikali ya CCM ni ya vizazi Kwa vizazi.
Miradi mikubwa yote ambayo hapo kabla ili " white elephant projects" na wapinzani Sasa imekuwa miradi yenye matokeo mazuri kwenye uchumi. Miradi hiyo itautesa upinzani Kwa miaka mingi sana na kama upinzani wataendelea kuzurura bila ajenda ,sioni mwisho kwao.
Mwenyezi Mungu mpe pumziko jema mja wako , matokeo ya kazi ngumu Kwa nchi hii tumeanza kuyaona Sasa.