Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Magufuli kwa miaka 5 aliyokaa madarakani alikopa trillion 37 akajengea SGR, bwawa la Nyerere, akanunua ndege, Kijazi interchange ubungo na 6 way mpaka Mbezi mwisho.
Magufuli hata kama aliiba lakini angarau alionyesha matokeo ijapo aliwadanganya wananchi kuwa matokeo hayo ni pesa zetu wenyewe wakati zilikuwa za mkopo.
Samia kwa miaka mitatu kakopa trillion 30 pesa kapeleka wapi? Miradi aliyoiacha Magufuli mingi ni kama imekwama.
SGR yenyewe inasua huku wafanyakazi wakifanya migomo kwa kutolipwa mishahara yao. Upande wa pili tren yenyewe ya SGR imechakachuliwa, tumeletewa tren iliyotumika kwenye movie ya Escape From Sobibor mwaka 1987 tukaambiwa ni tren ya mwendokasi. Ni juzi tu kwenye majaribio yao kutoka Dar mpaka Morogoro tren hiyo ilitumia takribani masaa manne sehemu ambayo ilitakiwa kutumia lisaa limoja. Kwa ufupi ni kwamba ukitaka kufika haraka ni heri upande Ngorika kuliko hili tren la Escape From Sobibor.
Sasa kwa mazingira haya ya utawala wa Samia wa kukopakopa na pesa zinaishia kuibiwa kwanini tusimuambie ajiuzulu? Binafsi naona Samia uwezo wake wa kiutendaji ni mdogo fikiria naye analalamika pesa zinaibiwa na yeye ndio mwenye mamlaka kikatiba kulinda pesa za umma na rasilimali za taifa.
Sasa ni muda wa kumlazimisha Samia ajiuzulu kupitia maandamano.
Asante.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Magufuli hata kama aliiba lakini angarau alionyesha matokeo ijapo aliwadanganya wananchi kuwa matokeo hayo ni pesa zetu wenyewe wakati zilikuwa za mkopo.
Samia kwa miaka mitatu kakopa trillion 30 pesa kapeleka wapi? Miradi aliyoiacha Magufuli mingi ni kama imekwama.
SGR yenyewe inasua huku wafanyakazi wakifanya migomo kwa kutolipwa mishahara yao. Upande wa pili tren yenyewe ya SGR imechakachuliwa, tumeletewa tren iliyotumika kwenye movie ya Escape From Sobibor mwaka 1987 tukaambiwa ni tren ya mwendokasi. Ni juzi tu kwenye majaribio yao kutoka Dar mpaka Morogoro tren hiyo ilitumia takribani masaa manne sehemu ambayo ilitakiwa kutumia lisaa limoja. Kwa ufupi ni kwamba ukitaka kufika haraka ni heri upande Ngorika kuliko hili tren la Escape From Sobibor.
Sasa kwa mazingira haya ya utawala wa Samia wa kukopakopa na pesa zinaishia kuibiwa kwanini tusimuambie ajiuzulu? Binafsi naona Samia uwezo wake wa kiutendaji ni mdogo fikiria naye analalamika pesa zinaibiwa na yeye ndio mwenye mamlaka kikatiba kulinda pesa za umma na rasilimali za taifa.
Sasa ni muda wa kumlazimisha Samia ajiuzulu kupitia maandamano.
Asante.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.