Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Heshima mbele..... Nilikuwa napitia magazeti nianze wiki nikakuta hii article inayohusu uboreshaji wa mikataba ya madini as commented/suggested by Mhuu wa Mkoa wa Arusha (prev in Mara).... Aisee kuna viwili hapo:
1. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kidogo upeo wa kuelea ni mdogo, au
2. Mwandishi wa habari hii ameleta part tu ya ushauri/jibu.

Hii ni sababu anaposema kuwepo na mTanzania katika kila mradi/mkataba wa madini amesahau/hajui kuna makundi matatu ya waTanzania katika miradi hii:
1. Kundi la kwanza ambalo ni kubwa ni "Wadanganyika" - Hawa ni wale wavuja jasho wa migodini ambao wanalipwa peanuts
2. Kundi la "Mafisadi" - Hawa ni wale waliotoa michongo kwa wawekezaji na kupewa 10% (or so commission/asante) kwa kuwachinja Wadanganyika
3. "Walaji kiulaini/ Watendaji" - Hawa ni wale ambao wanajaribu kuwatetea Wadanganyika lakini tatizo ni kwamba nao wana njaa so wakitaka kupioga kelele wanapewa cha juu au vijiposting serikalini/kwenye makampuni hayohayo kisha wanatulia!!!

Sasa Mhe Mkuu wa Mkoa alitakiwa awe muwazi na mkweli katika kuliongelea hili sababu kusema peke yake that '"Lazima awepo mTanzania katika kila mradi pekee" ni very VAGUE point ambayo being Mkuu wa Mkoa (miwili tayari na vijiposti vingine) inanifanya nishindwe kutambua uelewa na ufahjamu wa mzee wetu......

http://www.ippmedia.com/ipp/itv/2008/01/23/106883.html
 
Wanabodi:

Kama kuna chanzo cha uhakika cha mikataba mibovu basi ni ofisi ya mwanasheria mkuu!!!

  • Ofisi ya mwanasheria mkuu ndiyo yenye majukumu ya kuangalia ku-authenticate kuwepo au kutokuwepo kwa kampuni iwe feki au halali
  • Ofisi ya mwanasheria mkuu ikisema jambo hakuna waziri au mamlaka nyingine yeyote yenye uwezo wa kufanya tofauti. hatukuona ikithubutu kusema lolote kwenye hili la RICHMOND
  • Kwenye issue ya RICHMOND ni Tanesco iliyoonyesha umakini, wakati ofisi ya mwanasheria mkuu ikiwa imenyamaza kimya!
  • Hata hela BOT zisingekwibwa kama wanasheria wangekuwa makini na kazi zao
  • Kitivo cha sheria cha UDSM, kitivo cha kwanza kabisa cha UDSM kimeabishwa na matokeo ya graduates wake ku-saini utumbo!!
  • Tunaomba chama cha wanasheria (TLS) kitoe tamko kuhusu utendaji dhaifu wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.
  • Tunaomba Kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha Dar es Salaam kitoe karipio kali kwa wanasheria wake waliohusika kwenye mikataba mibovu.
  • Mwanasheria mkuu wa serikali alistahili kuwa mtu wa kwanza kuachia ngazi na kuomba msamaha kwa kusababisha waziri mkuu na mawaziri wawili kuachia ngazi...kwa kuwa ofisi ile ingefanya kazi yake... basi tusingeingia mkataba na non-existence company...
  • Ofisi hiyo ndiyo yenye kuangalia risk za mikataba kwa taifa...

Inawezekana nimepitiwa na jambo,,, naomba kusaidiwa wapi kamati ya Dr. Mwakyembe ilionyesha kwamba ofisi ya mwanasheria mkuu iishauri serikali iisiingie mkataba na Richmond, kampuni ambayo inasemekana haipo?

Kumbukeni:

Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali...
1. Mjumbe kwenye baraza la mawaziri
2. Mjumbe kwenye GNT
3. Mjumbe sijui kamati ya ....

Kila mahali ilikuwepo
 
Kwa waliosikiliza hotuba ya Dr Slaa bungeni jana watakuwa wamesikia akimtaja huyu mama (correct me kama nimekosea jina)Kwamba anahusika na process fulani za mikataba kusainiwa. Kama kuna mtu mwenye information zaidi aziweke tujue role yake na yeye maana Slaa mpaka kamtaja kwamba amesahauluka kwenye repot ya Richmond inaonekana kuna jambo. Bora tuanze tusiwe caught unaware. Nimekuwa curious baada ya kusikia Slaa anamtaja na kusuggest achunguzwe so msiniambie lete ushahidi and all that.
 
Ni kweli Dr.Slaa alimtaja huyo mama tena mara mbili baada ya kukosea mara ya kwanza. Sina info zozote za huyu mama, hila naamini mpaka ametajwa kuna jambo. wenye info tuleteeni hapa tuzifikishe kunako stahili
 
huyu mama alishausika na dudu moja hapo nyuma(tulishalijadili wakati fulani hapo kale bcs)lilio tuletea IPTL,sijui sie wadanganyika tumemkosea nini huyu mama maanake kila kukicha anatulubuni kwenye nishat,dude lenyewe nazani ndio hata Mhe Slaa alikuwa anamaanisha jana wakati akimtaja,dude lenyewe refu kama ifuatavyo(kumradhi).......

THE POWER AND THE VAINGLORY:

Anatomy of a $100 Million Malaysian IPP in Tanzania

Brian COOKSEY

Rutabanzibwa's former assistant, Prosper Victus, also testified that he was offered a similar amount to keep key information from Rutabanzibwa. Victus also implicates Mary Ndosi (later Maria Kejo), the state attorney who endorsed the IPTL contract on behalf of the government: ‘When she telephoned me, Mrs Ndosi said … that "we want you to help us get this power project approved" and then she reminded me that Mr Rugemalira would give me 100,000,000 Tanzanian Shillings if the IPTL project were approved. I was shocked to learn that Mrs Ndosi had apparently been corrupted by Mr. Rugemalira.' (Witness Statement, 19 April 2000, p. 3).

Another former assistant, Esther Mzunzu, testified to the Prevention of Corruption Bureau that she accepted a bribe from Rugemalira, albeit a rather small one. She alleges that Rugemalira came to her office sometime in December 1994 and said: "If our proposal goes through, I can give you money. How about $20,000?" She claims that she refused, but later accepted Shs100,000. Her generally pro-IPTL behaviour suggests that, if she only received Shs100,000, she was cheap at the price.

In a long letter to Attorney General Andrew Chenge, Rugemalira defends himself against these accusations and claims, as he has done many times before, that there is a conspiracy between Songas and the World Bank to drive him out of the market. He also announces his intention to sue Rutabanzibwa, Victus and Masunzu for personal defamation. Unless IPTL wins the arbitration case, James Rugemalira's days of unbridled hubris are behind him, and it would serve as an object lesson to like-minded international corrupters if the roles of Wärtsilä, Mechmar, Sime Bank, and Bank Bumiputra in this entirely unseemly saga were to be fully investigated.
 
Last edited by a moderator:
huyu mama,hafai,yuko pia kule buzwagi,yuko kila kona ya madudu,yuko tics,kinachouma zaidi nikwamba yumo pia kwenye ile tume ya raisi na klina zito kabwe,hapo ndipo nachoka kabisaa.
 
Nafikiri jina sahihi la huyu mama ni Maria Kejo (zamani Mary Ndosi)! Sijui vizuri historia ya yake ndani ya Serikali na issues za Mikataba!! Lakini kufuatana na lidocument hapo juu kwa Shukurani, alikuwa ni State Attorney in Cheng's office na ndiye aliye apparaise contract baina ya Governmnet na IPTL kwa niaba ya serikali,na kusema haina matatizo baada ya kupewa hongo na James Rugemalira, pia ilimshawishi kijana mwingine (Victus) kutunza taarifa za akina Rugemalira kwa kuahidiwa kupewa Tshs 100,000,000.

Kutokana na hilo document hapo juu, huyu mama anaonekana ni hatari sana kwa taifa hili!
Naomba kama kuna mtu mwenye in and outs za huyu mama azimwage hapa ili tuone kama anaonewa au ni moja wa maengineer wa ufisadi kama alivyo tajwa na Dr.Slaa!

festog
 
Kama alihusika kwenye Mkataba wa Dudu IPTL kama alivyodai Dk. Slaa basi huyo mama anafahamika vema na aliyekuwa Waziri wa Wizara husika Mhe. Rais JK.

Pili, kwa huyu mama kutajwa kwenye Tume Teule ya Bunge ya Dk. Mwakyembe basi TAASISI YA KUENDELEZA NA KUPAMBA RUSHWA (TAKUKURU)ilitakiwa iwe imeanza kazi ya kumfuatilia huyu mama.
 
Kama mheshimiwa JK anamfahamu vizuri huyu mama, inakuwaje jamaa kamteua kwenye ile tume???

Hapo ndo JK anaponiachaga hoi......Kusema kweli mpaka tuje tutoke kwenye haya matatizo ya ufisadi tuna safari ndefu, tatizo naliona bado lipo....
 
Huyu mama ni mkongwe.. kwanza yeye ndio ilikua awe AG badala ya mwanyika but she is smart.. Alikataa. Hataki kuwa kwenye lime light.. Anapesa nyingi kuliko mawaziri wengi. Senior state attorney.. kuna scandal moja ya loliondo-gate... nayo alihusika. inshort ameoza... hafai. Alikua anawekewa kifua na EL maana alikua samsingi yake long taimu marehemu muwewe Meja Moses Ndosi akiwa rafiki wa Edward Lowassa. Anaconnections nyingi na nimkongwe kweli kweli..
 
Wanabodi:

Kama kuna chanzo cha uhakika cha mikataba mibovu basi ni ofisi ya mwanasheria mkuu!!!

  • Ofisi ya mwanasheria mkuu ndiyo yenye majukumu ya kuangalia ku-authenticate kuwepo au kutokuwepo kwa kampuni iwe feki au halali
  • Ofisi ya mwanasheria mkuu ikisema jambo hakuna waziri au mamlaka nyingine yeyote yenye uwezo wa kufanya tofauti. hatukuona ikithubutu kusema lolote kwenye hili la RICHMOND
  • Kwenye issue ya RICHMOND ni Tanesco iliyoonyesha umakini, wakati ofisi ya mwanasheria mkuu ikiwa imenyamaza kimya!
  • Hata hela BOT zisingekwibwa kama wanasheria wangekuwa makini na kazi zao
  • Kitivo cha sheria cha UDSM, kitivo cha kwanza kabisa cha UDSM kimeabishwa na matokeo ya graduates wake ku-saini utumbo!!
  • Tunaomba chama cha wanasheria (TLS) kitoe tamko kuhusu utendaji dhaifu wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.
  • Tunaomba Kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha Dar es Salaam kitoe karipio kali kwa wanasheria wake waliohusika kwenye mikataba mibovu.
  • Mwanasheria mkuu wa serikali alistahili kuwa mtu wa kwanza kuachia ngazi na kuomba msamaha kwa kusababisha waziri mkuu na mawaziri wawili kuachia ngazi...kwa kuwa ofisi ile ingefanya kazi yake... basi tusingeingia mkataba na non-existence company...
  • Ofisi hiyo ndiyo yenye kuangalia risk za mikataba kwa taifa...

Inawezekana nimepitiwa na jambo,,, naomba kusaidiwa wapi kamati ya Dr. Mwakyembe ilionyesha kwamba ofisi ya mwanasheria mkuu iishauri serikali iisiingie mkataba na Richmond, kampuni ambayo inasemekana haipo?

Kumbukeni:

Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali...
1. Mjumbe kwenye baraza la mawaziri
2. Mjumbe kwenye GNT
3. Mjumbe sijui kamati ya ....

Kila mahali ilikuwepo

Hakuna mahali ambapo kamati imeonyesha jinsi Mwanyika livyoishauri sirikali kuhusu mkataba ule. Inaonekana kabisa kwamba Mwanyika alikwepa majukumu yake ya kusimamia mikataba hii, kwa hiyo anapaswa kupatilizwa kwa mujibu wa sheria! Nashangaa kwa nini mpaka sasa hajasikika kutangaza kuachia ofisi.
 
Pinda: Waliosani mikataba kushughulikiwa

na Charles Ndagulla
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


SERIKALI imeweka wazi msimamo wake kuwa viongozi wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine kwenye kashfa ya kuingia mikataba mibovu iliyoligharimu taifa mambilioni ya shilingi, watawajibishwa bila kuonewa haya wala huruma.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini hapa na Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Pinda, katika ibada ya misa ya kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kwa Askofu Mteule wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Moshi, Isaac Amani, aliyechukua nafasi ya Askofu Amedeus Msarikie.

Alisema kuwa mikataba yote iliyosainiwa na vingozi waliokuwa madarakani, imeundiwa tume zinazochunguza kama mikataba hiyo ina maslahi kwa taifa.

Hivi karibuni, aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, alilazimika kujiuzulu wadhifa wake baada ya kuhusishwa na kashfa ya mkataba wa uzalishaji umeme wa dharura, uliosainiwa na serikali na kampuni ya Marekani ya Richmond.

Pamoja naye - Nazir Karamagi aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, na mtangulizi wake (Nazir), Dk. Ibrahim Msabaha - nao walijiuzulu nyadhifa zao baada ya Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mkataba huo, chini ya uenyekiti wa Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela-CCM), kubaini kuwa walihusika kwa namna moja ama nyingine kuliingiza taifa katika mkataba wa hasara.

Hata hivyo, Pinda alisema kuwa kuvunjwa na kuundwa kwa Baraza jipya la Mawaziri bila kuwapo na machafuko yoyote kulitokana na dua na maombi kutoka kwa viongozi wa madhehebu ya dini yaliyomwezesha Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko hayo kwa busara, amani na utulivu.

Waziri Pinda alitoa wito kwa viongozi wa madhehebu ya dini kote nchini kuendelea kuiombea Tanzania amani ya kudumu, na pia kuombea kurejea kwa amani katika nchi jirani ya Kenya, iliyokumbwa na machafuko ya kisiasa, kutokana na kutokubalika kwa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.

Machafuko hayo yamesababisha watu wapatao 1,000 kuuawa na maelfu kuyahama makazi yao baada ya nyumba zao kuchomwa moto.

Waziri Mkuu Pinga, ambaye katika sherehe hizo alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete, alipongeza mchango mkubwa unaotolewa na madhehebu ya dini katika maeneo mbalimbali ikiwamo elimu, afya, maji na uhifadhi wa mazingira.

Alitolea mfano wa matokeo ya mtihani wa Kidato cha Nne ambako shule nyingi zinazomilikiwa na kuendeshwa na madhehebu ya dini zilifanya vizuri. Hata hivyo, alitoa wito kwa taasisi hizo kutoa huduma ya elimu kwa gharama nafuu.

“Huu ni udhibitisho kwamba madhehebu ya dini yako mstari wa mbele katika kuwapa maisha bora Watanzania, mnatoa changamoto si kwa serikali tu bali hata kwa sekta binafsi nyingine zinazoshughulika na elimu,” alisema.

Alisema kuwa Askofu Amani amepewa uongozi huku nchi ikikabiliwa na changamoto katika elimu, afya, maji, watoto yatima, wenye ulemavu pamoja na suala zima la janga la ukimwi.

“Changamoto hizi zinatupa vigezo vya kupima juhudi na uwezo wetu kama viongozi wa serikali na viongozi wa dini katika kuhudumia jamii. Katika elimu, tunayo changamoto ya kupeleka watoto takriban 419,136 waliofaulu mtihani wa Darasa la Saba kujiunga na Kidato cha Kwanza,” alisema.

Aidha, alibainisha kuwa takwimu zinaonyesha kuwa ni wanafunzi 396,068 ndio wanaotarajiwa kupata nafasi ya kujiunga na Kidato cha Kwanza, hivyo wanafunzi 26,586 kuwa katika hatari ya kukosa nafasi.

Kuhusu janga la ukimwi, alisema kuwa takwimu za makadirio ya mwaka 2007 zinaonyesha kuwapo kwa takriban watu 400,000 huku yatima wanaotokana na janga hilo la ukimwi wakikadiriwa kufikia 700,000 na idadi ya vifo kuongezeka hadi kufikia 187,000.

 
Waziri Mkuu mara baada ya kupitishwa alisema "yaliyopita si ndwele, tugange yajayo" kuhusu swala hili, leo anakuja na statement tofauti bila hata ya kuielezea statement yake ya kwanza.

Viongozi wetu wana matatizo ya kujisemea mambo bila kupanga wala consultation, sasa tuelewe kipi? Yaliyopita si ndwele au waliosaini mikataba watashughulikiwa? Au ile "yaliyopita si ndwele" ilikuwa kwa mkulu Lowassa tu na hivi vidagaa vingine tutavitoa bangusilo?

Inabidi kauli za viongozi wa kitaifa zipimwe kabla ya kufakamia vinasa sauti, mara nyingine "no comment" au tunajadiliana cha kufanya" inatosha, otherwise ndiyo mambo haya ya flip flopping na mixed signals katika jitihada za kum please kila mtu while hakuna cha maaana kinachofanyika.

Mpaka nitakapoona watu wanashughulikiwa mi naona haya ni mazungumzo baada ya habari tu, in other words populist propaganda.
 
Waziri Mkuu mara baada ya kupitishwa alisema "yaliyopita si ndwele, tugange yajayo" kuhusu swala hili, leo anakuja na statement tofauti bila hata ya kuielezea statement yake ya kwanza.

Viongozi wetu wana matatizo ya kujisemea mambo bila kupanga wala consultation, sasa tuelewe kipi? Yaliyopita si ndwele au waliosaini mikataba watashughulikiwa? Au ile "yaliyopita si ndwele" ilikuwa kwa mkulu Lowassa tu na hivi vidagaa vingine tutavitoa bangusilo?

Inabidi kauli za viongozi wa kitaifa zipimwe kabla ya kufakamia vinasa sauti, mara nyingine "no comment" au tunajadiliana cha kufanya" inatosha, otherwise ndiyo mambo haya ya flip flopping na mixed signals katika jitihada za kum please kila mtu while hakuna cha maaana kinachofanyika.

Mpaka nitakapoona watu wanashughulikiwa mi naona haya ni mazungumzo baada ya habari tu, in other words populist propaganda.

Wao walidhani kubadilisha baraza la mawaziri ndio kutawaridhisha Watanzania kuhusiana na kashfa hizo. Sasa wamegundua Watanzania wale wa mwaka 47 ambao walikuwa hawashinikizi chochote dhidi ya kashfa mbali mbali serikalini siyo sawa na Watanzania wa mwaka 2008. Tunasubiri kuona wahusika wote wa kashfa za BoT, mikataba ya madini, Richmond n.k. wanafikishwa mahakamani na hatimaye kufilisiwa.

Tumechoka kuona Watanzania walio wengi wakiishi maisha ya dhiki miaka nenda miaka rudi wakati 'viongozi' wachache wenye uroho wa utajiri wa haraka haraka wakiendelea kuwa mabilionea kupitia nyadhifa zao tulizowakabidhi.
 
Nina nukuu "Mikataba yote iliyosainiwa na viongozi walioukwa madarakani inaundiwa tume kuchunguza kuona kama ilikuwa na maslahi kwa taifa",mwisho wa kunukuu.

Tume juu ya tume, ndani ya tume, zidi ya tume, tume tume tume tume mpaka mwisho wa dunia.

Tume ya Mwakyembe ilichokifanya kimefanyiwa kazi?. Ama nini lengo la tume ya Mwakyembe?. Lengo halikuwa kuunda tume nyingine kuchunguza yale yaliyochunguzwa.

Mungu tumekosa nini Watanzania mpaka ukatupa akili za kuazima?
 
Waziri Mkuu mara baada ya kupitishwa alisema "yaliyopita si ndwele, tugange yajayo" kuhusu swala hili, leo anakuja na statement tofauti bila hata ya kuielezea statement yake ya kwanza.

Viongozi wetu wana matatizo ya kujisemea mambo bila kupanga wala consultation, sasa tuelewe kipi? Yaliyopita si ndwele au waliosaini mikataba watashughulikiwa? Au ile "yaliyopita si ndwele" ilikuwa kwa mkulu Lowassa tu na hivi vidagaa vingine tutavitoa bangusilo?

Inabidi kauli za viongozi wa kitaifa zipimwe kabla ya kufakamia vinasa sauti, mara nyingine "no comment" au tunajadiliana cha kufanya" inatosha, otherwise ndiyo mambo haya ya flip flopping na mixed signals katika jitihada za kum please kila mtu while hakuna cha maaana kinachofanyika.

Mpaka nitakapoona watu wanashughulikiwa mi naona haya ni mazungumzo baada ya habari tu, in other words populist propaganda.

......pamoja na kusema yaliyopita si ndwele tugange yajayo sidhani kama alimaanisha kuwa issues ata stake ndiobasi..............MP alisema pia kuwa mapendekezo ya tume yatafanyiwa kazi...isipokuwa mengine yatachukua muda......

kinachonishangaza.......hizo hasara anazozichunguza hivi sasa ni zipi tena, wakati tume ilishamuambia tunaingia hasara ya 152 million per day???!!!!!!!...na waliohusika na mikataba wametajwa.........

MP ondoa hao kwa manufaa ya umma.....PERIOD
 
Hii ngoma bado ni mbichi kabisa, inakuwaje hadi hivi sasa hakuna aliyeshitakiwa kwa uhujumu wa mali ya taifa? Inakuwaje waziri mkuu aliyejiuzulu bado kufikishwa mahakamani? Inakuwaje Karamagi bado anapeta tu wakati mkataba aliosaini unamneemesha yeye binafsi na tumbo lake?

Wako wapi wale waliopewa dhamana ya kuona haki inatendeka?
 
Pinda ni Mkatoliki tena naambiwa ni Mseminary sijajua kasoma wapi maana hata sijahangaika kutaka kujua katokea wapi maana la maana kwangu ni Tanzania kuwa na hali njema basi .

Pinda alikuwa akiongea haya mbele ya Maaskofu ambao anajua wana ujuzi mkubwa wa mambo .Ila nina wasi wasi pia wanaweza wakawa ni mafisadi vile vile kama wale wa KKT ambao sasa wanalia na Lowasa.Pinda ujue kwamba kila usemalo sisi tunaliweka katika kumbukumbu na tutakuuliza muda mfupi ujao .
 
......pamoja na kusema yaliyopita si ndwele tugange yajayo sidhani kama alimaanisha kuwa issues ata stake ndiobasi..............MP alisema pia kuwa mapendekezo ya tume yatafanyiwa kazi...isipokuwa mengine yatachukua muda......

kinachonishangaza.......hizo hasara anazozichunguza hivi sasa ni zipi tena, wakati tume ilishamuambia tunaingia hasara ya 152 million per day???!!!!!!!...na waliohusika na mikataba wametajwa.........

MP ondoa hao kwa manufaa ya umma.....PERIOD

Ogah,

Tatizo linakuja "yaliyopita si ndwele" na "mapendekezo ya tume yatafanyiwa kazi" ni kauli mbili contradictory.Which is exactly my point, inabidi wawe makini na kauli zao sio kujisemea mambo kwa vi-methali vague tu kisha kuji contradict.

Kwangu mimi "yaliyopita si ndwele" maana yake "let's forget what happenned, let's start afresh" (if not then ni ndwele).Sasa kama yaliyopita si ndwele mapendekezo ya tume yanafanyiwa kazi ili iweje na kwa sababu gani?

Foot-in-mouth disease inaanza mapemaaaaaa!
 
Ogah,

Tatizo linakuja "yaliyopita si ndwele" na "mapendekezo ya tume yatafanyiwa kazi" ni kauli mbili contradictory.Which is exactly my point, inabidi wawe makini na kauli zao sio kujisemea mambo kwa vi-methali vague tu kisha kuji contradict.

Kwangu mimi "yaliyopita si ndwele" maana yake "let's forget what happenned, let's start afresh" (if not then ni ndwele).Sasa kama yaliyopita si ndwele mapendekezo ya tume yanafanyiwa kazi ili iweje na kwa sababu gani?

Foot-in-mouth disease inaanza mapemaaaaaa!

agreed Pundit...............its very contradicting, nilimsamehe apale aliposema "mimi sio mwanasiasa".....then nika-assume alichosema sicho alichomaanisha

Ikifika wakati muafaka itabidi tumuwezeshe Mwanakijiji amuhoji MP pamoja na mambo mengine
 
Back
Top Bottom