Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Ngeleja aambiwa mikataba itamletea shida

Mgaya Kingoba, Dodoma
Daily News;
Sunday,April 20, 2008


MBUNGE wa Longido, Michael Laizer (CCM), amesema utekelezaji wa Muswada wa Umeme wa mwaka 2007, utakuwa kipimo cha Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, vinginevyo utamletea shida.

Akichangia majadiliano ya muswada huo bungeni mjini Dodoma juzi jioni, Laizer alisema wabunge sasa wameanza kuogopa miswada inayowasilishwa bungeni kwa sababu wanaipitisha kwa nia njema, lakini baadaye inazaa mikataba mibovu.

Aidha, Mbunge huyo ameahidi kwamba endapo umeme hautafika jimboni kwake ifikapo mwaka 2010, amekwisha kuwatangazia wananchi wa Longido kuwa hatawania tena kiti hicho. “Kila mkataba ni ufisadi mtupu. Hii mikataba ndiyo itakuletea shida Ngeleja.

Wananchi wamepoteza imani na mikataba hii,” alisema Mbunge huyo wa Longido na kuongeza: “Kwa mfano, sisi tunashiriki kupitisha miswada, kisha inazaliwa mikataba inatuletea matatizo. Dowans inachukua milioni 152 kwa siku, tulipitisha hapa; Meremeta Waziri wa Ulinzi alisema ni mradi wa jeshi, Meremeta leo iko wapi?

“Iundwe timu au Kamati ya Bunge, mikataba inapoandaliwa timu hiyo ishiriki kuiona na kuiangalia kama ina manufaa.” “Sisi sasa tumeanza kuogopa miswada inayoletwa bungeni. Nimepiga kelele hapa bungeni miaka 13, tangu wakati wa William Shija, Yona, Dk. Msabaha na Ngeleja huyu.

Mimi sina matumaini ya umeme. Nimewaeleza wananchi wangu kwamba kama umeme hautafika mwaka 2010, sitagombea tena ubunge,” alisema Laizer. Alisema anachangia muswada huo kwa masikitiko kwa sababu amebeba mzigo mkubwa wa kupitisha miswada ambayo ilizaa mikataba mibovu, akitolea mfano pia Kampuni ya NetGroup Solutions aliyosema badala ya kutatua matatizo ya wananchi, ilikuwa mzigo mkubwa kwao.

Aliitaka Wizara kuwa makini na mikataba itakayotokana na muswada huo na kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini. Kwa upande wake, Mbunge wa Iramba Mashariki, Mgana Msindai (CCM), alipendekeza kuundwa upya kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kwa kuanzia kwa Bodi ya Wakurugenzi.

“Wapo wafanyakazi ambao wamekulia humo, wamezeekea humo. Sisemi wote ni wabovu, lakini wapo ambao watakuwa ni kikwazo. Ni heri wakapumzike, wapewe chao wakapumzike,” alisema Msindai.

Alipendekeza shirika hilo liongezewe nguvu na fedha ili liweze kumudu ushindani utakaoanzishwa na muswada huo ambao kama ukipita, kwa mara ya kwanza Tanzania itashuhudia wawekezaji binafsi katika umeme.

Aidha, alipendekeza Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), isimamie vyema sheria, akisema, “Ikizubaa tu, tumekwisha.” Hoja yake kuhusu Tanesco iliungwa mkono na Mbunge wa Tunduru, Mtutura Mtutura, ambaye alisema alikuwa mfanyakazi wa Tanesco kwa miaka 15 na analijua vyema shirika hilo.

Alisema limefika hapo kwa kujitakia baada ya kujenga jengo la kitega uchumi kwa Sh bilioni mbili, bila ya haja hiyo; kuuza shamba la kuzalisha nguzo na sasa inazinunua kwa bei kubwa na wafanyakazi wake kununua umeme kwa bei ya kutupa huku wananchi wakiminywa. A

lisema wafanyakazi wa Tanesco wananunua umeme kwa Senti 20 wakati wananchi wanauziwa kwa Senti 165. Shirika hilo alisema lina wafanyakazi 4,670, hivyo kupoteza mamilioni ya shilingi. Mbunge wa Viti Maalumu, Margaret Mkanga (CCM), alifurahishwa na kuondolewa kwa gharama za uzalishaji (capacity charge), akisema kilikuwa chanzo kikubwa cha ulaji.

Mbunge wa Pangani, Mohamed Risherd (CCM), alitaka kupunguzwa kwa matumizi ya mafuta kwa umeme, na kupendekeza wawekezaji wadogo wasiingizwe kwenye Gridi ya Taifa.

Kwa upande wake, Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa (CCM), alisema zipo kampuni ambazo hazilipi kodi, na kuiitaka Wizara ya Nishati na Madini, kushirikiana na Wizara nyingine kuweka tozo katika kampuni hizo zikiwamo za vinywaji baridi na simu za mkononi ili fedha zitakazopatikana zipeleke umeme vijijini.

Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni (CCM), aliitaka Ewura kutoa leseni kwa uhakika ili kutowapa matapeli, huku Mbunge wa Nyang’hwale, James Musalika (CCM), naye akitaka mikataba yote ipelekwe bungeni ili wabunge waithibitishe.

Wabunge wataendelea kujadili muswada huo Jumatatu baada ya mapumziko ya mwisho wa juma na wanatarajia kumaliza Jumanne ijayo. Wabunge 50 wameomba kuchangia muswada huo ulioahirishwa mara kadhaa kusomwa bungeni kwa mara ya pili.

My TAKE:


Na nyinyi Wabunge pia ni wa kulaumiwa. Kuna ushahidi wa kutosha kwamba mikataba mingi ni ya kifisadi, lakini kila kukicha hamuhoji chochote kinachopitishwa mbele ya macho yenu. Kazi yenu kubwa bungeni ni kusifia CCM.

Mlikubali kunyamazishwa na Lowassa mlipokuwa mnahoji ufisadi wa Richmond. Hivyo na nyinyi muwe tayari kujibu maswali ya wananchi je huko bungeni mnafanya nini chenye maslahi na nchi yetu?
 

MBUNGE wa Longido, Michael Laizer (CCM),.......
Aidha, Mbunge huyo ameahidi kwamba endapo umeme hautafika jimboni kwake ifikapo mwaka 2010, amekwisha kuwatangazia wananchi wa Longido kuwa hatawania tena kiti hicho. “Kila mkataba ni ufisadi mtupu.


Mimi sina matumaini ya umeme. Nimewaeleza wananchi wangu kwamba kama umeme hautafika mwaka 2010, sitagombea tena ubunge,” alisema Laizer. Alisema anachangia muswada huo kwa masikitiko kwa sababu amebeba mzigo mkubwa wa kupitisha miswada ambayo ilizaa mikataba mibovu, akitolea mfano pia Kampuni ya NetGroup Solutions aliyosema badala ya kutatua matatizo ya wananchi, ilikuwa mzigo mkubwa kwao.


[/size][/color]



Huyu mbunge akitimiza ahadi yake hii 2010 nitamsifu sana kwa vile atakuwa amewathibitishia wananchi wake kuwa aliwadanganya wananchi na yeye kukubali kusema uwongo na kuwajibika kwayo.
 

MBUNGE wa Longido, Michael Laizer (CCM), amesema utekelezaji wa Muswada wa Umeme wa mwaka 2007, utakuwa kipimo cha Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, vinginevyo utamletea shida.

Akichangia majadiliano ya muswada huo bungeni mjini Dodoma juzi jioni, Laizer alisema wabunge sasa wameanza kuogopa miswada inayowasilishwa bungeni kwa sababu wanaipitisha kwa nia njema, lakini baadaye inazaa mikataba mibovu.

[/size][/color]


Mheshimiwa Laizer anaprove kuwa wabunge wa bunge la sasa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni incompetent ndio maana wapitisha mikataba mibovu. Ina maana huwa hawapewi copy za hii mikataba kabla ya kuijadili/kuipitisha!!!?? Kama wanapewa je huwa hawaisomi?? maswali kwa kweli ni mengi kuliko majibu. Inashangaza mtu unaposign/kupitisha kitu ambacho hukijui undani wake!
 
Mheshimiwa Laizer anaprove kuwa wabunge wa bunge la sasa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni incompetent ndio maana wapitisha mikataba mibovu. Ina maana huwa hawapewi copy za hii mikataba kabla ya kuijadili/kuipitisha!!!?? Kama wanapewa je huwa hawaisomi?? maswali kwa kweli ni mengi kuliko majibu. Inashangaza mtu unaposign/kupitisha kitu ambacho hukijui undani wake!

Bunge nafikiri hawajadili mikataba na walichokuwa wanajadili juzi was mswada wa umeme wa 2007 na sio mkataba. Kama wabunge wangekuwa wanajadili mikataba nina uhakika kusingekuwa na mikataba mibovu kama ilivyo sasa.
 
Press Release Source: Douglas Lake Minerals

Douglas Lake Minerals acquires massive 430 sq km alluvial gold deposit

VANCOUVER, May 9 /PRNewswire-FirstCall

The company is pleased to announce today that it has concluded an agreement with a Tanzanian National who holds the mineral rights to four Prospecting Licenses (PL's). The PL's cover an area of 430 square kilometers, and are situated in Mbwemkuru in the Lindi Region in Southeastern Tanzania.

The area is situated in the SE margin of the Karoo Basin, where there is an interland paleo basin comprising greater than 10 meters of gold bearing gravel and sandy material. The property is currently in small scale production by the current owner. One of the most significant prospects being a 8 km by 2km block, with high gold concentrations within 1.0 and 1.5 meter zones between the gravel's and the bedrock. Another zone, a 3 by 4 kilometer block, is covered by over 9 meters thick of gravel and sandy material from surface to bedrock. In order to determine the upside potential pertaining to these placer deposits situated in this block a systematic exploration program is planned to commence on June 1, 2008.

On a recent site visit it became obvious that the area has significant potential.

The closing date on the transaction is on or before June 30, 2008.

About Douglas Lake

DLKM is an emerging mineral exploration company focused on exploring and developing gold, copper, nickel, uranium and diamond mining opportunities in Tanzania. DLKM has a portfolio of 51 prospecting concessions and is negotiating to acquire an additional 80. For more information go to www.douglaslakeminerals.com.

This release contains forward-looking statements which involve risks and uncertainties. Complete forward-looking statement available at www.douglaslakeminerals.com/forwardlooking.html.

CONTACT: Douglas Lake Minerals Inc., Suite, 1445 West Georgia Street, Vancouver, BC, Canada, V6G 2T3, T (604) 669-0203, F (604) 669-3645, M (604) 825-1309, www.douglaslakeminerals.com



---------------------------------------

Source: Douglas Lake Minerals
 
Kuna taarifa zozote huko nyumbani zimetolewa kuhusu kuanza kazi ya uchimbaji LINDI kutoka kwa kampuni jamani? Nini hatma ya hao wachimbaji wadogo na ni nani hasa mmiliki mzawa. Any idea
 
Kuna taarifa zozote huko nyumbani zimetolewa kuhusu kuanza kazi ya uchimbaji LINDI kutoka kwa kampuni jamani? Nini hatma ya hao wachimbaji wadogo na ni nani hasa mmiliki mzawa. Any idea

ngoja nifuatilie. will come back
 
Kuna taarifa zozote huko nyumbani zimetolewa kuhusu kuanza kazi ya uchimbaji LINDI kutoka kwa kampuni jamani? Nini hatma ya hao wachimbaji wadogo na ni nani hasa mmiliki mzawa. Any idea


Mama.... yaani hii yawezekana kuwa 'breaking news', wanaLindi wanaweza wasiwe na hata punje ya maelezo, bali kusubiria mabango yaliyogongelewa kwenye miti ya kuwataka wahame mara moja kutoka kwenye vitalo vyao..

ngoja nifuatilie. will come back
.... na tutakungojea hapa hapa mheshimiwa, u tumaini la wengi wetu hapa!!
 
Mama.... yaani hii yawezekana kuwa 'breaking news', wanaLindi wanaweza wasiwe na hata punje ya maelezo, bali kusubiria mabango yaliyogongelewa kwenye miti ya kuwataka wahame mara moja kutoka kwenye vitalo vyao..


.... na tutakungojea hapa hapa mheshimiwa, u tumaini la wengi wetu hapa!!

au ndio hivyo tena kila mtu anajiamulia kuingia ubia tu? kweli ni kwamba nchi yetu haina sheria au ndio 10% zinatawala? Sasa hapa mtu mmoja mmoja kama hivi anamua kuingia ubia si ndio mwanzo wa kuingia mkataba feki. Au ndio miradi ya vigogo mafisadi? Shukrani kwa kufuatilia Mheshimiwa.
 
serikali ya MUUNGWANA ndio iko kazini hivyo

I think ni system yote tu imeoza. Inawezekanaje hao watu wa nje watoe press release kwamba wanakuja huku TZ kufanya majamboz halafu huku kwetu mambo sirisiri tu, Siri ya nini. Ilitakiwa kila kampuni inayokuja itangazwe hata miezi sita kabla ya kuanza kazi ili kuwajulisha wanaTz kwanza, we deserve to know!
 
I think ni system yote tu imeoza. Inawezekanaje hao watu wa nje watoe press release kwamba wanakuja huku TZ kufanya majamboz halafu huku kwetu mambo sirisiri tu, Siri ya nini. Ilitakiwa kila kampuni inayokuja itangazwe hata miezi sita kabla ya kuanza kazi ili kuwajulisha wanaTz kwanza, we deserve to know!

There is no need to think

This is an OPEN SECRET serikali yake jamaa imeooza TOP-DOWN

cha muhimu ni kuwa sasa hilo twalijua...the next question kuwa na listi ya watu wa kuwaongoa ...na kuendeleza mashambulizi left and right

 

There is no need to think

This is an OPEN SECRET serikali yake jamaa imeooza TOP-DOWN

cha muhimu ni kuwa sasa hilo twalijua...the next question kuwa na listi ya watu wa kuwaongoa ...na kuendeleza mashambulizi left and right



you mean list ya watu wa kuwaongoa au kuwaongoza. Kama system imeoza top-down that means mashambulizi hasa yawe bottom-up, maana hawa bottom guys ndio wanaofanikisha haya madili ( BRELA, TRA et al, all need to be sructinised)na ndio wengi, everyone has to be accountable and be responsible for own actions. Bora kupata wafanyakazi wapya na kuanza upya kuliko kuendelea kuwatumia hao hao ambao wako dirtly corrupt.
 
ngoja nifuatilie. will come back

I believe you will also do something in addition to coming back here. See, nature gave us almost everything we need (resources) including time(which we shouldnt waste anymore), the entropy has to be arrested now
 
Jamani, ukiacha Mwadui, Mererani, Kiwira, Buliyanhulu, Buzwagi na north Mara Tanzania kuna migodi gani mingine ambayo inaoperate large scale na small scale? Mwenye kujua naomba kuelimishwa kwenye hili
 
Kashfa ya mgodi wa dhahabu Buhemba, bilioni 30/- `zaliwa`

2008-05-11 12:06:39
Na Mwandishi Wetu


Kashfa ya ufisadi katika mgodi wa dhahabu wa Buhemba ulioko mkoani Mara, umesababisha mapato ya nchi yenye thamani ya Sh. bilioni 30 `kuliwa` na wajanja.

Fedha hizo `zilitafunwa ` katika Awamu ya Rais Benjamin Mkapa, kuanzia 2003 hadi 2006 kupitia wawekezaji wa kampuni ya Tangold `iliyojimilikisha` mgodi huo kinyemela.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopatikana kutoka Benki Kuu (BoT), jijini Dar es Salaam, Tangold ilichukua mgodi wa Buhemba ambao kuanzia mwaka 1997 ulikuwa ukiendeshwa kwa ubia na kampuni ya MEREMETA, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Triennex Properietary Limited ya Afrika Kusini.

Nyaraka nyeti kutoka BoT zilisema kuwa JWTZ na mbia huyo walianza kuchimba dhahabu Oktoba 1997 na baadaye mkataba ulimalizika na Tangold ilijimilikisha mgodi huo kuanzia mwaka 2003 hadi 2006.

Ziliibua kuwa mambo ya MEREMETA hayakwenda vizuri kwani miradi yote iliyoanzishwa ilitumia fedha za mikopo kutoka Benki ya Nedcor ya Afrika Kusini ambayo ilichukuliwa na kampuni ya Triennex Properietary kwa niaba ya Serikali ya Tanzania.

``Kwa kuhofia athari za mkopo huo kwa uchumi wa nchi, Rais mstaafu Benjamin Mkapa, aliunda Kamati maalum (task force) mwaka 2003 kwa ajili ya kuhakikisha mkopo unalipwa , kusimamia uendeshaji wa miradi ya MEREMETA na kuchunguza matatizo ya kampuni hiyo ya JWTZ na wawekezaji kutoka Afrika Kusini``, kilisema chanzo cha BoT.

Wajumbe wa kamati ya kuchunguza matatizo ya MEREMETA walikuwa ni Gavana wa BoT aliyefutwa kazi Dk. Daudi Balali, aliyekuwa Mwenyekiti.

Wengine ni Makatibu Wakuu Bw. Gray Mgonja wa Wizara ya Fedha, Bw. Patrick Rutabanzibwa -Madini na Nishati, (sasa Wizara ya Maji na Umwagiliaji), Bw. Vincent Mrisho aliyekuwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (sasa Ofisi ya Waziri Mkuu) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya awamu ya tatu, Bw. Andrew Chenge.

Bw. Chenge mwezi uliopita alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu kufuatia tuhuma za kuhifadhi zaidi ya shilingi bilini moja zinazodaiwa kuwa ni rushwa aliyopewa katika ununuzi wa rada iliyogharimu bilioni 70/-

Baada ya Tangold kuchukua Buhemba, ilichimba dhahabu yenye thamani ya Dola milioni 121.3 sawa na Sh. bilioni 147.

Dhahabu iliyochimbwa kwa kipindi hicho ni mali ya serikali kwani mgodi huo ulikuwa ni mali ya umma na ilikuwa na thamani ya Dola.

Taarifa zilizoifikia Nipashe Jumapili zilieleza kuwa katika kipindi hicho cha miaka minne, Tangold ilichimba karibu kilo 10,000 za dhahabu kutoka mgodi huo na kupata faida ya bilioni 30/-.

Tangold ilionyesha kuwa ililipa mrahaba wa Dola milioni 3.6 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Vijijini ambao ni sawa na Sh. bilioni 4.36 kwa muda wote.

Takwimu za uchimbaji zilionyesha kuwa mwaka 2003 zilichimba kilo 2,848. 874, wakati mwaka uliofuata zilipatikana kilo 291.290. Mapato yanaonyesha kuwa mwaka 2005 ilipata kilo 2,220. 560 na mwaka 2006 ilipata kilo 1,890.934 na kwa jumla zilipatikana kilo 9, 941.658.

Hata hivyo, baada ya kupata kiasi hicho BoT ilionyesha kuwa Tangold iliilipa kampuni moja ya Afrika ya Kusini gharama za kuendesha mgodi ambazo ni kati ya Dola milioni 80 na 90 kwa miaka minne ambazo ni sawa na Sh. bilioni 100 mpaka 116.3.

Hata hivyo, licha ya kupata mabilioni hayo Tangold haikuwasilisha fedha hizo serikalini.

``Taarifa za Tangold haziko Wizara ya Fedha-Msajili wa Hazina , wala kwa Msajili wa Biashara (BRELA) hata BoT hazikuwahi kuwasilishwa,`` kilisema chanzo cha BoT.

Pesa hizo bilioni 30 ni mali ya umma lakini hazijulikani zilipo na swali linaloendelea kuulizwa ni wamiliki wa kampuni hiyo ni akina nani?

Katika Mkutano wa Bunge wa mwezi uliopita Mbunge wa Musoma Vijini Bw. Nimrod Mukono, alitaka kufahamishwa wamiliki wa mgodi wa Buhemba.

* SOURCE: Nipashe
 
Mama,
Hii ni hatari ktk taifa changa kama hili, kwani few people benefit the national cake and the majority wanaumia, mikataba hii imeendelea kuwa siri mpaka lini?
 
Hingekuwa busara sana kama migodi hii ingemilikiwa na halimashauri husika na serikali kuu ikabaki kusimamia mambo ya msingi pamoja na kutoa wataalamu.hata kama kuingia ubia basi ingekuwa ktk ya halimashauri pamoja na huyo mbia.
kila kitu kufanywa na serikali kuu ni kuwanyima haki wananchi ambao wanaishi ktk maeneo ya mgodi na kuwapa umasikini wa milele.
 
Ndugu zangu wana Jamiiforums naomba tulijadili hili na kuona ni Jinsi gani tunaweza kuwasaidia au kuwa-amsha ndugu zetu jinsi ya kujitetea na Viongozi wetu mafisadi.

Maana naona wanacho fanya ni kuanzisha sera zenye nia ya kuwapora wanyonge kwa kutumia msemo kwamba ardhi na madini ni mali ya serekali, hivyo ndugu zetu wa Mererani , wameporwa maeneo yao ya madini na Tanzania one kwa kusaidia na viongozi wetu, pia viongozi binafsi kama Kapuya , na wengineo wametumia mwanya huo kujimilikisha maeneo ya madini at the expense ya wanyonge, pia ndugu zetu wa Buzwagi , Geita, Buhemba, North Mara na sehemu nyingine wameporwa na Barrick etc na viongozi wachache walio tumia nafasi hii kujikatia Blocks za madini.
Suala endelevu kwanini rai hao hawakupewa Shares katika hayo makampuni kwa kutoa hiyo ardhi yao? na kudhaminisha kilicho chini ya ardhi? au hata halamashauri husika.

Wanasheria wetu wako wapi katika kuwatetea watu hawa especially hizi NGO za Kisheria na individual lawyers ? Wabunge nao mko wapi katika kuwatetea wapiga kura wenu? Je mwajua maafa ya kuwauza watu wenu? na taifa kwa Jumla? au mnaona raha kuwa na wapiga kura wasio na nyumba bora, barabara bora etc.

Je was it legal na moral right to do so?
 
Back
Top Bottom