Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

Mikataba ya Madini na Serikali ya Tanzania

huwa nashangaa sana linapotokea jambo watu mkamuona jk hausiki.jamani muungwana anajua kila kinachotokea,na hili ni dili lake mwenyewe,kwa utawala wa kibongo waziri hana kauli huwa wanafuata maagizo tu.waziri yeyote atakaye amua kufanya kitu kutokana na matakwa yake,basi huyo kesho hana kazi
 
huwa nashangaa sana linapotokea jambo watu mkamuona jk hausiki.jamani muungwana anajua kila kinachotokea,na hili ni dili lake mwenyewe,kwa utawala wa kibongo waziri hana kauli huwa wanafuata maagizo tu.waziri yeyote atakaye amua kufanya kitu kutokana na matakwa yake,basi huyo kesho hana kazi

KT hapo nakuunga mkono mia kwa mia, Muungwana lazima alijua hili na kama hakujua basi sioni Urais ni wanini kama hawezi hata kujua subordinates ambao yeye mwenyewe amewa appoint. There is something funny here, kuwa kila jambo baya linapotokea kunakuwa na spinning kuwa Muungwana aidha hakulijua au kashauriwa vibaya. Yaani its like people don't want to believe that there "redeemer" can't do anything wrong. In reality Muungwana anatakiwa ajirudi maana haya mapenzi ya wana wa nchi yakija kuchuja itakuwa balaa kubwa.
 
mTz,
huyu jamaa ni mtu wa hovyohovyo tu,tutaula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua.
 
KT hapo nakuunga mkono mia kwa mia, Muungwana lazima alijua hili na kama hakujua basi sioni Urais ni wanini kama hawezi hata kujua subordinates ambao yeye mwenyewe amewa appoint. There is something funny here, kuwa kila jambo baya linapotokea kunakuwa na spinning kuwa Muungwana aidha hakulijua au kashauriwa vibaya. Yaani its like people don't want to believe that there "redeemer" can't do anything wrong. In reality Muungwana anatakiwa ajirudi maana haya mapenzi ya wana wa nchi yakija kuchuja itakuwa balaa kubwa.

Kila linalowezekana linafanyika ili kuonyesha kuwa rais hafanyi makosa. Ni yale yale ya askari kujitoa mhanga kumlinda jenerali wake asitekwe. Kikwete alikuwa na habari zote, na huu ulikuwa ni mpango uliokwisha kamilishwa kila kitu na kupewa baraka zake zote. Hakuna waziri mwenye ujasiri wa kuficha maelezo ya mkataba kama huu, na kuusaini kisirisiri bila ya kupata baraka zote za mkuu wake wa kazi. Tunaambiwa upuuzi usiokuwa na maana yoyote hapa.

Kikwete is allowing himself to be a crook. What a pity!
He seemed to be so much of a good promise to many of us; what a let down, and so fast?
 
Ofisi ya Rais imechemsha kwa kudai kwamba Rais haihitaji kuarifiwa kuhusu mikataba. Karamagi wizara imeshamshinda na hana tena credibility hapo wizarani na hata machoni kwa Watanzania. Muungwana inabidi atafute mtu mwingine ili aongoze hii wizara nyeti.

Muungwana nae nchi pia imemshinda. Nijuavyomimi issue za mkataba ya uwekezaji inahusiha wizara ya mipango kuchambua kama huo mradi unamasiliaha kwa taifa, Wizara ya fedha kuchamboa mapato ya serikali kutoka huo uwekezaji, wizara ya mazingira kuangalia environmental impact, wizara husika (Nishati na Madini) na Atony genearal chember kuangalia maswala ya kisheria. Je huu mkataba ulipata imputi za mwanasheria mkuu wa serikali?

Ni sheria ya nchi gani inasimamia huo mkataba? ni UK au Tanzania? Je mkataba unasema kuwa utasainiwa UK? Je sheria ya madini inasema si muhimu kwa raisi kujua wakati mkataba uanasaini? Sasa raisi anastahili kujua nini? Kama kweli raisi hanahaja ya kujua kuhusu maliasili ya nchi anatakia wajue nini? maana rasili mali ndio nchi yenyewe. Mbunge na wanachi hawakujulishwa lolote, je huu mradi ukiwa na madhara yakuhatarisha maisha yao nani alaumiwe?
 
Nimesoma maelezo ya wachangiaji wengi yaonyesha wazi wananchi bado wana mapenzi na rais, bado wana matumaini na rais wao na hata Huyo Zitto aliya onyesha kwa kumtahadharisha lakini yaonyesha wazi kuwa miti yote inaanza kumteleza.
Rais wetu amezungukwa na watu ambao wanataka kuhakikisha anaanguka!. Na ataanguka kweli tena vibaya kiasi kwamba itakuwa historia ya nchi yetu!
 
Ama kweli tutaona na kusikia mengi ya kustaajabisha kabla ya 2010. Hivi kweli inaingia akilini kwa rais upo safari moja na waziri wako kwenye briefcase kabeba mihuri ya serikali anakwenda kusaini mkataba wewe haujui na wala yeye asiku brief hata kidogo. Kama hayo ni kweli basi kuna tatizo kubwa sana katika uongozi wa nchi yetu.
 
Milioni $400 ni sawa:

  • 1.7% of GDP (2004)
  • 34.0% of Public debt (2004)
  • 20.2% of Revenues (2004)
  • 19.3% of Expenses (2004)
  • 33.3% of Economic aid (2004)
Inamaana raisi hajui ancho kifanya? I don't think so. Muungwana na watu wa ikulu wote waongo.
 
siku zote alikuwa wapi huyu!? 😕

Mbunge wa CCM naye akerwa na wawekezaji katika migodi
* Awakoromea mbele ya Waziri Mkuu Lowassa

Na Mkinga Mkinga, Mara
Kutoka Gazeti la Mwananchi


MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono, amewashutumu wawekezaji katika migodi ya madini mkoani Mara kuwa wanahamisha rasilimali hiyo na wakiwaacha wananchi wakiwa masikini, huku wakichangia kiasi kidogo kwenye maendeleo ya jamii.

Alisema licha ya kuchimba madini ambayo yanawapatia fedha nyingi, mchango wao katika jamii hauendani na kile wanachokivuna kwenye mgodi hiyo.

Mbunge huyo alisema kinachofanyika ni kuhamisha madini hayo na kuwaachia wananchi umaskini mkubwa.

Akizungumza katika ziara ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kukagua shule za sekondari zilizojengwa na mbunge huyo kwenye Kijiji cha Busegwe, Mkono alisema mchango wa wawekezaji hao ni kidogo sana.

"Katika mkoa mzima huwezi kuona shule nzuri kama nilizojenga mimi, hata ukienda shule zilizojengwa na hao wawekezaji," alitamba Mkono huku Lowassa akiwa amekaa kimya.

Mkono amekuwa akipinga kiwango kidogo cha michango ambacho kimekuwa kikitolewa na wawekezaji katika mendeleo ya jamii kama ujenzi wa shule na vituo vya afya kuwa, hailingani na thamani ya rasilimali wanayovuna.

Mbunge huyo aliwahi kususia makabidhiano ya Sh240 milioni kutoka kwa wawekezaji, akidai kuwa hataki kuona uchafu ukifanyika mbele yake kwa sababu hajui umiliki wa migodi hiyo pamoja na uliokuwa jimboni lake la Buhemba.


?Sitaki kuona uchafu huo unafanyika mbele yangu. Maana hiyo mikataba mimi siijui, hata ule wa mgodi wa Buhemba, ambao uko jimboni kwangu sijui unamilikiwa na nani,? alinukuliwa Mkono wakati akisusia kushuhudia makabidhiano hayo kati ya Kampuni ya Barrick Gold Tanzania na halmashauri za wilaya ambako kuna migodi yake.


Wilaya zenye migodi inayomilikiwa na kampuni hiyo ni Tarime, Kahama na Biharamulo.


Mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria, anahoji uhalali wa kiwango cha dola 200,000 zilizoainishwa kwenye mikataba kwa ajili ya halmashauri husika na anapendelea kupitia upya mikataba kabla ya kupokea fedha hizo.

?Kisheria kukubali kidogo ina maana umekubali moja kwa moja, hapa huwezi baadaye ukataka watoe fedha zaidi,? aliendelea kunukuliwa Mbunge huyo.


Wakati mbunge huyo akitoa shutuma hizo, kuna sakata linaloendelea kati ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kabwe Zitto na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi kuhusiana na kusainiwa mkataba wa mgodi wa Buzwagi nje ya nchi. Mgodi huo pia unamilikiwa na Kampuni ya Barrick.

Sakata hiyo imesababisha Zitto kusimamishwa shughuli za ubunge baada ya kuwasilisha hoja binafsi bungeni, akitaka kuundwa kwa Kamati Teule kuchunguza mchakato wa mkataba huo.

Tangu kuibuliwa kwa tuhuma hizo, kumekuwa na maelezo yanayokinzana kuhusiana na ufafanuzi juu kwa upande wa Barrick na Waziri Karamagi, huku wakichanganyana kwenye tarehe za mchakato hadi kusainiwa London, Uingereza.
 
teh teh aisee ilibidi nicheke, eti anamkoromea mbele ya PM wakati PM mwenyewe inawezekana amekula hapo hapo....
 
Wababaishaji hao, si ndio walikuwa wanasheria wa Serikali katika kuuza Mashirika mengi wakati wa kupora mali ukianzia na NBC.
 
Ogah,

Asante kwa kunikumbusha kwamba kwa kuangalia yaliyotendeka huko nyuma, ni kwamba share yetu itabidi iwe 3%, na itoke kwenye hiyo share ya Barrick.

Sasa tukipata 3% toka kwa hiyo 50% ya Barrick, ni kwamba tutakuwa tumepata 1.5% ya share zote. Tatizo linakuja hivi: kwa vile inabidi tuilipe kampuni fulani 1.9% toka kwenye kawaida yetu ya 3%, ina maana itabidi tukope mahali kuongezea huo mshiko wetu wa 1.5% ili tufikishe hiyo 1.9% ya hiyo kampuni.

Kwa maneno mengine, ni kwamba kwa mpango huu, tutabaki sio na shimo na uchafuzi wa mazingira tu, bali na deni zito vile vile.

Sasa nimeelewa kidogo ni kwa nini wakubwa wanapenda kufanya haya mambo kwa SIRI. Wananchi wakifahamu kinachoendelea wanaumia sana tu.

Augustine Moshi
 
Inawezekana anakerwa na wawekezaji wa madini akiwa Jimboni kwake, nje ya jimbo(Dar na Dodoma) kila kitu kwake ni sawa.Mbona hatukumsikia Bungeni akisimama kumtetea Zito Kabwe.
 
Nilipata kichefuchefu saba ninaposoma Waziri Karamagi akijibu hoja ya Zitto kwa kutamba kuwa serikali imepitia mikataba upya na sasa makampuni yamekubali kuchangia dola 200,000 kwa mwaka kwenye halmashauri za wilaya. Nikaona kweli watanzania tumelizwa. Madini haya siyo sawa na mazao ya shamba kuwa tutalima mengine, yakishaenda yamekwenda. Ni afadhali yangechukuliwa na mkoloni, tungejua ametudhulumu kwa nguvu, lakini kuyaacha yachukuliwa huku tunachekelea na upuuzi kabisa.

Huyu Mkono ni mtu wa ajabu sana; msimamo wake kuhusu wawekezaji haueleweki na sijui kama hapa anafanya unafiki au ndiyo msimamo wake kweli kweli. Kumekuwa na tetesi zisizothibitishwa kuwa yeye alikuwa msitali wa mbele katika kutayarisha mikataba ile na hivyo kujipatia mapesa mengi sana. Makampuni mengi ya nje yaliyoingia Tanzania yameptia kwake, na kuna siku aliwahi kusema kuwa yeye ndiye aliuza MNB. Sasa imekuwaje? hata mimi sielewi, nadshani huu utakuwa unafiki tu.
 
Walijua Watanzania ni wasahaulifu hivyo baada ya muda kelele zote zitakwisha na wao waendelee kupeta. Kumbe sivyo, maoni ya Watanzania katika swala hili hata wale ambao ni wanachama wa CCM yanaonyesha jinsi ya kukerwa na madini yetu kuchimbwa bila kufaidika ukilinganisha na nchi za wenzetu.

Huyu Mkono ni mnafiki tu, kama utakumbuka gazeti ,oja lilipoandika kwamba kalipwa mabilioni na BOT akatishia kulifungulia mashtaka gazeti hilo. Baada ya siku chache kamati ya Bunge ikaweka hadharani kwamba Mkono alilipwa bilioni 8 na BOT. Ni mnafiki tu anajaribu kufanya kila namna ili ajipatie umaarufu asiokuwa nao, lakini tumeshamshtukia kama tulivyomshtukia Majiyatanga Mchangawarukwa Mzindakaya.
 
Nilishawaambieni zamani tu kwamba tutabaki na makorongo! Period.
 
Kama hivyo ndivyo, basi atoe ushuhuda tuusikie sote bila kuficha. Mikataba yote kati ya serikali na mashirika aliyoipitia, na sasa kuiona kuwa haifai aianike hapa. Vinginevyo huo sio ulokole wa kweli, bali ni ubabaishaji.

Pili, aende bungeni, aungane na akina Zitto/Slaa katika juhudi zao za kulinusuru taifa letu na haya majambazi ya kitaifa na kimataif.
 
Cha kushangaza zaidi maeneo mengine yanayogunduliwa yana dhahabu yanaenda kwa mwendo ule ule wa mikataba iliyotangulia ambayo haina maslahi kwa Watanzania. Sasa hivi cha kupigia kelele na kuwashinikiza hawa viongozi uchwara na kuiweka mikataba hiyo hadharani ili wote tujue maslahi yake kwa Tanzania. Hili la kusema kwamba wachukuaji watalipa kodi zaidi na wakati huo huo mikataba imebaki siri halina maana yoyote kwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom