Nimemsikia Waziri kagasheki akilalamikia polisi wa vyeo vya juu kufifisha vita dhidi ya ujangili na kwamba baadhi yao wanashiriki kuwaachia/kuwatorosha watuhumiwa. Sijui kwa nini viongozi wetu wa serikali tena viongozi wa juu wanalalamika kwenye vyombo vya habari kuhusu udhaifu ndani ya serikali. Wanashindwa nini kuzungumza na kuchukua hatua stahiki kuliko kuja kutulalamikia sisi wananchi.
Hivi Waziri anapolalama hajui kuwa anaidhalilisha serikali yake. Kagasheki anawalalamikia polisi wakati yeye ni Waziri, na zaidi alishakuwa Waziri wa mambo ya ndani akiwasimamia polisi! Kama hawezi kuchukua hatua si amwendee Raisi wake ili achukue hatua. Inakera kusikia Waziri au Kiongozi coyote wa serikali akilalamika.
Hakuna la ajabu. Katika serikali ya awamu hii almost kila kiongozi analalamika.