Mh.Kagasheki: RPC Arusha awatorosha majangili

Mh.Kagasheki: RPC Arusha awatorosha majangili

Twilumba

Platinum Member
Joined
Dec 5, 2010
Posts
13,594
Reaction score
16,491
RPC Arusha kuchukuliwa hatua baada ya kuhusika kuwatorosha majangili raia wewenye asili ya kiarabu mapema baada ya kukamatwa wakihusika na ujangili.

Hii ni kwa mujibu wa Waziri Wa maliasilia na Utalii alipoongea na vyombo vya habari leo hii.

Mh. Kagasheki amesema kuwa RPC huyo alihusika moja kwa moja kuwatorosha majangili hao ambapo aliwarudihia passport na kusaidia kuwapa mbinu za namna ya kutoroka nchini baada ya yeye kuruhusu waachiwe baada ya kukamaatwa.

Source: Clouds F-Taarifa ya habari saa 12 jioni!
 
Jamani kuna wanachi wanauwawa huko Manyara na maafisa wanyamapori in the name of ujangili...

while i support majangili kushughulikiwa, nina wasiwasi kwamba hii kitu inakua abused, na majangili halisi (kama hao waarabu) wamekua mitaji ya wakubwa wa polisi
 
Jamani kuna wanachi wanauwawa huko Manyara na maafisa wanyamapori in the name of ujangili...

while i support majangili kushughulikiwa, nina wasiwasi kwamba hii kitu inakua abused, na majangili halisi (kama hao waarabu) wamekua mitaji ya wakubwa wa polisi

Very possible coz wanaona wanawabana kwenye suala la uuaji wa tembo!
 
Waziri Kagasheki alifungukia jeshi la polisi

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Hamis Kagasheki amesema vitendo vya rushwa kwa baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi bado ni kikwazo kwenye mapambano dhidi ya ujangili.
Amesema licha ya watuhumiwa kukamatwa na vithibitisho lakini bado wengi hususan raia wa kigeni wamekuwa wakiachiwa na hivyo kuhamasisha vitendo hivyo kuzidi kushamiri.
Licha ya kuanzisha operesheni maalumu ya kamata majangili yenye lengo la kudhibiti mauaji ya tembo lakini baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi wameendelea kuwa kikwazo katika mapambano hayo.
Waziri Kagasheki anasema operesheni hiyo yenye baraka zote za Amiri Jeshi Mkuu wa nchi Rais Jakaya Kikwete itaendelea licha ya wahujumu hao kuingilia juhudi hizo, huku akiahidi kuwachukulia hatua za kisheria watakapobainika.
Aidha katika oparesheni hiyo ya kamata majangili baadhi ya watumishi wa wizara hiyo wamebainika kuwa washirika wa biashara hiyo haramu.
 
Ukisikia majanga ndiyo haya sasa polisi wamekuwaje tena wakibainika ni vema sheria itembee juu ya migongo yao.
 
Ukisikia majanga ndiyo haya sasa polisi wamekuwaje tena wakibainika ni vema sheria itembee juu ya migongo yao.

Ingawa hajamtaja wazi wazi lakini kasema Arusha kuna askari anatumia nyota zake vibaya kiasi cha kufanya wanaokamatwa kupelekwa kushtakiwa katika mikoa mingine.Hivi Tanzania tutaogopana mpaka lini?Kwa nini hasimtaje kama ni RPC raia wema tujue?Maana najua mamlaka (polisi,usalama wa taifa) watakuwa wanamjua lakini kama kawa bongo kulindana!!
 
Kesi za ujangili wa Arusha zinaendeshewa maeneo mengine kwa sababu kuna "mkubwa" mmoja aliyepewa nyota zetu na magwanda yetu anahusika kuwatetea na hata kuwatorosha. Wasaudi arabia waliotoroshwa ana..... "Tutawachukulia hatua, hata yeye tutawachukulia hatua"
 
Kesi za ujangili wa Arusha zinaendeshewa maeneo mengine kwa sababu kuna "mkubwa" mmoja aliyepewa nyota zetu na magwanda yetu anahusika kuwatetea na hata kuwatorosha. Wasaudi arabia waliotoroshwa ana..... "Tutawachukulia hatua, hata yeye tutawachukulia hatua"
Mkuu na wewe wa hovyo kweli yani unaandika kama unaongea hujaeleweka hata chembe jipange tena.
 
Akamatwe mara moja na kupelekwa mahakamani afungwe maisha au apigwe risasi kabisa.
 
Watu hamjamuelewa waziri! Askari alietorosha hao majangili sio RPC sabas, ni OCD ila hakumtaja jina wala kusema ni wa wilaya gan.

Sema sabas Arusha imemshinda bora alivyokuwa Manyara.
 
RPC akamatwe mbona Mh. Lema walimkamata saa saba za usiku?
 
hii habari nimeiona itv usiku huu...nimesikiliza kaga..nimeogopa
 
RPC Arusha kuchukuliwa
hatua baada ya kuhusika kuwatorosha majangili raia wewenye asili ya
kiarabu mapema baada ya kukamatwa wakihusika na ujangili.

Hii ni kwa mujibu wa Waziri Wa maliasilia na Utalii alipoongea na vyombo
vya habari leo hii.

Mh. Kagasheki amesema kuwa RPC huyo alihusika moja kwa moja kuwatorosha
majangili hao ambapo aliwarudihia passport na kusaidia kuwapa mbinu za
namna ya kutoroka nchini baada ya yeye kuruhusu waachiwe baada ya
kukamaatwa.

Source: Clouds F-Taarifa ya habari saa 12 jioni!

Yale ya ukoo wa mapanya hawa wezi kuwakamata panya wenzao yanazidi kutimia nchi nayo inazidi kumalizika waziri kagasheki anawajua majangili wa tembo hapa nchi ni akina nani lakini hana nguvu za kuwashika kwani ni watu wakubwa ndani ya serikali ya maccm

hapa nina nukuu maneno yake :kuna mtu moja amedriki kunielwa pigia simu ana lalamika anasema eti atakwenda kumueleza mheshimiwa Rais nami nkamjibu aende
kwani nina baraka zote kutoka kwa amri jeshi mkuu ambaye ni yeye.Swali la kujiuliza hawa panya watawashika panya wenzao ?
 
Back
Top Bottom