msemakweli10
JF-Expert Member
- Oct 14, 2013
- 229
- 46
Wale waleee! Sishangai.
By Mag3![]()
![]()
Hapa kweli pagumu...waziri vs Rpc, CCM vs CCM! Heri Simiyu Yetu keshachagua upande...bado ifweero, ZeMarcopolo, CHAMVIGA, Ritz, Chris Lukosi, chuki, Annael, FaizaFoxy, MSALANI, MwanaDiwani, stroke, masopakyindi na kikosi kizima cha Lumumba team...duh, kumeza kutema! Kaazi kweli kweli!
Naipenda nchi yangu zaidi ya mnavyofikiri. Mimi sio kipofu.
Mulongo ndie m/kiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Arusha.
Haya maswala yametokea arusha ambako lema ndiyo mbunge na lema tabia yake iko wazi sasa mnategemea nini.
Khaa!!sasa mkuu hapo mulongo kaingiaje?
Mwanzoni niliona umeongea point nzuri sana ila kwa hii post yako inaonyesha kabisa akili zimelala..lema na RPC wana mahusiano gani mazuri??
Bwana mdogo si uliwahi kunieleza kuwa 'dili' kama hizi zinakuweka mjini!Hii nchi inaendeshwa kiliberali sana. Yani waziri anapgwa biti?
Ukisikia majanga ndiyo haya sasa polisi wamekuwaje tena wakibainika ni vema sheria itembee juu ya migongo yao.
Ni kweli kabisa kwani ana makosa manne makubwa aliyoyafanya katika utumishi wake
1. Alisaidia na kupanga shambulizi la Bomu pale kwenye mkutano wa CDM Soweto
2. Alisaidia kuwatorosha wale waarabu waliohusishwa na Mlipuko wa Bomu pale kanisani Olasiti
3. Alifanikisha kutoroka kwa wale waharifu waliomchinja Mwenyekiti wa CDM pale Usariver
4. Amehusika kuwatorosha waarabu ambao walikamatwa kwa ujangiri wa wanyama Poli
Huyu nina wasiwasi atakuwa ni mjumbe katika kikosi kazi cha Kinana cha Tokomeza Tembo Tanzania (TTT) sidhani kama atashughulikiwa .
Hata mimi naamini wewe sio kipofu, kinachonisikitisha siku zote ni michango yako.
Mingi ya michango yako huwa haina base wala mwelekeo. Huwa unatoa kashifa na maneno makali kwa hoja za kizushi
Sasa kwa mambo mazito kama haya lete msimamo wako badala ya kushupalia nadharia za slaa na familia yake.
Akamatwe mara moja na kupelekwa mahakamani afungwe maisha au apigwe risasi kabisa.
Nimemsikia Waziri kagasheki akilalamikia polisi wa vyeo vya juu kufifisha vita dhidi ya ujangili na kwamba baadhi yao wanashiriki kuwaachia/kuwatorosha watuhumiwa. Sijui kwa nini viongozi wetu wa serikali tena viongozi wa juu wanalalamika kwenye vyombo vya habari kuhusu udhaifu ndani ya serikali. Wanashindwa nini kuzungumza na kuchukua hatua stahiki kuliko kuja kutulalamikia sisi wananchi.
Hivi Waziri anapolalama hajui kuwa anaidhalilisha serikali yake. Kagasheki anawalalamikia polisi wakati yeye ni Waziri, na zaidi alishakuwa Waziri wa mambo ya ndani akiwasimamia polisi! Kama hawezi kuchukua hatua si amwendee Raisi wake ili achukue hatua. Inakera kusikia Waziri au Kiongozi coyote wa serikali akilalamika.
Who is dr slaa in this country mpaka atishie nchi haitotawalika? Mimi usinifundishe la kuandika. Heshimu michango yangu japokuwa haina mbele wala nyuma. Naipenda nchi yangu ninawachukia wahujumu nchi.
Jipe shughuli...mbona sisi tumemuelewa...acha ushauri wako kama nguvu za giza.
Mzee amenawa mikono na kushtaki kwa wanainchi (wenye inchi)...sasa huko unakomshauri aende kungeendeka angesubiri nini ?
Tusubiri tuone ni wangapi ndani ya hiyo serikali watamuunga mkono au ni yale yale ya kukaa kimya kinafiki....na kama kweli kuna nia safi miongoni mwa viongozi wa serikali, basi watakaa nyuma ya Kagasheki na huyo/hao wanaolinda uchafu wabaki mwenyewe.
bwana mdogo si uliwahi kunieleza kuwa 'dili' kama hizi zinakuweka mjini!