Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Poleni sana mlitumiwa.

Sasa nendeni kwenye nyumba za ibada mkatubu dhambi maana maisha yamepotea.
 
NJAA NI KITU MBAYA SANA.
Njaa inaweza kukufanya Uwe mnafiki na kuikana nafsi yako.
Njaa inakufanya upoteze MSIMAMO,WELEDI NA MWELEKEO.
Njaa itakufanya uone ni sawa MKE wako kutembea na Bosi wake ili mradi analeta mkate mezani.
Njaa haina USHUJAA..na hili limedhihirika kutokana na Hawa INTERNS NJAA.

Wakati wanahangaika na kusumbua WATANZANIA kumbe walikuwa hawana PLAN B!?
Leo hii mnarudi kuomba Radhi na kutaka msamaha ili mrudi kazini!? Halafu msamaha mnaomba kwa Rais na sio kwa WATANZANIA MNAOWATUMIKIA NA MLIOWAHADAA NA MGOMO WENU NJAA!?

Mwende tu huko Zimbamwe na Botswana mkafanye INTERNSHIP sasa. Weledi wenu umeingia doa chafu.
NJAA NI KITU HATARI.
 
Nilisema siungi mkono mgomo wa madaktari niliyajua hayo sasa wende kwa mapro wa CHADEMA wakaombe ajira kwani wao walikuwa wakiwaunga mkono kwa nguvu zote na zile ajira za nje ya nchi zimeishia wapi
 
Jamani madaktari kugoma ni haki yao. Ila cha maana wanatakiwa wawe na utu. Kusomea somo lolote kwa mtu mwenye akili anajua anafanya nini. Yafuatayo ni mambo yanaowakuta watu kwa kadri ya kazi yake.
1. Walimu, wanaishi katika mazingira magumu, hawana mishaara mizuri, wanaona kwamba hawathaminiwi, wameanza migomo siku nyingi kabla sijazaliwa
2. Wanasiasa, wanaishi mazingira mazuri, mishaara minono, wanaamini wanaeshimiwa, si wakweli hata kidogo. Sikuzote wanajiangalia wao tu
3. Wanajeshi, magereza, polisi, wanaishi mazingira mabaya kuliko wote, watiifu kwa yeyote aliyepo madarakani, mishaara sio mizuri, hawaheshimiki na wengi
4. Madaktari, mishahara sio mizuri, mazingira mabaya, wahaheshimika unapoumwa tu au ukiwa na mgonjwa, wanataka kuonekana wa maana kuliko mtu yeyote duniani kisa tu eti ukiugua yeye atakuokoa, wanatabia ya kugoma mara kwa mara
sasa wewe una mtoto wako anataka kusomea udktari unamruhusu vipi kwa historia hii. Kwanini asisomee wanasheria, biashara, uhasibu, sijawahi kusikia wamegoma.

Eliah G Kamwela says sorry for this very kilazaful post.
 
Kwanza mlalahoi gani ana uwezo wa kugharamia matibabu? huku uswazi tunatumia mix ya muarobaini, mpera, na mjengaua! Kiu yenu si kuhudumia wananchi bali ni kukamua beberu maziwa!Unafiki mkubwa huo!

 
kweli mama toto walikuwa wanatishia nyau, warudi tu wakaendelee kupokea vi rushwa vya 5000/- waasije kufa njaa!!

inabidi washtakiwe kwa kusababisha vifo. Maana wamekiri wenyewe. Pumbaf zao, na tuone kama watarudishwa. Wamesahau kuwa hata wanamuhas waliomba msamaha wakaishia kusimamishwa chuo wengine kufukuzwa.
 
nakumbuka hiki kikundi cha interns wasaliti kilianza harakati zake wakati wa mgomo wa mwisho kwa kutuma sms za ushawishi zenye mrengo wa serikali wa kujaribu kuwagawa madaktari kwa misingi ya dini.harakati hizi zilifanyika ndani ya nyumba za ibada.sishangai kuwaona wakija na tamko hili.
Hapa utagundua kuna wawakilishi wa system ndani ya madaktari ambao kwa namna moja au nyingine walikuwa wakivujisha siri za mienendo ya comrade ulimboka.
 
Kamati nyingine hii..."kamati kivuli"..hii ni kamati inayohitaji msamaha wa Rais mkuu.

sio vibaya walivyo amua .wanatumia busara kwani 2015 sio mbali .watakapo lipiza kisasi chao kwa serikali hii iliyopo madarakani ,mtumikie kafiri upata mrada wako
 
wamejiharibia sana hawa ndugu zetu, kosa namba moja ni pale mlipoamua kugawanyika wakati wa kugoma. Kosa namba mbili ni sasa mnapowageuka MAT na kuwatupia mpira wa lawama wakati utashi wa kugoma ulikua juu yenu.
Mwisho kabisa nasikitika kusema ya kwamba JK au serikali yake haitawasemehe kwa kuwa imeshagundua wapi mna kasoro, tafadhali jaribuni tu kutafuta career nyinginezo maana inaonesha hamkuwa na plan B.
Suala na ninyi kugoma ama kutokugoma ilipaswa mliongee vizuri hapo awali kwenye vikao vyenu vya ndani huku mkishauri na kushauriwa kutoka MAT.

Usimsemee Rais wala Serikali yake, huna ubavu huo.
 
Kwa kuwa mmejuwa makosa yenu na mmeamuwa kutubu kwa nia njema, au kama yuko aliyewashauri mfanye hivyo kwa nia njema. Tutakuwa nyuma yenu kuwaombea Serikalini na kwa Rais awakubalie ombi lenu na awasamehe yaishe.

Nna uhakika Rais Kikwete ni msikivu, hata Chadema walipokwenda Ikulu kumuomba aliwasikiliza.
 
ndio maana muda wa vikao vya wafanyakazi huwa naenda kusimamia biashara zangu
 
uzuri wa medical field ni mmoja tu.
Kosa la kusaliti medical fratenity ni baya kuliko yote.serikali ikiwasemehe hawa vilaza specialists ambao ndio waalimu wao professionally hawatawasamehe na matokeo yake hawatamaliza internship and ultimately they will never qualify to practise medicine in Tz.kamwe kikwete hana uwezo wa kusema hawa ni madaktari kamili,so they have to choose kama watapiga magoti kwa serikali au walimu wa madaktari.this is a big battle!
 
Back
Top Bottom