Hata rais wa zamani wa Marekani, Ronald Reagan [rais ambaye alishinda kwa kishindo] mwanzoni alikuwa ni mwanachama wa chama cha Democrat na akahama kambi na kuhamia chama cha Republican na baadaye kugombea urais kupitia chama hicho na kushinda mihula miwili.
Sasa nini cha ajabu hapo?
Mbona Uhuru Kenyatta na William Ruto walikuwa kwenye kambi pinzani huko Kenya kwenye uchaguzi wa 2007 lakini mwaka juzi wakaungana na kugombea kupitia muungano wa Jubilee na wakashinda [kama walishinda kihalali] na sasa hivi ni rais na makamu wa rais....
Kuhama kambi, kubadili itikadi, kubadili fikra, na kadhalika, si marufuku kwenye siasa bali ndo uhalisia wake.
Mbona kwenye maisha tu haya ya kawaida watu huwa tunabadili mawazo kila kukicha. Sasa kwa nini iwe dhambi mtu akibadili chama kwenye siasa?