Leo tunaaminishwa tatizo si mtu ila tatizo ni mfumo,tunaambiwa EL alikua fisadi,mla rushwa,mnyonyaji na muhujumu uchumi sababu ya mfumo.Huku tukiendelea kuona walewale waliotoka kwenye mfumo mbovu wakiendelea kumiminika kuandaa unaoitwa mfumo thabiti.Tena hawafuati chama ila wanafuata madaraka.
Inashangaza kuhama kwao kwa masharti.
"mimi nakuja ila nipeperushe bendera,au mimi nakuja ila tukishinda niwe PM".
Ni dhahiri kwa wana UKAWA kumuachia EL rungu awasaidie kuwapeleka magogoni wenyewe wameshindwa.Nidhahiri huwezi taka msaada kwa kitu ambacho wewe unakiweza.
Mwanzo tulizungumza mtu mmoja EL lakini sasa ni kundi la watu tena wenye tabia zakufanana,
Ni kweli mtu mmoja hawezi kukamilisha mfumo kwani mfumo unahitaji muunganiko wa watu,
Lakini sasa si EL pekeyake tena,kila uchao tunashuhudia watu kutoka kwenye unaoitwa mfumo mbovu kuja UKAWA hivyo kwa wingi wao wata play part kubwa kukamilisha mfumo,
Ikumbukwe pia ushahidi wakimaabara(DNA) imeonesha EL ufisadi upo kwenye damu,
Kama hivyo ndivyo kwa vyovyote iwavyo kwa nafasi alionayo ndugu EL ambaye tumepata uthibitisho wakimaabara kwamba ufisadi upo kwenye damu tutarajie mfumo uleule unaopigiwa kilele.
Ni wendawazimu watu waliohusika kwa kiwango kikubwa kuandaa mfumo unaoitwa Mbovu waje kutuletea mfumo thabiti kwa hili UKAWA mnatuhadaa wananchi na hapa ndipo shaka inapokuja kwamba mwenyekiti ameshadaka mshiko na kukiuza chama kwa mafisadi huku wengine tukiendelea kukaririshwa habari za mfumo.