Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Ndugu nisaidieni, hivi kweli ni sahihi kwa serikali kupanga mipango ya kuwa nyanyasa kwa namna yoyote ile raia wake? Binafsi nilidhani kazi ya serikali ni pamoja na kuwalinda raia wake?

Nilipo sikia sakata hili, nilidhani pengine Mengi kalishwa KASA habari hii si kweli, Yaani nipo ndani ya butwaa kusikia kwamba serikali inamtafuta waziri aliye vujisha siri hizo ikiwa na maana kwamba ni kweli walikaa na kupanga hivo!!

Mbona hii ina inatisha??? YAANI HII NI BALAA!!
 
1.
Mkuu FMES, jee unaamini asilimia miamoja kuhusu Uhuru wa Habari? Na kama una respect uhuru wa habari, nadhani utakubaliana na mimi kuhusu public judgement. Kama magazeti ya mengi hayako fair nadhani ni haki ya public kurespond na sio haki ya waziri.

- Hapa labda sina uhakika na unachokisema, Mengi binafsi amtuhumu serikali sio magazeti unless kuna something nina-miss kwenye hoja yako,

- Uhuru wa habari sio kuwa na nyeti za serikali kinyume na sheria, na sio kuituhumu serikali katika ishu ambazo zilipaswa kwenda kwenye sheria, alichofanya Mengi sio uhuru wa habari ila ameituhumu serikali wka tuhuma nzito sana!


2.
Swali langu kubwa ni mmoja tuu Mkuu, Jee unaona any wrong doing kutoka kwa Masha katika hii case? Na kama hivyo what is it?

- Labda wewe uniambie, maana so far yeye amesema ana-uphold sheria kama waziri wa serikali iliyotuhumiwa na some serious allegations na mwananchi Mengi, sasa mkuu ukinionyesha kwamba waziri yuko wrong kwa kusimamia sheria za jamhuri sitakua na tatizo kukubali, je unasema waziri yuko wrong kisheria na all his act so far kwenye hii ishu?
 
Hivi Siku 7 zimekwisha au la?....

Kwa Maoni yangu...Mengi Kama alikuwa na ushahidi kwanini Hakwenda Mahakamani...au ndio kutafuta attentions na sympathy za wananchi...?...Angeunguziwa Products zake kama Bakhresa ingekuwaje....

Sijui wapi Masha kazungumza hii issue ya Kodi dhidi ya Mengi...kwa kuwa Masha mlevi kuna uwezekano mkubwa akawa kaitoa hio statement ktk Vikao vya ULEVI...

Ikiwa Masha kaizungumza ktk VIKAO rasmi vya SERIKALI...basi hapo kuna mambo ya msingi ya kuyaangalia.....Nadhani pia kama Mengi anajua hili limezungumzwa huko, basi hata yeye anakhoufu kwenda Mahakamani asije ulizwa Habari hizi nani kakupa...na hapo ndipo mzozo utakapokuwa mkubwa!!!!.....Let us wait n see the GAME in the court.


Uko sahihi kuwa kama itakuwa kwenye vikao vya serikali ataulizwa katoa wapi habari kwa maana ni siri ya baraza .Lakini ushahidi kwa kesi ya kwanza kama ushahidi utakuwa umetolewa na kama alisema sheria sidhani kama ina mlinda Masha maana alicho comment ni kinyume na katiba ya Tz.

Kama watataka ku counter sue the guy of breaching gov . secret hilo ni jambo jingine .

Kuhusu kwenda mahakamani pia ni timing nyingine kama vile kuchinja kobe.Si unaona mpaka sasa haja taja jina wala kwenda mahakamani lakini waziri kijana tayari anajichanganya .Ndugu hizi ni mbinu za porini,kupata haki unapidi ujue sheria itakusaidiaje uipate hiyo haki ni cha kusema na wakati gani sio kukimbilia mahakamani hasa uki deal na mtu mwenye sehemu ya dola.
 
Mkuu Mengi kama watanzania wengine wanahitaji ulinzi,kama jinsi ulinzi ulivyoongezwa kwa Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano,JK.Mengi si mtu wa kwanza kutishiwa.......Kuna Spika wa Bunge,Dr.Mwakyembe na wengineo wengi.Hapa suala lililomkatisha tamaa Mengi na Watanzania wote kwa ujumla ni pale watu wanapojitolea kufichua maovu ndani ya Serikali ili kurahisisha utendaji lakini serikali hiyohiyo ndio inayofikiria na kupanga mikakati ya siri ya kuhujumu raia wake waliojitoa kuisaidia serikali.Swali langu,Mbona MAFISADI HAWAFILISIWI? BASI hata kusikia taarifa kwenye hivyo vikao vya siri kwamba wanataka kuwafilisi? Je ni kweli KUwashitaki akina Mramba na Yona ni nia ya dhati ya kupambana na Ufisadi au ni vita ya kisiasa ndani ya CCM.Sipati picha maana Waziri kama Masha hakupaswa kuwa na jazba katika kutoa kauli yake kuhusiana na madai ya Mengi,Je Masha kageuka Mahakama? Kama Mengi ameidhalilisha serikali ni kwa nini serikali isimshitaki Mengi ili yeye akatoe uthibitisho mahakamani? Mbona MIgomo ya walimu serikali mahakamani kama kawa.............kwa nini sio Mengi ambaye ameituhumu serikali ,ISIJE IKAWA YALE YA TICS NA KARAMAGI KWAMBA kikao cha baraza la mawaziri ndicho kilichoongeza muda.Hapa suala lililopo mezani kwetu ni kwamba kama serikali inaweza kufanya vikao na kulipana posho kubwa ambazo kimsingi ni kodi za wakulima watanzania na kuanza kujadili jinsi ya kufilisi watanzania wenzetu wanaofanya biashara zao bila kukwepa kodi,wanaotoa ajira kwa watanzania na hivyo kukuza uchumi wetu kwa kweli ni aibu kwa serikali.

Hivi ni makampuni mangapi ya madini,mafuta,mahoteli yanapata misamaha ya kodi......leo hii serikali inafikiria kumfilisi mtanzania anayelipa kodi

Hivi ni watanzania wangapi,vijana wangapi kutoka vyuo vikuu hawana ajira.......leo hii serikali inafikiria kumfilisi mtanzania anayetoa ajira kwa wazalendo.

Hivi ni watanzania wangapi ambao hawapati taarifa sahihi kuhusu mapato na matumizi ya kodi zao........leo hii serikali inafikiria kuhujumu vyombo vya habari vya mtanzania mwenzetu.

Hivi ni watanzania wangapi ambao wanakosa fedha kwa kuchangia gharama za masomo za vyuo vikuu kwa umasikini unaosababishwa na serikali yao..........leo hii serikali inatumia vikao halali na posho nono, fedha za walipa kodi kujadili masuala ambayo hayana tija kwa maendeleo ya taifa.

Hivi ni watanzania wangapi ambao hawakuwa na ujasiri kama mengi ambao mpaka sasa wamefilisiwa,wemefungwa magerezani au wamefukuzwa kazi........Hii ni hatari ninaamini hakuna marefu yasiyo na ncha,mambo haya hayajaanza leo wengi wamekwisha umizwa.Yale ambayo yapo chini ya Mamlaka ya Fisadi MASHA ameyafanya.,Bali hili la Mengi lilikuwa zito sana

MImi nadhani huu ndio muda muafaka wa kuzungumzia DEEP GREEN NA EMMMA ADVOCATES ILI MASHA atueleze.

KUHUJUMIWA KWA MENGI NA MASHA NI SAWA NA LILE LA MWANAHALISI NA WAZIRI WA HABARI NA MICHEZO.hiyo ndio serikalali yetu,inakimbia kivuli chake.
 
- Otherwise, akiwa UV-CCM Mwanza Lau amefanya mengi sana, infact alifikia mahali aliacha kazi IMMA na kuhamia Mwanza, mpaka alipopata ubunge ndio alirudi Dar na ni mchango wake kule kwenye commuinity za jimbo lake ndio ulioihsia kumpatia ubunge, kwa hiyo kwenye hili sina wasi wasi nalo kabisa kwamba Lau analitimiza kwa kiasi kikubwa lakini inaweza kwua sio kama ulivyotegema wewe mkuu.

IMMA wana branch Mwanza,na sababu kubwa ya kuwa huko ni biashara kubwa walionayo huko.Kuna IMMA House Mwanza
 
Afadhali kesi yenu iishe turudi kwenye mada,

Swali ni, je, ni halali kabisa serikali kukiri kupanga kumshughulikia raia wake kwa njia za uonevu? (rejea serikali kumtafuta waziri aliye vujisha siri yao)

Je hii haitutoshi kutuogofya wananchi na kutukosesha imani na serikali yetu?

Na naomba niongezee kwamba nimeona wachanche wakichukulia kwamba Masha alijieleza kwamba alitoa siku saba akiwa ana nia ya kum-protect Mengi.

Ukweli ni kwamba alisema alitoa siku saba akiwa na nia ya kuji-protect mwenyewe. Ambayo inaweza ikawa na ka-implication kwamba anajua (soma "anajua" sio "anahisi") kwamba shutuma ni zake na zina ka-ukweli. (kuna mtaalamu mmoja humu ndani alii-spot hii kitu vizuri sana).
 
Sipendi kuingia katika huu mjadala kwa kuwa tayari naona una mambo mengi ambayo sipendi kuyajadili kwa sababu za "KITAALAMU" ambazo baadhi yenu munazifahamu.

Lakini nina maswali machache ambayo pengine yatasaidia kuboresha mjadala;

1-Ninavyofahamu Waziri Masha ni mwanasheria mahiri na kijana msomi pamoja na kuwa na kasoro zake za kibinadamu kama tulivyo binadamu wote kwa hiyo je, kisheria alikuwa sahihi kutoa majibu aliyoyatoa kwa waandishi wa habari?

2-Kwa ninavyofahamu Masha ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, wizara ambayo chini yake kuna Jeshi la Polisi, Magereza na Uhamiaj kwa hiyo ninajiulizai, je, hoja ya Mengi ilikuwa inahusu maeneo yaliyo chini ya wizara yake? Kwa kuanzia polisi wanashughulikia makosa ya jinai ina maana kauli ya Mengi ina jinai?

3-Kama kuna jinai inaangukia katika sheria gani? maana kasema kuna waziri kijana amependekeza abambikiwe kesi na hajasema serikali imeamua/imekubaliana/imepokea ushauri kwa hiyo hata huo ushauri haifahamiki kama umekubaliwa ama ulikataliwa.

4-Waziri Masha kasema kwamba asipotoa ushahidi baada ya siku saba sheria itachukua mkondo wake, sheria ipi? Sheria ya Uhaini? Uchochezi? Kashfa? kusema uongo?

5-Taarifa ya Mengi ilihusu tuhuma za kubambikiwa kodi na suala la kutishiwa kuuwawa liliibuka wakati wa mijadala/maswali baada ya hitimisho lake kusema "Waziri huyo na wale wote wanaotoa vitisho" na baadhi ya waandishi wakaunganisha kwamba na waziri ametoa pia vitisho vya SMS jambo ambalo Mengi hakulisema katika taarifa na hata katika maswali na majibu, sasa Je, Masha na polisi (waliohojiwa na magazeti) walitumia nukuu gani kusema kwamba "polisi hawana taarifa za Waziri kumtishia Mengi"? Mbona wamejibu na kuandika mambo wanayoyafikiria ama wanayoyajua?

MAONI: Pamoja na maswali yangu hapo juu, kwanza kabisa kuna udhaifu mkubwa katika uelewa, uchambuzi, utafiti na uandishi wa waandishi wetu wa Tanzania tena hata wale wa vyombo vikubwa vya habari na hivyo mara nyingi naona baadhi ya migogoro na matatizo yanasababishwa na upotofu wa taarifa zinazotolewa katika vyombo vyetu vya Bongo. Waandishi wetu wanakosea na mara nyingi kupotosha sana mambo.

Katika upotoshaji ambao mara nyingi unatokana na uvivu, nakumbuka wakati Mkurugenzi wa TAKUKURU, Edward Hosea, aliposema kuna vigogo watafikishwa mahakamani kwa ufisadi, waandishi wakaandika "Vigogo wa EPA kufikishwa mahakamani" wakati Hosea hakusema ni wa EPA na alijua kabisa si wa EPA na waandishi walikuwa wavivu hata kufikiri kwamba Hosea hajawahi kutoa tamko kuhusiana na watuhumiwa wa EPA na hata Press Conf ya kina Mwanyika na IGP, Dk. Hosea hakuwapo. Hosea alikuwa akimaanisha Mramba na Yona na baadhi ya waandishi wakataja kuna mawaziri wawili na wakaendelea kusema ni tuhuma za wizi wa fedha za EPA bila hata kufanya marejeo katika magazeti ya THISDAY, KULIKONI na hata RAIA MWEMA waliowahi kuandika kuhusu kina Mramba kabla hata ya kushitakiwa kwao.

Mifano ni mingi lakini suala la Mengi na Masha pamoja na udhaifu wa hoja zilizoibuka waandishi wetu wanachangia kuchochea mgogoro huo.

*Jambo lingine muhimu ni kwamba kwa kuwa Masha amezungumzia "serikali itachukua hatua" kwa hiyo yeye ndiye msemaji wa serikali? kwa hiyo Wizara ya habari kupitia Maelezo wana kazi gani? Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu ina kazi gani?

Hoja yangu ya mwisho ni kwamba yaliyotokea kwa Masha sitaki kuamini aliyoniambia mtu mmoja kwamba Waziri huyo kijana, alishitukizwa maswali na waandishi wa TBC1 waliomhoji katika kipindi cha jambo na hakuwa amejiandaa kwani alikwenda kuzungumzia suala la Albino. Pamoja na kwenda kuzungumzia Albino, tayari alikwishapokea simu nyingi kuambiwa kwamba Mengi kamtaja, na yeye (Masha) bila kujipa muda (kama walivyo wakongwe wengi wa siasa) alitoa majibu ya haraka kwa TBC1 na sehemu kubw aya majibu yaliegemea zaidi kwa taarifa za simu alizopata na si kwa kusoma taarifa HALISI ya Mengi au hata angetumia muda kuwasiliana na Mengi. Masha alijiamini na akaonyesha kiburi na jeuri ya utawala kwamba polisi wote wa Tanzania wako chini yake na anaweza kuwaamuru, kwa kusema, "kamata Mike wa JF, kamata Mac wa JF, kamata Kubenea" na wakakamata kabla ya kujikuta wamechemsha. Amesahau cheo ni dhamana. Hivi kwa mfano angekuwa ni Kingunge, Kagasheki, Wasira, Nagu au hata Dk. Husein Mwinyi, wangetoa majibu sawa na Masha?
 
Mifano ni mingi lakini suala la Mengi na Masha pamoja na udhaifu wa hoja zilizoibuka waandishi wetu wanachangia kuchochea mgogoro huo.

Asante.

Je ni hulka ya waandishi (labda wa Tanzania) kupindisha au kuyakuza mambo/issues ili wauze magazeti bila kuproject associated impacts?

Wanahabari wako business oriented than profession/al oriented?

Wengine watasema Tanzania hakuna media na kama ipo basi it is crummy. Msemo huu ni kweli?
 
Nyongeza MUHIMU:


Kuna mtu amepiga simu na kusema maneno haya na ninamnukuu bila ku-edit:

"Tunajua Mzee Mengi ana huruma na anaweza kuingia makubaliano na Masha kwa hiyo, hata kama Mengi asipoutoa huo ushaihidi hadharani kwa sasa, ijulikane kwamba kwa sasa uko mikononi mwa watu wengi na mahali kwingi kwa hiyo hata wakiingia makubaliano na Mengi wajue iko siku na saa aliyoyasema Masha yatakuwa hadharani kwa njia ya kushitukiza."

Nilipotaka kuuliza maswali mtu huyo alikata simu na hadi sasa simu yake haipatikani.
 
Nyongeza MUHIMU:


Kuna mtu amepiga simu na kusema maneno haya na ninamnukuu bila ku-edit:

"Tunajua Mzee Mengi ana huruma na anaweza kuingia makubaliano na Masha kwa hiyo, hata kama Mengi asipoutoa huo ushaihidi hadharani kwa sasa, ijulikane kwamba kwa sasa uko mikononi mwa watu wengi na mahali kwingi kwa hiyo hata wakiingia makubaliano na Mengi wajue iko siku na saa aliyoyasema Masha yatakuwa hadharani kwa njia ya kushitukiza."

Nilipotaka kuuliza maswali mtu huyo alikata simu na hadi sasa simu yake haipatikani.

Hongera Halisi kwa kuwa na kichwa kizuri namna hiyo. Ingekuwa mimi ningesahau neno au ningetia neno m-badala katika maneno mawili matatu hivi. U mzuri kwenye kauli taarifa, umefikisha ujumbe kama ulivyousikia!
 
Mimi sio mwanasheria lakini sheria inasemaje kuhusiana na HAKI YA HABARI/TAARIFA kati ya mtoaji, mpokeaji na mwenye habari! Inavyoendelea sasa inaonekana ni kama lilikua tamko au kikao "nyeti" ndo kilikua kina-discuss hayo mambo! Nani aliitoa hiyo nyeti kwa Mengi! Its obviously ni wazalendo na wasio taka uonevu na ufisadi katika TAnzania hii ya leo lakini ambae alibahatika kuwa mmoja wa hao wakulu na hivyo kuingia kwenye hiko Kikao.

Lakini pia Mengi anapenda publicity stunt na jamii wa Watanzania wamuone kama mtetezi wa wanyonge lakini kikubwa mara nyingi kuonekana kwamba anaonewa na vyombo vya serikali ili shughuli zake ambazo ni "halali" ziendelee.

Japo hakumtaja jina, at last tumemjua ni Masha! Sasa huyu Bwana si wavutane mahakamani kama hawataki kutoa vielelezi ( supporting evidence) hadharani! Ili tupate ukweli?

Naamini Mengi amesema ukweli, na he can prove that in the court of law! Maana hiyo issue ni kubwa na inayohitaji Masha angekuwa ashajiuzulu! Au kwa sababu ni kilikua kikao nyeti kina splitting au divided responsibility:kwamba hiko kikao ni breeding ground for evasion of responsibility and inefficiency as "group" responsibility means every member feeling unaccountable?

It looks maybe there's a light at the end of the tunnel!
 
MAONI: Pamoja na maswali yangu hapo juu, kwanza kabisa kuna udhaifu mkubwa katika uelewa, uchambuzi, utafiti na uandishi wa waandishi wetu wa Tanzania tena hata wale wa vyombo vikubwa vya habari na hivyo mara nyingi naona baadhi ya migogoro na matatizo yanasababishwa na upotofu wa taarifa zinazotolewa katika vyombo vyetu vya Bongo. Waandishi wetu wanakosea na mara nyingi kupotosha sana mambo.

Katika upotoshaji ambao mara nyingi unatokana na uvivu, nakumbuka wakati Mkurugenzi wa TAKUKURU, Edward Hosea, aliposema kuna vigogo watafikishwa mahakamani kwa ufisadi, waandishi wakaandika "Vigogo wa EPA kufikishwa mahakamani" wakati Hosea hakusema ni wa EPA na alijua kabisa si wa EPA na waandishi walikuwa wavivu hata kufikiri kwamba Hosea hajawahi kutoa tamko kuhusiana na watuhumiwa wa EPA na hata Press Conf ya kina Mwanyika na IGP, Dk. Hosea hakuwapo. Hosea alikuwa akimaanisha Mramba na Yona na baadhi ya waandishi wakataja kuna mawaziri wawili na wakaendelea kusema ni tuhuma za wizi wa fedha za EPA bila hata kufanya marejeo katika magazeti ya THISDAY, KULIKONI na hata RAIA MWEMA waliowahi kuandika kuhusu kina Mramba kabla hata ya kushitakiwa kwao.

Mifano ni mingi lakini suala la Mengi na Masha pamoja na udhaifu wa hoja zilizoibuka waandishi wetu wanachangia kuchochea mgogoro huo.

Nakubaliana kabisa na maoni yako mkuu.

Mimi nadhani tatozi si la hawa wanahabari tu. Hawa wanahabari wanatoka katika jamii yetu, na wengi katika jamii hizi zetu ndivyo tulivyo. Kuna tatizo kubwa sana la kutofautisha ukweli (mambo yaliyothibitika) na na mambo ambayo hayajathibika (imani, speculations, maoni). Unasikia kitu, unatafsiri jinsi unavyoelewa, halafu unaichukulia tafsiri yako kama ndio ukweli, halafu unai-present kama ndio ukweli, na saa nyingine watu wakikuuliza umelitoa wapi unakuwa mkali kweli.

Ni rahisi sana kwa muandishi kuepuka kupotosha kwa kufanya mawili:
1. Kumnukuhu mtu kama alivyosema, na kuepuka kuongezea interpretation yake.
2. Kabla ya kuingiza intepretation yake, kumuuliza msemaji kama ndicho alichomaanisha.

Pia, waandishi wetu wengi ni waoga wa kuuliza maswali. Na saa nyingine wakiuliza unaweza kupata shida sana kujizuia kucheka, lakini insikitisha.

Kwa mfano kitu mwandishi wa ile habari ya "Barrick kujitoa tanzania" angefanya ni kumuuliza yule jamaa "je, unamaanisha mnataka kujitoa Tanzania?". Sasa yeye akasikia jamaa analalama, yeye akatengeneza hisia kwamba huwa jamaa wanataka kuondoka (yaani nashindwa hata kupata picha hii hisia ilitoka wapi), halafu akaamu kuandika hiyo intepretation yake kama vile ndio ukweli.

Ukitaka kujua hili ni tatizo kubwa, ona kwamba hiyo article ilipita kwa watu kadhaa, including mhariri, na hakuna aliyestuka. Hakuna aliyejiuliza hivi kuna ukweli hapa? Hakuna aliyejaribu hata kudadisi zaidi, au hata kumuuliza muandishi "e bwana huyu jamaa amekwambia wanataka kuondoka hapa?".

Ndio maana huku kwetu majungu yanaenea kwa urahisi sana, maana wapo wenzetu wengi wakotayari kuyatetea kwa nguvu zote hata kama hawawezi kuthibitisha wanayoyatetea.

Kuna rafiki yangu mwandishi wa shirika flani la habari la kimataifa, ukimkuta anaifanyia kazi story utaona raha yaani jinsi anavyohangaika kuutafuta ukweli. Kwa sababu anajua akiipeleka article yenye majungu yasiyo na uthibitisho uliosimama lazima article itarudi tu. Kama ni kitu kimesemwa na mtu na yeye hakuwepo, basi ni lazima apate kumhoji yeye mwenyewe au msemaji wake kuthibitisha, la sivyo hiyo story ndiyo imekufa. Very thorough and detailed.

Na nimmooja wa waandishi wawili ninaowafahamu ambao hawapokei vijibahasha baada ya press-conferences kamwe. Kama ulikuwa hujui, ni siri iliyowazi kwamba kwenye press-conference nyingi (za serikali na makampuni binafsi), waandishi huwa wanapewa vijibahasha waende navyo. Wewe nenda kwenye press conference nyingi utakuta waandishi wanasainishwa. Halafu waulize hayo majina na hizo signature ni za nini uone unavyopigwa siasa.

*Jambo lingine muhimu ni kwamba kwa kuwa Masha amezungumzia "serikali itachukua hatua" kwa hiyo yeye ndiye msemaji wa serikali? kwa hiyo Wizara ya habari kupitia Maelezo wana kazi gani? Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu ina kazi gani?

Hoja yangu ya mwisho ni kwamba yaliyotokea kwa Masha sitaki kuamini aliyoniambia mtu mmoja kwamba Waziri huyo kijana, alishitukizwa maswali na waandishi wa TBC1 waliomhoji katika kipindi cha jambo na hakuwa amejiandaa kwani alikwenda kuzungumzia suala la Albino. Pamoja na kwenda kuzungumzia Albino, tayari alikwishapokea simu nyingi kuambiwa kwamba Mengi kamtaja, na yeye (Masha) bila kujipa muda (kama walivyo wakongwe wengi wa siasa) alitoa majibu ya haraka kwa TBC1 na sehemu kubw aya majibu yaliegemea zaidi kwa taarifa za simu alizopata na si kwa kusoma taarifa HALISI ya Mengi au hata angetumia muda kuwasiliana na Mengi. Masha alijiamini na akaonyesha kiburi na jeuri ya utawala kwamba polisi wote wa Tanzania wako chini yake na anaweza kuwaamuru, kwa kusema, "kamata Mike wa JF, kamata Mac wa JF, kamata Kubenea" na wakakamata kabla ya kujikuta wamechemsha. Amesahau cheo ni dhamana. Hivi kwa mfano angekuwa ni Kingunge, Kagasheki, Wasira, Nagu au hata Dk. Husein Mwinyi, wangetoa majibu sawa na Masha?

Uko sawa kabisa mkuu. Mimi nadhani wengi, tukieka ushabiki pembeni, wanakubali (hata kama ni kwa kimoyomoyo tu) kwamba mshakaji alichemka angalau kidogo.

Kuhusu kama alishtukizwa na maswali TBC1, mimi hiyo ndiyo imebaki kama kitu pekee cha kunaelezea kwa nini alipitiliza vile. Nahisi tu kwamba kama angepewa maswali kabla, pengine angepata mda wa kujituliza, na hata kupata ushauri wa jinsi ya kuwakilisha, na pengine asingerauka namna ile. Imenifanya nijiuliza kama huyu jamaa ni smart kama wengi wanvyomuelezea? au pengine tatizo alilonalo mbele yake ni kubwa kiasi cha kuweza kumpanikisha kiasi kile?

Sasa hivi nalalia upande wa la pili ... kwamba tatizo aliloliona ni kubwa kuliko tunavyoliona sisi. He was in panic mode kwa sababu he didn't see what was comming, na hakuwa amefikiria vizuri nini cha kufanya.
 
Asante.

Je ni hulka ya waandishi (labda wa Tanzania) kupindisha au kuyakuza mambo/issues ili wauze magazeti bila kuproject associated impacts?

Wanahabari wako business oriented than profession/al oriented?
Kinachoniogopesha ni kwamba inawezekana ni uwezo mdogo wa baadhai ya wenzetu hawa katika kupambanua mambo, na kutenga facts na fiction.

Kama mtu anapindisha ukweli kwa makusudi akijua fika anachokifanya na anachotaka ku-achieve, hiyo inaniogopesha.

Lakini kama hajui analolifanya, hiyo inaniogopesha zaidi.

Wengine watasema Tanzania hakuna media na kama ipo basi it is crummy. Msemo huu ni kweli?

lol
Mimi hilo sijui
 
Hongera Halisi kwa kuwa na kichwa kizuri namna hiyo. Ingekuwa mimi ningesahau neno au ningetia neno m-badala katika maneno mawili matatu hivi. U mzuri kwenye kauli taarifa, umefikisha ujumbe kama ulivyousikia!

Uko sahihi, lakini kaka teknolojia imekua sana bongo huwezi kuamini ndio maana nasema baadhi ya viongozi wetu wanatambaa wakati watu wanakimbia na watashangaa na kuona watu "wachawi" wanapokuwa informed kwa mambo ambayo wanadhani ni siri. Dunia ya sasa hakuna tena cha siri.
 
Hakuna suala la nyeti za serikali kwenye vikao batili au siri ni batili. Viapo wanavyoapa hawa mawaziri na Katiba vinatosha kuifanya nyeti hiyo kutokuwa nyeti tena. Mf. Baraza la mawaziri haliwezi kaa likapitisha maazimio ya kuipindua nchi, au kuwauwa wananchi wake au kuuza nchi then still hizo zionekane ni nyeti za serikali.Nyeti za serikali ni lazima ziwe halali. Sasa kama kweli Mengi atakuwa kweli kaipata toka ndani ya baraza na ikathitishwa kuwa kweli ilizungumzwa then, lazima iangaliwe uhalali wake kwanza ndo Mahakama watatafsiri usiri wake. Sio kila kila kitu kinakuwa siri eti tu kwa kuwa sheria ipo.

Huyu Masha anaonekana ana shombo ya ufisadi na ulimbukeni wa madaraka. Tanzania mpya hii babake mpaka kufuli zitambana.
 
Uko sahihi, lakini kaka teknolojia imekua sana bongo huwezi kuamini ndio maana nasema baadhi ya viongozi wetu wanatambaa wakati watu wanakimbia na watashangaa na kuona watu "wachawi" wanapokuwa informed kwa mambo ambayo wanadhani ni siri. Dunia ya sasa hakuna tena cha siri.


Okay. Asante teknolojia. Nilidhani umesikiliza ujumbe then ukatuwalishia toka kwa kurecall toka kwa ubongo wako.
 
JK hana jinsi bali kumtosa Masha ameshakuwa bomu katika serikali ya Kikwete

Raza ajitosa mvutano wa Mengi, Masha

2008-12-10 16:07:15
Na Mwandishi Wetu

Mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar, Mohamed Raza, amejitosa katika mvutano uliopamba moto nchini sasa wa njama za kuhujumiwa kwa mfanyabiashara Reginald Mengi, kwa kusema kwamba anaungana naye katika harakati zake za kupambana na ufisadi.

Raza akizungumza na Nipashe kwa simu kutoka Zanzibar jana asubuhi, alisema ameamua kuzungumzia suala hilo kama salamu zake kwa siku ya Uhuru wa Tanganyika, kwamba anaungana na Mengi katika kuendeleza mapambano dhidi ya mafisadi kwa sababu Rais Jakaya Kikwete mwenyewe ameonyesha nia ya dhati kabisa kutokomeza ufisadi nchini.

Alimtakia kila la kheri Mengi na kumhakikishia kwamba Watanzania wapo nyuma yake.


Alisema Mengi ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, ikiwamo ya The Guardian Limited linalochapisha gazeti hili, atalindwa na Mungu kwa sababu anasimamia katika ukweli.

``Kila mmoja anakwenda kanisani au msikitini kumuomba Mungu, na ndiye atamlinda Mengi,`` alisema na kuongeza:

``Ufisadi umeharibu nchi. Maana ya Uhuru wa Tanganyika kama ilivyokuwa kwa Mapinduzi ya Zanzibar ni kuwapatia watu wao heshima; huduma bora za maji, umeme, barabara na afya.

Kuna wananchi vijijini hawana maji, hawana umeme, hawana barabara, lakini wapo matajiri waliojilimbikizia mabilioni ya shilingi kwa njia ya kifisadi. Hawa hawawezi kuachwa tu kwani uhuru hautakuwa na maana kwa wananchi.``


Alisisitiza kwamba kama ambavyo watu wengi wametoa kilio chao juu ya kampuni ya Kagoda Agriculture Limited ambayo imetajwa kujinufaisha na fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), ni vema wahusika wake wawekwe wazi. Kagoda iwekwe wazi,`` alisema.

Raza ambaye wakati wa utawala wa Rais wa Zanzibar, Dk. Salimin Amour, alikuwa mshauri wake wa masuala ya Michezo, alisema kwamba akiwa ni mwanachama mwaminifu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anaamini kwamba nchi haiongozwi na kundi la watu.

``Kundi haliongozi nchi, wala halitaongoza. Ni vizuri wazee wakae na kutafakari kwamba wakati tunasherehekea uhuru wa Tanganyika nchi inakwenda wapi?`` alisema na kusisitiza:

``Matajiri hawawezi kuwa wakuu kwa kila jambo. Leo ukitaka uongozi iwe ni udiwani au ubunge ni lazima utembee na mfuko wa Rambo uliojaa fedha ndipo upate uongozi. Sasa hii ndiyo misingi aliotuachia Mwalimu Nyerere?``

Aliwaomba wananchi kwa ujumla wao wamuunge mkono Rais Kikwete kwa sababu anapigania maslahi ya nchi, na kusema suala la kuweka ubinafsi mbele kuliko nchi ndilo linaangamiza taifa.


Alisema: ``Katika nchi hakuna urafiki.``
Raza alisema kwamba kuna matatizo ya makundi Tanzania, na akaonya haya yasipodhibitiwa ndiyo yataharibu nchi, alitumia usemi kikulacho ki nguoni mwako.`

Tangu Mengi atamke hadharani kwamba wapo watu wanatishia maisha yake kutokana na vyombo vya habari anavyomiliki kuwa mstari wa mbele kupambana na ufisadi, pia kufichua njama za Waziri mmoja kijana kutaka abambikiziwe kodi kubwa ili ashindwe kulipa hivyo afilisiwe, Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, amejitokeza katika kile kinachoonekana kuhusika katika kadhia hiyo.

Mengi alisema kwamba njama za kutaka abambikiziwe kodi kubwa zilikuwa zinasukuwa na waziri mmoja kijana, hata hivyo hakumtaja jina.

Siku moja baadaye Masha alijitokeza hadharani na kumpa Mengi siku saba kuwasilisha ushahidi kwake juu ya njama za kutaka kubambikiziwa kodi, vinginevyo angekumbana na nguvu za sheria.

Hata hivyo, baada ya kuibuka shinikizo kubwa kutoka kwa umma juu ya njama hizo, Masha alibadili kauli kwa kusema kwamba nia ya kumtaka Mengi atoe ushahidi ililengwa kumlinda dhidi ya njama hizo mbaya na si kumtisha.

Hadi sasa watu mbalimbali na vikundi vya kijamii wametoa kauli zao wakimpinga Masha, wengine wakieleza wazi kwamba kitendo chake cha kujitokeza hadharani kumjibu Mengi ni kielelezo kwamba anahusika na tuhuma za kusuka mpango wa kumbambikizia kodi ili kumfilisi hivyo kumnyamazisha kabisa katika vita yake dhidi ya ufisadi.

SOURCE: Nipashe
 
Hakuna suala la nyeti za serikali kwenye vikao batili au siri ni batili. Viapo wanavyoapa hawa mawaziri na Katiba vinatosha kuifanya nyeti hiyo kutokuwa nyeti tena. Mf. Baraza la mawaziri haliwezi kaa likapitisha maazimio ya kuipindua nchi, au kuwauwa wananchi wake au kuuza nchi then still hizo zionekane ni nyeti za serikali.Nyeti za serikali ni lazima ziwe halali. Sasa kama kweli Mengi atakuwa kweli kaipata toka ndani ya baraza na ikathitishwa kuwa kweli ilizungumzwa then, lazima iangaliwe uhalali wake kwanza ndo Mahakama watatafsiri usiri wake. Sio kila kila kitu kinakuwa siri eti tu kwa kuwa sheria ipo.

Huyu Masha anaonekana ana shombo ya ufisadi na ulimbukeni wa madaraka. Tanzania mpya hii babake mpaka kufuli zitambana.

Walipotaka kumbana Dk. Slaa kuhusu kuvujisha habari "nyeti" alitumia argument hii.Kwamba hata kama unakula kiapo cha baraza la mwaziri, mki discuss kitu illegal na ukaja kufanya whistleblowing the illegality of the original matter voids the strength of the oath.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom