Membe: Tunasubiri talaka Jumuiya Afrika Mashariki

Membe: Tunasubiri talaka Jumuiya Afrika Mashariki

Kusema kwamba wenzetu wamechukizwa na viongozi wa kidunia kututembelea huo ni upuuzi, viongozi wakubwa wanakuja Tanzania kwasababu wakati huu wanaweza kutuhadaa na kupata mikataba ninono kwa faida ya nchi zao kitu ambacho Kagame hawezi kufanya kwasababu ukweli ni kwamba ana akili. ni aibu kiongozi kutoa hoja kama hizo.

Lamsingi sioni tunachofaidika na hiyo EAC. kama wenzetu wamejitoa kwa nia ya dhati ya kiuchumi basi wataendelea, lakini kama tu ni kumkomesha kikwete wanajisumbua kwasababu wanaihitaji Tanzania zaidi ya tanzania inavyowahitaji, sisi tuendelee na msimamo wetu kwamba swala la Ardhi haliko kwenye EAC wakitutenga shauri yao, tusijitoe tuwaache watutenge sisi tujipange
 
wewe na membe ni vipofu.
mtajutia sana haya maneno ya kanga yanayotumiwa na membe badala ya kutumia namna ya kidiplomasia kutatua matatizo ya kimahusiano.

CCM mnaakili kweli?

Katika kujadili jambo hili tunatakiwa kuwa na maono ya kitaifa zaidi, kuangalia advantages na disadvantages. Katika ulimwengu wa leo ulivyo wa utanda wazi kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na social life sioni kama kuna jambo la kututishia kutokana na utashi wa hao Museven, Kagame na Kenyata.

Disadvantages zinazidiwa na advantages katika suala hili maana nchi zinazoizunuka Tanzania ni nane, na waliojitenga ni watatu kati ya nane, papo tu wanajamii kusini mwa Afrika.

Uimara wa Tanzania kulinda rasilimali zake ndio uliowafikisha hao wa utatu kufanya hilo, na binafsi naipongeza sana serikali kusikiliza maoni ya wananchi kulinda ardhi na rasilimali zetu, vingienvyo maeneo yote yenye vivutio, madini nk yangenunuliwa na wananchi kukosa ambao ardhi ndio moyo wa maisha ya wananchi walio wengi nchini.

Kikwete hakuteleza kumteua Samwel Sitta katika nafasi ya uwaziri Afrika Mashariki, pengine sitakuwa nimekosea kuwa maongozi ya Mungu.
 
Wakenya, Waganda na Warwanda ni waroho sana wa ardhi yetu. Na pia si watu wa kuwachekeachekea kabisa kwani ni hawana utu hata kidogo. Tukizubaa na kukubaliana na matakwa yao tutaishia kuwa watumwa ndani ya nchi yetu. Let them go, hatuna cha kupoteza na wala hatuwahitaji.

Tunaogopa kuungana na Waafrika wenzetu eti wanatamani utajiri wetu lakini tumekuwa radhi kuwaachia Wageni (Wazungu,Wachina,Waarabu) watuibie hizi rasilimali zetu kisha wakajenge kwao Ulaya,Asia na Arabuni.Juzi kuna Mchina inasemekana ameonwa na Madini ya TANZANITE.It doesn't make any sense to me!We are so mean and stingy against our fellow Africans but in the mean time we look very generous towards the Foreigners.This is totally absurd and ridiculous!
 
Nini tamko la Tanzania hapo?
nadhani sisi watanzania tuna matatizo ya kufikiri na kupambanua. Viongozi wetu wameamua kuwa tuna kwenda polepole na kwa tahadhari kubwa kwenye full shirikisho. Wenzetu wao wanataka kuharakisha wanao kwa kufanya hivyo kuna manufaa kwao. Sasa tunalalamikia kutengwa, basi tujiunge nao! Waziri naye hana jipya kutembelewa na obama, bush, clinton nk kumepunguza nini kwenye budget tegemezi? Ukipendwa sana na marekani juwa mwisho wake ni kiama kawaulize gadafi, sadam na wengine wengi tu! Tumebarukiwa kuwa sehemu nzuri kijiografia lakini tumeshindwa kuitumia fursa hiyo tunabaki kuringa na kushebedua tu
 
Kagame na Museveni si watu wa kuwaamini kamwe! Hawa ni jamii moja yenye lengo moja ya kutawalakwa gharama yo yote ile!

Lazima tujiulize Wanyarwanda, Waganda, Wakenya na hao Warundi wanaofuata upepo wameshirikishwa kiasi gani?

Enzi za Nyerere wananchi wengi kutokana na kuwa na upeo mdogo wa mambo ya kimataifa waliwaamini sana viongozi wao na hivyo cho chote kilichoamuliwa na viongozi wa wakati huo hakihojiwa na wananchi! Enzi zile kama Nyerere, Kenyatta na Obote wangeamua kuanzisha umoja wa kisiasa na kuziunganisha nchi hizi tatu wangefanikiwa bila upinzani mkubwa!

Huu ni wakati mwingine (Enzi mpya) yenye watu wanaofikiri kwa kina na kuhoji motive behind, faida na hasara za jambo lo lote. Kwa kuwa tunafahamu namna wote wanne (Kagame, Museveni, Kenyatta na Mkuruzinza) walivyoingia madarakani tuna kila saabu ya kuhoji na kikubwa zaidi kushirikishwa katika kila kitu watakachotaka kukitekeleza kwa niaba yetu wananchi!
 
nadhani sisi watanzania tuna matatizo ya kufikiri na kupambanua. Viongozi wetu wameamua kuwa tuna kwenda polepole na kwa tahadhari kubwa kwenye full shirikisho. Wenzetu wao wanataka kuharakisha wanao kwa kufanya hivyo kuna manufaa kwao. Sasa tunalalamikia kutengwa, basi tujiunge nao! Waziri naye hana jipya kutembelewa na obama, bush, clinton nk kumepunguza nini kwenye budget tegemezi? Ukipendwa sana na marekani juwa mwisho wake ni kiama kawaulize gadafi, sadam na wengine wengi tu! Tumebarukiwa kuwa sehemu nzuri kijiografia lakini tumeshindwa kuitumia fursa hiyo tunabaki kuringa na kushebedua tu

Hao walipendwa sana na Marekani ndiyo maana kiama kikawapata?. Mbona sielewi hoja yako?.

By the way, Tanzania hailalamiki kutengwa bali inalalamika taratibu za kuelekea shirikisho kamili hazifuatwi na baadhi ya washirika.
 
Delete futa kabisa huo umoja wa Eac
Kwanza hatufaidiki nao cha chochote kile
 
Kwa Mtanzania anayeona EAC ina manufaa ahamie Uganda au Rwanda. Tz imestukia hii kitu zamaniii... Musseveni yy anataka kufast track hiyo federation awe rais wake!
M7, Fidodido, Mzee wa jani na Mrundi ninyi oneni njia yenu bwana, Tz imeshtukia dili.
 
Hata kama tumeichoka CCM lakini linapokuja swala la kitaifa hawa vikaragosi wa Kitusi wasidhani Watanzania tutagawanyika.

Naunga mkono kauli ya Membe na ninaunga mkono msimamo wa Serikali kwenye hili. Wao mfano Kenya ardhi kubwa inamilikiwa na watu 20 tu akiwemo Kenyatta sasa upumbavu huo ndio wanataka kuuleta Tanzania.

Jamani tumalizane na Zanzibar kwanza ndio tuangalie mengine. Hiyo wizara ya Sitta ni waste of tax payers money, ivunjwe.
 
Hiyo talaka asubiri yeye asiseme tunasubiri
 


Enzi za Nyerere wananchi wengi kutokana na kuwa na upeo mdogo wa mambo ya kimataifa waliwaamini sana viongozi wao na hivyo cho chote kilichoamuliwa na viongozi wa wakati huo hakihojiwa na wananchi! Enzi zile kama Nyerere, Kenyatta na Obote wangeamua kuanzisha umoja wa kisiasa na kuziunganisha nchi hizi tatu wangefanikiwa bila upinzani mkubwa!

Huu ni wakati mwingine (Enzi mpya) yenye watu wanaofikiri kwa kina na kuhoji motive behind, faida na hasara za jambo lo lote. Kwa kuwa tunafahamu namna wote wanne (Kagame, Museveni, Kenyatta na Mkuruzinza) walivyoingia madarakani tuna kila saabu ya kuhoji na kikubwa zaidi kushirikishwa katika kila kitu watakachotaka kukitekeleza kwa niaba yetu wananchi!

Ni kweli Nyerere alikuwa analia kuanzisha hilo shirikisho la kisiasa nchi hizo ikiwemo za Rwanda na Burundi alizotaka ziwe sehemu ya Tanzania wakamdharau.Alikuwa yuko tayari hata kuachia ardhi iwe ya wote kama alivyofanya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.Hawakujali.Sasa hivi wao wanataka sisi hatutaki.Kama tulivyowavumilia walipokataa muungano wa kisiasa Nyerere aliotaka uharakishwe na sisi watuvumilie vile vile kama tulivyowavumilia wao walipogoma shirikisho la kisiasa.Wasinune tena wakome.Wao wenyewe walishatugomea miaka ya nyuma kuwa na shirikisho la kisiasa ambalo Nyerere alikuwa yuko tayari hata kuachia uraisi ashike mwingine kwenye hilo shirikisho la kisiasa kama lingeanzishwa.
 
nadhani sisi watanzania tuna matatizo ya kufikiri na kupambanua. Viongozi wetu wameamua kuwa tuna kwenda polepole na kwa tahadhari kubwa kwenye full shirikisho. Wenzetu wao wanataka kuharakisha wanao kwa kufanya hivyo kuna manufaa kwao. Sasa tunalalamikia kutengwa, basi tujiunge nao! Waziri naye hana jipya kutembelewa na obama, bush, clinton nk kumepunguza nini kwenye budget tegemezi? Ukipendwa sana na marekani juwa mwisho wake ni kiama kawaulize gadafi, sadam na wengine wengi tu! Tumebarukiwa kuwa sehemu nzuri kijiografia lakini tumeshindwa kuitumia fursa hiyo tunabaki kuringa na kushebedua tu

Tulijitoa COMESA ili tuweze kutembea pole pole kama sikosei na hadi sasa hivi sijui ni zaidi ya miaka mingapi tumeshatimiza tangu tujitoe?Cha kushangaza ni kwamba bado tupo pale pale,Hatuoni kwamba huu ndio wakati wa kuchangamana na wanaokimbia ili kama tulikuwa tunakwenda taratibu kwasababu ya uvivu au uzembe wetu basi tubadilike nasi tukimbie kama wenzetu?Tutakwepa hadi lini?
 
wewe na membe ni vipofu.
mtajutia sana haya maneno ya kanga yanayotumiwa na membe badala ya kutumia namna ya kidiplomasia kutatua matatizo ya kimahusiano.

CCM mnaakili kweli?

Sio kila jambo ni CCM vs CHADEMA. Hujajitambua bado.
 
Hao walipendwa sana na Marekani ndiyo maana kiama kikawapata?. Mbona sielewi hoja yako?.

By the way, Tanzania hailalamiki kutengwa bali inalalamika taratibu za kuelekea shirikisho kamili hazifuatwi na baadhi ya washirika.
Binafsi namuunga mkono Membe,ukisoma ilo bandiko vizuri utamwelewa Membe vizuri,ili shirikisho linaenda kwa stage tatizo wenzetu wanakiuka makubaliano,issue ya political,currency moja havijapitishwa bado ila wao wanalazimisha kuviingiza...
Hapa Tanzania kwanza bhana,siyo shamba la bibi hili.
 
Huyu jamaa wa ajabu sana badala ya kuwaambia hao jamaa wa Kenya, Uganda na Rwanda hizi issue anaenda zungumzia Clouds!! watasikia kweli? au ni yaleyale ya kusemea chumbani ukitoka nje kimya..
 
Back
Top Bottom