Membe: Tunasubiri talaka Jumuiya Afrika Mashariki

Membe: Tunasubiri talaka Jumuiya Afrika Mashariki

Hawa akina Museveni, Kagame na Kenyata baada ya kupima kina cha maji ya Kikwete na kukuta yana kina ambacho hawawezi wala kuthubutu kuogelea, wamejikuta ndani ya minority group kwa siku zijazo, hivyo kuamua kivyao kujaribu kutafuta njia mbadala kujinusuru.

Jambo moja la Msingi ambalo Kikwete atakumbukwa siku za usoni ni hili la kuitangaza Tanzania kwa mataifa, Tanzania ya leo si ile ya siku za nyuma iliyotumiwa na Kenya vivutio vyake kutumika kupitishia watalii Kenya.

Binafsi naona tu njia walizotumia ni utashi wa viongozi wa juu wa nchi na wala si matakwa ya wananchi wao, hivyo mambo ya uchumi wa dunia ya leo unabaki kuwa huru na katu huwezi Kikwete hawezi niwekea mipaka mie kupitishia mizigo yangu bandari ya Beira - Msumbiji au kwengineko ndivyo yatakayowapata hawa viongozi wa utatu.

Tanzania inahitaji tu kuboresha njia za usafirishaji na hivyo ukaribu wa bandari ya Tanzania kwa nchi za Rwanda na Burundi una nafasi bado. Uganda nao wako katikati, lakini kuna kilichowavutia wakati ule kupitishia mizigo yao bandari ya Dar sijui kama sababu zimetoweka kwa hoja zipi.

Tishio la ugaidi la Wasomali lisipothibitiwa kutosha ni kitu kinachoweza kusitisha mipango ya kutumia bandari ya Mombasa.

Mkuu kuna njia njingi za kuzuia importation kutoka nchi fulani.Ni rahisi kwa nchi hizo kupandisha Import Tarrifs ili ku discourage importation from Tanzania.Lakini hili hua linafanyika kwa bidhaa ambazo sio necessities kwa sababu ukipandisha tarrifs kwa necessities ambazo nchi yako lazima ifanye importation utakua uanatengeneza njia ya Inflation.
 
Kwani muungano wa tanzania una ridhaa ya wananchi wake?huwa nawashangaa watanganyika wametolewa eac wanalalamika mbona z'br ikitaka kujitoa kwenye muungao inakuwa nongwa?kama tanganyika mmetolewa kwenye eac basi iachieni zanzbr huru ijiunge.

Kosa ni kurudia kosa.
 
Mkuu kuna njia njingi za kuzuia importation kutoka nchi fulani.Ni rahisi kwa nchi hizo kupandisha Import Tarrifs ili ku discourage importation from Tanzania.Lakini hili hua linafanyika kwa bidhaa ambazo sio necessities kwa sababu ukipandisha tarrifs kwa necessities ambazo nchi yako lazima ifanye importation utakua uanatengeneza njia ya Inflation.

Mkuu,

Tariff haziwekwi kienyeji they must adhere international trade convention and guideliness za WTO na huwezi kuweka tariffs kiholela unaweza kuathiri hata uchumi wa nchi za kimataifa. Vile vile tariffs ukiweka unaencourage trade wars kwani Tanzania inaweza kuweka tariffs and quotas kwa nchi husika matokeo yake pande zote mbili zikaathirika kiuchumi. Mfano Tanzania inafanya biashara kubwa sana na Kenya sisi tukiagiza finished goods wao wakiagiza raw materials. Sasa hivi Tanzania ndio inalisha nchi za Afrika Mashariki na ukiweka quotas na tariffs our neighbours may be shooting on their own foot bila ya kujijua.
 
Wakat kagame na m7 wanafanya mambo yao kwa utash wa kisiasa Tz ijkite kuboresha miundombinu yake. Hakuna mfanyabiashara atakaekubal kupatata hasara kwa kupitishia mzgo wake long way eti tu kwa sababu political figures wanataka iwe hvo. Kuhusu political federation, haitaweza ku survive long kwan ukiangalia kenya, Rwanda na Burundi bado wanasumbuliwa na jnamz la ukabila. Lakini pia kagame na m7 wanaweza kugeukana baadae kwani wote wanauchu wa madaraka.
 
Nadhani hili tunaloshuhudia leo hii ni Kosa lililofanywa na Tanzania wakati wa kuandika Mkataba wa Jumuiya. Pamoja na umakini wa namna hatua ya Shirikisho ilivyowekwa kwenye Mkataba wa Jumuiya, lakini kulifanyika kosa kuruhusu hatua ya Shirikisho kuwa sehemu ya Muunganiko wa EAC. Kimsingi ilitakiwa Mkataba uishie hatua ya Single Market, then kungewekwa kiashiria kwamba Nchi Wanachama zitajadili Mkataba upya(Mkataba wa Jumuiya siyo wa Shirikisho) ikiwa zitahitaji kuendelea na hatua za juu zaidi baada ya kufikiwa kwa Single Market. Iwapo Mkataba ungekuwa hivi, kusingekuwa na habari za kuharakisha Shirikisho, badala yake Nchi zingekuwa serious kufikia Single market, Hata hivyo bila shaka kuaminiana kulikuwa kukubwa sana wakati wa majadiliano ya Mkataba.

Maana hizi Jumuiya za kisasa za Kikanda Afrika zinatokana na idea ya Lagos Plan of Action/ na Abuja Treaty lakini zote hizi hakuna sehemu ambako zinabainisha Shirikisho la Kisiasa kwa level ya Kikanda, ila United States of Africa kwa kuunganisha kanda zote. Je ni kwanini kulikuja wazo la Shirikisho la Kisiasa? Kwani kujenga mtandao wa Barabara, Reli na Customs area kunahitaji Shirikisho la Kisiasa?
 
Mkuu kuna njia njingi za kuzuia importation kutoka nchi fulani.Ni rahisi kwa nchi hizo kupandisha Import Tarrifs ili ku discourage importation from Tanzania.Lakini hili hua linafanyika kwa bidhaa ambazo sio necessities kwa sababu ukipandisha tarrifs kwa necessities ambazo nchi yako lazima ifanye importation utakua uanatengeneza njia ya Inflation.

Mkuu,

Tariff haziwekwi kienyeji they must adhere international trade convention and guideliness za WTO na huwezi kuweka tariffs kiholela unaweza kuathiri hata uchumi wa nchi za kimataifa. Vile vile tariffs ukiweka unaencourage trade wars kwani Tanzania inaweza kuweka tariffs and quotas kwa nchi husika matokeo yake pande zote mbili zikaathirika kiuchumi. Mfano Tanzania inafanya biashara kubwa sana na Kenya sisi tukiagiza finished goods wao wakiagiza raw materials. Sasa hivi Tanzania ndio inalisha nchi za Afrika Mashariki na ukiweka quotas na tariffs our neighbours may be shooting on their own foot bila ya kujijua.

Yeah, uko sahihi Mdondoaji. Suala la Tariffs sio kiholela. Kimsingi kila nchi ime-commit Tariff Bound kule WTO, na huwezi kupandisha applied tariffs zako zaidi ya kiwango hiki ulicho-bound. Iwapo utataka kubadilisha Tariff Bound zako, huna budi kupata ridhaa kutoka kwa nchi zote 159 wanachama wa WTO na itakubidi ufanye "compesation" kwa baadhi ya Nchi zitakazoathirika (Transparency adherence). Haitoshi, Trade Policy ya kila Nchi mwanachama huwa zinafanyiwa Review na WTO kila baada ya miaka 6 (kwa nchi zetu changa); hivyo si suala la kuamka na kuamua. Vilevile sidhani kama Quota-import basis haijafutwa na WTO hivyo hai-apply tena nowdays. Kadhalika suala la retaliation nalo lina athari zake
 
Binafsi nimekua mmoja wa wale ambao nachangia sana kuhusu EAC nikiwa na msimamo kwamba tunahitaji EAC na wao wanatuhitaji.

Sababu anazo toa Membe kwa maoni yangu ni nyepesi sana,naamini hata yeye anafahamu alikua anaongea siasa zaidi kuliko uhalisia. Ardhi ktk Katiba yetu ya sasa haiwezi milikiwa na mgeni yoyote! Jibu ni wazi!

Muungano wa kisiasa ni wazi ni jambo ambalo linatakiwa kuwa mwisho kabisa. Lakini sisi tumekua hata yale ambayo tulikwisha kubaliana na majirani tunavuta mjguu! Na niseme sitashangaa hatua hii ikazusha mgogoro zaidi kati ya Tanganyika na Zanzibar. Sauti za Wazanzibari zitasikika zaidi wakitaka kujitenga na Watanganyika ili wajiunge na EAC kama mwanachama kamili,

Mengine eti kwasababu ya kupeleka majeshi DRC na Mtanzania kuchaguliwa kuwa SG wa SADC naona ni sababu hafifu sana! Nimekua natoa maoni yangu kwamba hakuna ukanda wenye uhaba wa ardhi kama SADC! Sasa sijui na hawa wakianza kuzunguzia ardhi tutajitoa huko ama?
 
Tunaogopa kuungana na Waafrika wenzetu eti wanatamani utajiri wetu lakini tumekuwa radhi kuwaachia Wageni (Wazungu,Wachina,Waarabu) watuibie hizi rasilimali zetu kisha wakajenge kwao Ulaya,Asia na Arabuni.Juzi kuna Mchina inasemekana ameonwa na Madini ya TANZANITE.It doesn't make any sense to me!We are so mean and stingy against our fellow Africans but in the mean time we look very generous towards the Foreigners.This is totally absurd and ridiculous!

Mchango mzuri mkuu,na hii itafanya tuendelee kutawaliwa na wageni milele tena kwa manyanyaso makubwa,serikali kuwafukuza watz na kuwapa wageni ni sawa ila akichukuwa mwafrka mwenzio ni haramu,bado tunahitaji ukombozi wa fikra.
 
Kuhusu jinsi gani kitendo cha kuwapiga M23 kinavyodhoofisha muungano alisema: “Kwa sababu wale M23 Tanzania inakwenda kwa principle (misingi) inayosema tunapoona nchi ya Afrika Mashariki au ya Sadc inakwenda kinyume cha matakwa ya wananchi au haifuati kanuni za uongozi bora, sisi huwa tunaingilia, siyo maana kwamba tunavunja Jumuiya Afrika Mashariki.”

Kumbe Tanzania ndio Marekani (polis) ya EAC.!!!???
 
Nimekuelewa sana Membe kwa kucheza na psycology ya hawa wahuni na sitashangaa baada ya kikao chao cha siri huko Kigari mwezi ujao sie huku tukaanda bunge letu kikao kijacho kupitisha azimio la nchi kujitoa rasim eac

Wanaume wanakutana Kigali mwezi huu( tarehe 28 na 29). Kanyaga twende dead weights achana nao.
 
Wakenya, Waganda na Warwanda ni waroho sana wa ardhi yetu. Na pia si watu wa kuwachekeachekea kabisa kwani ni hawana utu hata kidogo. Tukizubaa na kukubaliana na matakwa yao tutaishia kuwa watumwa ndani ya nchi yetu. Let them go, hatuna cha kupoteza na wala hatuwahitaji.
Kuondoka hawa jamaa ni ngumu sana,inawezekana kwa nchi zao kusepa,lakini raia wao tunao wengi sana humu nchini mwetu na wengine wakiwa na uraia kabisa wa nchi yetu tena ambao umepatikana kwa mizengwe,hawa jamaa wana vitambulisho vya kupigia kura tunao tele humu uraiani na wengine wanamiliki mapande makubwa sana ya ardhi kwa kutambulika kama watanzania.
 
Tujenge njia zetu kuu za uchumi ikiwepo miundombinu bora halafu tutapata geographical favor nao wao watakuja tu
 
Apa hakuna cha U ccm wala upinzani! Lazima tujue dhamira za hawa viongozi wa KENYA na UGANDA km mlifatilia mahojiano ya Prof Paramagamba Kabudi jinsi ni kwanini EAC ya zamani ilivunjika basi usishangae na ya sasa kuvunjika unless TZ iwe mburuzwaji na hawa....Mie nadhani tumepata picha halisi ya nini cha kufanya lets them go
 
Kiongozi ukiwa unaongozwa na Wananchi wako ni hatari.Kuwa Kiongozi inamaanisha kuongoza njia.Kuna baadhi ya mambo mazito Wananchi hawana uelewa nayo wa kutosha maana tungetumia busara hiyo hiyo ya kuheshimu MAONI ya Wananchi nahisi leo hii tungekuwa bado tupo katika mfumo wa Chama kimoja.Watanzania hii mentality yetu ya kubadilika pole pole mno wakati sehemu nyingine za Dunia zinabadilika kwa kasi.Binafsi nafurahishwa na hatua za mageuzi ya kiuchumi zinazochukuliwa na Rwanda na hasa ile mipango yao ya kujenga jiji jipya na la kisasa kabisa la Kigari pamoja na kuanzishwa kwa matumizi ya IT bure ambayo inalenga kutengeneza mazingira mazuri ya kibiashara na uewekezaji Nchini Rwanda.Hizi ndio faida tungeweza kuzipata ktk EAC kupitia kubadilishana uzoefu na Nchi nyingine.

Kubadilishana uzoefu wa mambo ya kiuchumi lazima tuungane kisiasa?
 

Usipotoshe. Hoja ya Tanzania iko wazi labda uamue tu kutotaka kuielewa. Kuungana ni process sio announcement na hasa kama kuungana kwenyewe ni kwa Nchi. Tanzania msimamo wake uko wazi kwamba Muunganiko wa kisiasa utokane na kuimarika kwa muunganiko wa kiuchumi; Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja na Umoja wa Fedha. Hivi leo hizi nchi ziko katika hatua ya Soko la Pamoja, kabla hatujaenda mbali, unadhani Afrika Mashariki imefikia hata vigezo vya utekelezaji wa Soko la Pamoja? Au unataka kutuambia ni feasible kuanza Shirikisho la Kisiasa pasipo kuimarika kwa misingi ya Kiuchumi? Uchambuzi mzuri sio ni kupinga kila kitu. Au tupe japo mfano wa Mtangamano wowote wa Kikanda duniani ulionza na Siasa kisha kuelekea kwenye Uchumi. Hata hizo Taasisi za kisiasa zitatekelezaje maujukumu yake kama hakuna Economic Integration?

You nailed it mate, thanks.
 
Kusema kwamba wenzetu wamechukizwa na viongozi wa kidunia kututembelea huo ni upuuzi, viongozi wakubwa wanakuja Tanzania kwasababu wakati huu wanaweza kutuhadaa na kupata mikataba ninono kwa faida ya nchi zao kitu ambacho Kagame hawezi kufanya kwasababu ukweli ni kwamba ana akili. ni aibu kiongozi kutoa hoja kama hizo.

Lamsingi sioni tunachofaidika na hiyo EAC. kama wenzetu wamejitoa kwa nia ya dhati ya kiuchumi basi wataendelea, lakini kama tu ni kumkomesha kikwete wanajisumbua kwasababu wanaihitaji Tanzania zaidi ya tanzania inavyowahitaji, sisi tuendelee na msimamo wetu kwamba swala la Ardhi haliko kwenye EAC wakitutenga shauri yao, tusijitoe tuwaache watutenge sisi tujipange
Akili kama yakwangu japo nakuzidi kiduchu tu!
 
Kuondoka hawa jamaa ni ngumu sana,inawezekana kwa nchi zao kusepa,lakini raia wao tunao wengi sana humu nchini mwetu na wengine wakiwa na uraia kabisa wa nchi yetu tena ambao umepatikana kwa mizengwe,hawa jamaa wana vitambulisho vya kupigia kura tunao tele humu uraiani na wengine wanamiliki mapande makubwa sana ya ardhi kwa kutambulika kama watanzania.

Kama unawajua wapo kiharamu basi walipoti kunakohusika na kama huwezi ni PM majina yao na wako sehemu gani mimi nitalimaliza hili suala.
 
Kiongozi ukiwa unaongozwa na Wananchi wako ni hatari.Kuwa Kiongozi inamaanisha kuongoza njia.Kuna baadhi ya mambo mazito Wananchi hawana uelewa nayo wa kutosha maana tungetumia busara hiyo hiyo ya kuheshimu MAONI ya Wananchi nahisi leo hii tungekuwa bado tupo katika mfumo wa Chama kimoja.Watanzania hii mentality yetu ya kubadilika pole pole mno wakati sehemu nyingine za Dunia zinabadilika kwa kasi.Binafsi nafurahishwa na hatua za mageuzi ya kiuchumi zinazochukuliwa na Rwanda na hasa ile mipango yao ya kujenga jiji jipya na la kisasa kabisa la Kigari pamoja na kuanzishwa kwa matumizi ya IT bure ambayo inalenga kutengeneza mazingira mazuri ya kibiashara na uewekezaji Nchini Rwanda.Hizi ndio faida tungeweza kuzipata ktk EAC kupitia kubadilishana uzoefu na Nchi nyingine.

Huo siyo uongozi bali ni Udikteta wakudhani wananchi hawaelewi ila kiongozi anaelewa na hiyo ndiyo kanuni ya Viongozi madikteta! kwa Rwanda tunawatakia kila raheli ktk kuanzisha kiagali mpya na Internet mitaani! sisi tuna mambo yetu na changamoto zetu ambazo sol zake siyo za kukopy kutoka Rwanda!Kama shirikisho la EAC watz wengi wananchi wamelikataa na ndiyo wenye nchi siyo viongozi.
 
Back
Top Bottom