Membe kuwania urais 2015...

Membe kuwania urais 2015...

bernard-membe-165x300.jpg

Nimeona nami nije na style ya Mwanakijiji ya kuwapa Vitendawili mvitengue.

Wakati masakata ya akina Sitta na wenzie yanawaweka watu bize..huyu bwana has been busy na mambo mengi tuuu ambayo ni sinister na yanaenda na kinyume na NATIONAL INTEREST na NATIONAL SECURITY


Sasa hiki ni kitendawawili ambacho naamini GREAT THINKERS na INSIDERS wataweza kukitengua



JF home of GREAT THINKETS & INSIDERS


btw
tegemeeni influx wale watetezi wake wa wakati wa sakata la dili lake la Vitambulisho


..............Wewe GT unaharibia watu NIA zao oohh hooo..........
 
Mimi nadhani huyu jamaa ni tishio la Lowasa, RA, Mudhihiri, na mafisadi wengine wanoona kwamba ana nafasi ya kuukwaa ukuu wa nchi na hiyo ikitotekea wamekwisha!! Kama sio tishio lao wala hasingekuwa anajadiliwa, na kadri tunavyomjadili ndivyo tunavyompandisha!!

Uongo, fitina, na uzushi zote ni kete za good politicians. Leteni hoja mzito against this man, if any.

I think JK ana kila sababu za kujivunia kwa Membe; unfortunately JK hasikii ushauri na ni mwoga wa kivuli chake. So far Membe ni miongoni mwa mawaziri wachache sana ambao sio waoga wa kuongea na wandishi wa habari na kuwapa msimamo wa serikali na kuacha wananchi wamchambue kadri wapendavyo. Mwenyewe JK hili limemshinda, matokeo yake Membe anakazi ngumu ya kuongelea hata mambo ambayo hayako kwenye wizara yake na kujaribu kuu cover uozo na mapungufu ya JK.

Nimemsikia Membe akiongea radioni several times, the guy can speak what he thinks is right na sio mwoga kutoa msimamo wa serikali, hata kama wananchi wataukataa. To the contrary nikamsikia Pinda akilialia bila kutoa msimamo wa serikali, nimemsikia Pinda akiwa kama analyst badala ya kutoa msimamo wa serikali. Nikamsikia JK, yeye hana flow ya thoughts na wakati mwingine nilitamani nimwekee maneno kinywani mwake mana anakigugumizi cha mawazo.
 
I like the kigugumizi cha mawazo analogy. I may borrow it from time to time.
 
WazeeSijui GT anaelekea wapi, lakini wafuatiliaji wa mambo ya Magogoni wanaweza kuwa na haya ya kusema kuhusu Membe:-Amejihusisha na suala la dual citzenship, na suala hili ni divisive (National na security interests zipo hapa)-Amejihusisha sana na suala OIC (national, security and constitutional interests zipo). Actually hili ni bomu la petroli.-Amejihusisha na suala la mgombea binafsi kwa kumwaga fitna nyingi na kuichonganyisha mahakama, bunge na serikali.-Ana deal moja kubwa inaendelea na serikali ya Libya ambayo details zake haziko wazi. Kukosekana kwa uwazi kwa deal hii, ni kichaka cha GT kuzua lolote....Kwenye matrix za siasa kuna mvutano kati yake na kundi la EL. "Kumalizika" kwa mjadala wa Richmond bila madhara makubwa kwa EL, kunatishia nafasi ya Membe kuelekea Ikulu 2015. Lazima siku za usoni aonekane anacheza rafu ili kuhakikisha suala la Richmond linaibuka kwa njia nyingine ili kuziba nafasi ya EL. Of course JK anachekelea kwa chati anapoona marafiki zake waliomweka madarakani wanaparurana na kamwe hawezi kufanya kosa kusema ana makosa.
 
Muungwana na Membe ni marafiki wa kutupwa..yote mengine ni unafiki tu...unajua unaweza ukawa na best friend ila hukawa unamuona ni mtu wa masihala na asiyeaminika coz unazijua tabia zake na linapokuaj suala la kumkabidhi aliende familia yako au malia haumpi na kumchagua mtu wako wa karibu..ndiyo ilivyo kwa jk,membe na EL..Muungwana na EL ni marafiki wa kutupwa ila Mkwere hamuamini kabisa Mmasai..so lazima Membe achukue kijiti
 
Mimi nadhani huyu jamaa ni tishio la Lowasa, RA, Mudhihiri, na mafisadi wengine wanoona kwamba ana nafasi ya kuukwaa ukuu wa nchi na hiyo ikitotekea wamekwisha!!=.
SITAKI KUAMINI KUWA NI TISHIO,
ninachoamini Membe anatamani sana madaraka, anayataka kwa udi na uvumba kwa gharama za umaarufu binafsi, maana Membe huwa anatoa maagizo hata kwenye Idara ama Wizara zisizo muhusu, anajidai yeye ndio msemaji wa JK, KWELI HUYU SIONI KAMA ANATOFAUTI SANA na MKAPA katika udikteta, kujiona anaakili kuliko wenzake, hapendi vyombo vya habari, sishabiki wa kukosoana,, anavisasi zaidi ya Lowassa, ni mtu wakuogopwa kama ukoma katika madaraka ya Taifa hili.
 
sijawahi kukutana na waziri mpenda sifa na muongo kama MEMBE kwenye maneno matano chukua moja. watu wa karibu na huyu bwana mwambieni aache kudanganya watu,uongo wake nadhani ni wa kuzaliwa au kurithi.
For me, samahani lakini mababa na mabibi, mwanaume akishajipodoa kama ambavyo huyu jamaa anavyojipodoaga namwona hafai sipendi hata kumwona na hivyo namwona ni ndumila kuwili asiye na msimamo.
 
NINA SWALI HAPA:

Hivi kuna kiongozi MUISLAAM ambaye alishawahi kushambuliwa na Game Theory?

Naomba jibu la ndiyo au hapana kama una uhakika ili niweke rekodi zangu sawa. Tafadhali usiingize story zaidi au maneno mengi ambayo mie siyataki. Jibu fupi tu nahitaji.
 
Watu wa Usalama wa Taifa wamekamata vyeo karibu vyote katika serikali yetu kwa muda wote huu tangu tupate uhuru. Tulipo na tunakoelekea kama taifa ni kitendawili. Membe wa nini tena?
 
Zungumzeni yoote mnayoyataka lakini mimi binafsi bado namchagua Membe kuwa mmoja wa viongozi bora tulowahi kupata, sema tu anafikiri tofauti sana na Wadanganyika wengi. Na sababu kubwa ni kwamba hata wasomi wetu bado wana fikra za Utumwa, elimu yao ya kuelewa ni duni kwa sababu wengi wao wamefanya kukariri elimu yao kama ilivyoandikwa ktk vitabu..

Membe kafanya kipi cha ajabu?.. Vitambulisho vya Uraia!.hamtaki nambieni why? na mnipe mfano wa nchi yeyote huru inayofanya hivyo muonavyo. Je, ni hilo deal na Libya kuna ubaya gani!...Je mnajua ni mikataba mingapi ambayo mwalimu na Mwinyi waliingia mikataba na Libyapasipo nyie kufahamu kitu! Ama ni swala la OIC, kuna tatizo gani kulizungumzia ikiwa muswada umewakilishwa...hii kama sii udini wa fikra zenu kipi kingine! bila shaka Ufinyu wa kuelewa.

Kwa nini kwanza msijichunguze nyie wenyewe kuangalia fikra zenu zilivyopwaya ktk dunia hii ya leo..
Katika mjadala wake wa Dual citizenship niliwasoma wasomi wetu jinsi wanavyofikiria na hata yeye Membe alipokuwa akitoa hoja zake hawakumwelewa kabisaaaa! Kifupi ule mjadala ulitoa picha halisi ya wasomi wetu ambao matamanio na husda ya nafsi zao ndio kumejenga elimu yao..

Binafsi namjua Membe toka akiwa Ubalozini Canada na nitasema tena hakuna watu waliokuwa karibu na wananchi kama Membe, Aziz, Mama Chipungahelo, na sasa hivi Richard Tibandibage na Sokoine.. Hawa ni watu walioonyesha mwamko mkubwa sana ktk uongozi na wanazitumia vizuri nafasi zao ktk madaraka toka wakiwa ngazi za chini..na kwa bahati mbaya hawa wote hawakupendwa toka utawala wa Mkapa.

Isje kuwa hizi ni mbinu za watu wanaotafuta sifa..Membe ni mmoja wa viongozi bora ktk nafasi hiyo kwa sababu ndiye pekee ktk nafasi hiyo ameweza kuweka sera zinazowahusu Watanzania. iwe mnazipenda ama hamzipendi lakini he is the only one amesimama kuhakikisha baadhi ya maswala mazito na yenye utata yanazungumziwa na pengine kupewa sheria. Mawaziri wote wa nje siku zote wamekuwa wakikimbia hoja, hakuna aliyesimama ama kuzungumza kwa maslahi ya wananchi ktk maswala mazito ya jamii, zaidi ya kuwakiliwa nchi na siasa zetu nje...

What else mnachokitaka toka kwa Waziri wa mambo ya nje? awe kimya kama waliopita wakiwakilisha tusichokifahamu?..Kama unapingana na Mheshimiwa Membe weka hoja zako hapa wazi tuzijadili na toa mwelekeo unaofaa na sababu zake ili nasi tuyaone makosa ya Mh. Membe..Mnamwita mwongo tufahamisheni uongo wake uko wapi na utaathiri vipi maslahi ya nchi yetu..

Aaaaah watu wa Mkapa jamani hawaishi kujenga fitna wakiona urafiki wa JK na Membe kuwa sababu ya kupewa madaraka wakati wao walipeana nafasi kufuata koo za kuoleana nyumba moja...
 
...... mimi binafsi bado namchagua Membe kuwa mmoja wa viongozi bora tulowahi kupata, sema tu anafikiri tofauti sana na Wadanganyika wengi..........

Mkandara naomba kutofautiana na wewe na nafsi yako. Kati ya viongozi bora kwa kizazi kijacho cha Tanzania ni Mh learned brother L Masha. Lipi la ajabu amewahi kufanya? Kam si kuwa kwake Msukuma, angeweza kuwa successor wa Kikwete.
 
Mkandara,

Unaweza kunipa habari juu ya hii habari ya Libya kama siyo siri?

Mwisho, naomba maelezo kidogo (ukiweza zaidi) juu ya huyo Sokoine.

Nimekuwa nikisikia sifa zake kwa ufupi tu. Labda kuna haja ya kumrudisha nyumani amalizie kazi aliyoacha Eddy Moringe Sokoine? Anaweza kuja kuwa Putin wetu eti......
 
Sikonge,
Hii deal la Libya ni habari za wazushi na siwezi kuingilia kati zaidi kwa sababu sielewi kinachogomba. tatizo kubwa la Libya ni kutokana na watu wengi kutompenda Gadaffi basi...
Sokoine mkuu wangu ni jamaa ambaye unaweza ku hang naye na usichoke wala kujisikia mdogo...Kisha hakimbnii simu ya mtu kama walivyo viongozi wengine as a fact mara ya kwanza nimeongea naye kaniomba simu yangu jambo ambalo sijawahi kuona toka kwa viongozi wetu...
 
Mkandara,
Membe haijui Tanzania na Watanzania. Atawafaa sana ninyi mlioko nje. Vinginevyo kama unataka akabembee kule Jamaica sawa.
 
Ningependa mtoa hoja atueleze matatizo ya Membe ni nini. Unaposema ni muongo, ni vizuri ukatueleza uongo wake ni nini, na alimdanganya nani? Mbona shutuma hizi zinafanana sana na zile wanazozitoa maadui zake kisiasa?

Nikipata maelezo ya shutuma zake nitaeleza kwa undani chanzo cha hoja hii kuletwa bila ufafanuzi.
 
Mkandara naona umerudi kwa moto mkali na hivi ndivyo tunavyotaka

Nimesema kuwa Membe pamoja na ukimya wake amekuwa yuko bize na mambo ambayo kwa tafsiri ya haraka haraka ni kinyume na NATIONAL INTEREST na mbaya zaidi karibuni alifanya jambo ambalo linaweza kutafsirika kama threat to our NATIONAL SECURITY

Sasa kwa sababu huu ni uwanja wa GREAT THINKERS na WACHAMBUZI nimeona nije na style ya kuwapa hiki kitendawili. Nashangaa wale vijana wake bado hawajaja kumjibia lakini I'm sure soon watakuja


Labda ungetuambia zaidi kuhusu hiyo LIBYAN connection..we are getting somewhere at least kwa sasa...
 
Back
Top Bottom