MgonjwaUkimwi,
..kwani Mkapa alihusika vipi na udanganyifu ktk matumizi ya fedha za serikali uliofanywa na mke wa Col.Kitine?
..ninavyokumbuka Lt.Gen.Imran Kombe alifariki akiwa tayari ameshaondolewa Usalama wa Taifa na nafasi yake kuchukuliwa na Apson.
..je, unafahamu sababu zilizosababisha Kombe kuondolewa usalama? je, unaweza kusema kimaadili Lt.Gen.Kombe alikuwa mtu wa aina gani? rekodi yake kama Dir if Inteligence ilikuwaje?
Joka Kuu, heshima kwanza.
Wewe soma tu posting zangu na zielewe kama navyozitoa. JK namfahamu sana, Lowasa namjuwa nje na ndani, Membe namjua na naweza kumchambua hadi machweo, Mwikalo namjuwa kuliko anavyonijuwa mimi, RA namjua kama usiku na mchana, Mudhihir namjuwa sana na nayajuwa mengi juu yake, Mkapa naye naweza kumchambua hadi tukimbiane.
Tatizo mimi sio mwanasiasa, na hivyo sipeperushwi na upepo wa siasa. Ila nitakuambia kwamba wanasiasa makini nawafahamu, ajali za kisiasa nazifahamu, majungu kama ya Mudhihir nayafahamu. Mimi si mchangiaji mkubwa wa jukwaa la siasa, ila uongo ukitokea nitaunyoosha, majungu yakiletwa nitayapinga. Kama mada ya kisiasa siijui sichangii.
Nikirudi kwenye maswali yako, sitapenda nitoe data zaidi ya nilizotoa. Kwani kufanya hivyo ni kutowafanyia haki wahusika na ni mwanzo wa kutoka nje ya mada husika. Na ieleweke kwamba mchango wangu juu ya hili ni kukanusha madai ya Mudhihir juu ya Membe na madai kwamba Mwikalo ndie aliyefanya Membe awe waziri. Vile vile nikatika kujibu hoja yako juu ya wabunge kuwa watu wa usalama wa taifa. Na hapa nitarudia tena kwamba TANGU 2000 MEMBE SI MTU WA USALAMA.
Nitaendelea kuimba kwamba MWIKALO SIO MFADHILI WA KAMPENI ZA MEMBE. Yeye mwenyewe (Mwikalo) kama mfuasi HALISI wa dini ya uislamu anajuwa kwamba uwaziri wa MEMBE SIO MATUNDA YAKE, bali ni matunda ya urafiki wa Membe na JK ulioanza miaka ya mwisho ya 70, na kuimarika 1995 Chimwaga wakati Membe alipoikacha kambi ya Mkapa (jirani yake kimkoa) na kujiunga na kambi ya Kikwete. Yeyote anayesema kwamba Mwikalo ndio mfadhili wa Membe hamjui Mwikalo, wala hajui urafiki wa Membe na JK.
Nilipokuwa BSC times mwaka 2005 kama member wa forum nilieleza kwa undani urafiki wa JK na Membe. Wanaokumbuka, wakiwemo FMS, Mkandara, na wengine watajuwa nini nakiongea na level ya confidence niliyonayo kwa mambo nayoandika. Wanaokumbuka postings zangu wala hawakushangaa JK alipomteua Membe kuwa waziri wa mambo ya nje, na walishangaa kwanini alimteua Migiro kwanza kabla ya Membe.
Sasa ninayoyajuwa mimi sio anayoyajuwa kila mtu, ila pale ukweli unapopindishwa nitakuwa mstari wa mbele kuunyoosha. Tunajuwa kwamba Mudhihir anatumiwa na mafisadi waliojichafua tangu enzi za Nyerere. Tunajuwa kwamba enzi za JK ni enzi pekee tangu uhuru kutupa mafisadi waliokaribu na viongozi, na wanaoendeleza ufisadi wakizani wanakinga. Mudhihir anapindisha ukweli akizani kwamba kwa kufanya hivyo ataukwaa tena ubunge. Amechelewa, na anajuwa amechelewa, sasa ni mfa maji.
Tunajuwa kwamba JK kaoa Lindi, kwanini Mudhihir hakudai kwamba JK amemtilia ngumu ujezi wa kiwanda cha cement Lindi mjini? Tunajuwa kwamba JK hatasita kuinua mji wa mkoa alioolea, Mbona Mudhihir halioni hili?