Membe kuwania urais 2015...

Membe kuwania urais 2015...

Hold on,wakati mwingine tunapenda kurusha mawe bila utaratibu au bila backup.

Membe ameshachemka mara nyingi tu lakini kwenye suala la kutoa misimamo ya Serikali anajitahidi na huyu jamaa nikifuatilia naona angalao ukilinganisha na Jk alipokua foreign affairs basi utaona huyu jamaa anafanya kitu kulingana na Taaluma yake.Na hata anapowahutubia mabalozi,nadhani he needs experience zaidi!
 
labda niwape clues

MEMBE the person

MEMBE the minister for Foreign Affairs

MEMBE the aspiring presidential Candidate for 2015

MEMBE the WALTER MITTY character

ohhh kwa msiojua maana ya hilo neno hapo juu tafsiri yake ni:

(wôltr mt)
n.
An ordinary, often ineffectual person who indulges in fantastic daydreams of personal triumphs.

http://www.thefreedictionary.com/Walter+Mitty
 
sijawahi kukutana na waziri mpenda sifa na muongo kama MEMBE kwenye maneno matano chukua moja. watu wa karibu na huyu bwana mwambieni aache kudanganya watu,uongo wake nadhani ni wa kuzaliwa au kurithi.

Mbona mnamwita muongo lakini you do not substantiate allegation zenu kuwa huyu bwana ni muongo kwa kusema hivi na hivi!! G.T nae analeta uzushi wake kuwa jamaa anahatarisha usalama wa Taifa letu lakini haelezi huyu Membe anahatarisha vipi Taifa: je anauza siri za nchi?? Please come out of your shell.
 
....MEMBE the WALTER MITTY character

Are you saying Membe has a multiple personality disorder? A minister of foreign affairs playing 'pretend' president, attorney general/ registrar of parties/ national electoral commission chairman.........

I was just wondering of his stint as National Security Analyst 1977-1990 - what qualifications did he have then?
 
Sikonge said:
Hivi kuna kiongozi MUISLAAM ambaye alishawahi kushambuliwa na Game Theory?

Sikonge,

..Mustafa Mkulo na degree yake feki.
 
Wakati watu wanafikiria siasa za Kyela kule.. siasa nyingi za mwaka huu zitakuwa ni huko Lindi.. kutanoga!!
 
GT can you tell us what is wrong with Membe? Especially when you saying he is threatening national security? He is a liar, and so... ili tumtendee haki tunahitaji kujua shutuma zake ni zipi, otherwise tutakuwa kama washabiki wa kitchen party ktk kuchangia hoja yako. Please come out...
 
Kinachonishangaza ni kuwa ktk hoja yako ukajilinda mapema kwa kusema ""tegemeeni influx wale watetezi wake wa wakati wa sakata la dili lake la Vitambulisho"". Hivi bado unataka kuudanganya umma kuwa mradi wa Vitambulisho ni wa Membe? How is he involved in this project?
 
GT kuwa mkweli kwa Mungu wako, hivi ni mara ngapi uliomba kazi Wizara ya Mambo ya Nje? ni sababu gani ulikosa nafasi ulizoomba? Unataka tuamini kuwa hizi ndio hasira zako kwa Membe? Kabla sijaanza kumuelezea Membe ni nani, ni vizuri kwanza tujue chanzo cha mtoa hoja, na hoja yenyewe. JF sio mahali pa kuleta umbea wako umetoka nao huko unakokujua wewe.
 
Nadhani la kusema lipo. Ni waziri mwenye jazba isiyofaa kama kiongozi nakumbuka wakati wa mjadala wa mahakama ya kadhi akihojiwa na TBC1 hakuonesha busara katika kujibu. Vinginevyooo.... ni mwanachama hai wa CCM anayetetea lolote litokalo ndani ya chama hata kama halina tija kwa wananchi1
 
Pamoja na baadhi ya matatizo ya Membe, mimi nafikiri ni bora kuliko wengi wa wanasiasa wetu.

Binafsi ninapenda watu ambao wanaweka misimamo yao wazi ili mtu uamue kama anafaa au hafai. Vinginevyo unakumbana na wapenda sifa ambao huangalia upepo na kwenda huko huko.

Kama watu wana ushahidi juu ya matendo mabaya ya Membe basi telemsheni, vinginevyo tutaishia kumvuta chini kila anayejitokeza na matokeo yake sidhani kama yatakuwa mazuri kwa mtu yeyote.

Tukiendelea kuhukumu watu kwa hisia, sidhani kama tutakuwa tunaitendea jema nchi yetu.
 
Shutuma ulizompelekea Membe hazijaanza leo. Ni shutuma ambazo hutolewa na maadui zake kisiasa, ambao nitawataja kwa majina na nafasi zao wanazoshika ktk jamii, nitafanya hivyo tu pale utakaponiambia, Membe anatishia vipi usalama wa nchi, na ni muongo vipi, alimdanganya nani, na lini?. Sijawahi kumsikia Membe akisema kwa mtu yeyote kuwa anautaka Urais mwaka 2010, lakini napenda kukufahamisha kuwa hakuna dhambi yeyote kwake kugombea nafasi hiyo, kama ilivyo kwa Mtanzania yeyote. Tatizo hapa ni kuwa kuna watu wamejipanga kuutaka Urais, na wanaona kuwa mwanaume huyu ni kikwazo kwao, wanaanza kutafuta kila namna ya kumchafua.
 
Genekai, hivi jazba za Membe zinatishia vipi usalama wa nchi? Hivi jazba hizo ndio uongo wa Membe? Namtaka GT atueleze kinagaubaga, Membe anahatarisha vipi usalama wa nchi? Nina wasi wasi GT alipitia ktk kijiwe fulani akakuta wanamsema hivyo Membe nae akawaahidi kuwa ataenda kumlipua, na hilo ndio bomu lenyewe. Ni vizuri GT ukajitokeza na kutujibu maswali yetu, otherwise, tutakuhukumu kwa Uongo, Uzandindiki, Fitna, Husda, Wivu, Chuki na kila aina ya ushenzi wa namna hiyo unaouleta hapa JF. Hapa sio kitchen party ndugu yangu.
 
kama huna idea,AU HAUPO KWENYE SYSTEM hii thread ni ngumu kuijadili...!i am watching
 
Nimeamua kuchangia kwa umakini ktk hoja hii kwa sababu nilishtuka sana pale GT alipoleta hoja halafu mwishoni akasema kuwa "tegemeeni influx wale watetezi wake wa wakati wa sakata la dili lake la Vitambulisho". Halafu hakuleata ushahidi wowote wa shutuma zake kwa Membe. Huyu ni mtu hatari sana na inafaa kumwangalia kwa umakini sana, kwani yeye ndio wale wahenga walisema, "Hutwanga mbuyu na kuwaachia watu waule".
 
GT, ili kulinda heshima yako, jitokeze utueleze Membe anahatarisha vipi usalama wa nchi, na amemuongopea nani, lini na kwa jambo gani? Linda heshima yako kabla sijakuumbua. Tunahitaji kukomesha tabia ya mtu kuzuka na ujinga wake huko halafu anatuletea hapa JF, na wenzangu bila kufanya utafiti wa kufaa munachangia kwa jazba. Mwambieni GT atujibu maswali hayo kama kweli yeye ni mkweli.
 
Back
Top Bottom