
Nategemea DC PAUL MAKONDA atamshtaki Bishop GWAJIMA mahakamani kwa kosa la kumdharirisha.

Nategemea JESHI LA POLISI litamkamata na kumhoji Bishop GWAJIMA kwa kumchafua MTUKUFU DC PAUL MAKONDA.

Nategemea Waziri wa Elimu Prof JOYCE NDALICHAKO atajitokeza hadharani kutoa ufafanuzi,Kuthibitisha au kukanusha hizi tuhuma zinazoendelea ili kulinda hadhi ya elimu ya Tanzania ambayo Inadharirika kwa hizi tuhuma za kufoji vyeti..

Nategemea MTUKUFU DC PAUL MAKONDA atajitokeza hadharani,kulikana jina la DAUD BASHITE,atajitokeza na vyeti vyake vya kuzaliwa,cheti cha darasa la saba,cheti cha form four,Six na cha chuo ili kutoa ukweli wa uhalali wa jina lake

Nategemea Mamlaka iliyomteua MTUKUFU DC PAUL MAKONDA Kwa maana taasisi ya Rais itatoa tamko,Either Kuiamrisha wizara husika ifuatilie uhakiki wa vyeti vya mkuu wa mkoa,Au itatoa taarifa ya kuthibitisha juu ya uhalali wa vyeti vya Paul Makonda,Na kujiridhisha ka amejipatia ajira serikalini kwa taarifa za uongo (Obtaining Employment with fake documents) ama Itengue uteuzi wake ili kulinda Hadhi ya utawala bora na Maadili ya Umma.

Nategemea Immigration kuanza uchunguzi Ili kujua kwamba MTUKUFU DC anahusika na wizi wa taarifa za mtu mwingine(Identity theft),Kujipatia hati ya kusafiria kwa taarifa za uongo (Obtaining passport using fake Information),Kusafiri nje ya nchi kwa kutumia taarifa za kughushi/Za mtu mwingine (Travelling with false documents)
#NB
Haya yote ni kwa manufaa ya MTUKUFU DC PAUL MAKONDA kwanza itasaidia kuweka ukweli bayana hii italinda hadhi yake na utu wake,Lakini italinda hadhi ya utawala bora na Maadili ya umma.
Lakini italinda na kusafisha elimu ya Tz ambayo imeshaanza kuingia dosari.
Pia italinda hadhi ya uwajibikaji na usawa kwa vyombo vyenye mamlaka ya kuthibitisha haya mambo kwani Ganzi waliyopigwa sasa plus ukimya unaleta shaka na walakini katika uwajibikaji na utendaji wao.
NATAMANI nisikie sauti ya MTUKUFU DC PAUL MAKONDA ikisema "DAUD BASHITE nikukute Central kesho saa nne"
NGOJA NINYWE KIROBA NILALE MAANA HAYA MAPAMBIO YA DAUD BASHITE yamekata usingizi wanguuu...