Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Mange kimambi ndiye aliyeibua hoja ya RC Paul Makonda kuwa alipofeli kidato cha nne, alitumia cheti cha mtu mwingine kwenda Chuo. Haijajulikana vyanzo vya habari za Mwanadada huyu anayeishi ughaibuni, lakini anaonekana kuwa "active" sana kupata habari za moto moto kutoka Bongo na kuzisambaza.

Askofu Gwajima kwakumwamini sana Mange Kimambi, alizichukua habari zile na kuzisanifu vizuri na kuongezea mbwembwe na kuzihubiri madhabahuni pa Bwana mbele ya wanakondoo wa Mungu. Huku akitegemea kupata "Updates" zingine kutoka kwa Mange, Juu ya vyeti halisi vya Mh. RC kijana zaidi nchini Tanzania aliyepewa dhamana na Mh.Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. JP Magufuli kuliongoza Jiji lenye "population" kubwa zaidi ya watu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati, Jiji la Dar es Salaam Mh.Paul C. Makonda...(mwanzilishi wa vita na mpambanaji dhididi ya madawa ya kulevya) na akahaidi kuviweka hadhalani baada ya siku tatu kwakuwa anavyo ofisini kwake.
Wataaram wa kufasiri mambo wanasema kitendo cha Askofu kumtaka RC amwombe msamaha ndani ya siku tatu lasivyo ataweka vyeti wazi, ndiyo ilikuwa inatambulisha kuwa hana, na ama alikuwa anategemea mtu ampe.

Mange Kimambi naye kule alikotegemea kupata vyeti ili aviweke mtandaoni na kumpa Askofu Gwajima NETWORK imekata.
Mange amenukuliwa ameandika hivii katika acc. yake ya Instagram "I wish I could be NECTA ningesha maliza mchezo"
Kwa kauli hii, Mange hana vyeti na Gwajima hana vyeti..wanategemea huruma ya NECTA..
GWAJIMA AMEACHWA KWENYE MATAA NA MANGE KIMAMBI.
UBARIKIWE MTUMISHI.
KWA UBONGO WAKO UNAOTEGEMEA MTAA WA LUMUMBA NDIO UMEKUSHAURI USEME HAYA??!!!
Bora viloba vimezuiwa tungesema umebugia vi3 lkn kumbe umevulugwa na LUMUMBA.. kwa akili yako unavoona MCH. GWAJIMA anamtegemea KIMAMBI?
Hebu jiongeze uondoe ubongo hapo lumumba ili upate nafuu bado binti mdogo sana wewe.. kuharibikiwa ktk umri huo ni mbaya sana.
 
Kwenye akaunti yake ya facebook, kada wa CCM ndugu Yohana Mabena ameandika hivi

"Mh Mkuu Wa Mkoa Wa Dar-es-salaam Mimi binafsi na kupongeza sana kwa kazi zako unazozifanya kuhakikisha Jiji la Dar-es-salaam linakuwa Jiji la biashara na linakuwa Jiji la ushindani .

Pili naomba nikupe ushauri wangu kwa kutoa mfano Wa mtu mmoja tu au wawili Mh Mwigulu Nchemba aliwahi tuhumiwa kuwa vyeti vyake vinatofautiana na ikazungumzwa sana kwenye mitandao na wanaccm tulipata utata sana kumtetea humu lakini kwa muda mchache alitoa vyeti vyake hadharani kila mtu aliviona na akaeleza sababu ya vyeti vyake kutofautiana jambo hilo likaisha.

Tatu kulikuwa na tuhuma dhidi ya Mh Zitto Kabwe kuwa hana shahada ya kwanza baadae akatoa cheti chake hadharani mjadala ukaisha.

Nikija kwako kuhusu tuhuma ya vyeti vyako ambayo inatupa shida sana sisi wengine wanaccm kukutetea humu kwasababu wewe ndiye pekee unayeweza kutuondolea utata huu .

Ushauri wangu Fanya kama walivyofanya viongozi wengine hao kwa kuweka vyeti vyao hadharani iliutuondolee utata huu kwani kukaa kimya au kuanza kubishana na Watu haisaidi hata kidogo njia pekee ya kuondoa utata huo wewe in kutuwekea vyeti hadharani na kama kuna ukweli kuhusu tuhuma hizo tupe sababu watanzania kuhusu hilo .

Huo ni ushauri wangu kwako Mkuu Wa Mkoa Wa Dar-es-salaam kwani ndiyo njia pekee ya kuondoa utata huu unaoendelea kila siku .

Kwani ni dhambi kubwa na ni kosa kubwa kwa kiongozi Wa umma kutuhumiwa na kushindwa kutoa Maelezo juu ya tuhuma zinazomkabili".

[HASHTAG]#Mytake[/HASHTAG]:

Makonda hana namna nyingine zaidi ya kutoka na kusafisha upepo huu. Hata wanaomsapoti humu unafikia wakati wanashindwa na kuishiwa pumzi. Kutoa vyeti tuu kwani bei gani? Kulia pekee hakuwezi kumsafisha. Hata kusingizia kuwa tuhuma hizi zinatokana na vita yake dhidi ya madawa ya kulevya hakuwezi kumwacha salama. It's high time for him to come out bravely and clean the windscreen before it becomes worse
 
Salam..

Binafsi, nimeamua kuyaweka maoni yangu katika mtindo huu "WATETEZI WA DAUDI BASHITE NA ULEMAVU WA FIKRA". Kwasababu robo tatu (3/4) ya wanaccm wamekuwa watetezi wakubwa kwenye ishu ya vyeti feki vya ndugu yetu DAUDI BASHITE.

Hakuna mtanzania mwenye akili anaweza kupinga vita dhidi ya dawa za kulevya, lakini vita hiyo hakuhalalishi mtu kughushi vyeti.

Ndugu zangu wanaCCM, Athari za tabia hii ni kutengeneza wataalamu bandia ambao baadaye hawatathaminika katika soko la ajira la kimataifa na mwishowe kulitia doa taifa letu. So ni jambo njema sana kwa mtu kuwa na vyeti halali,,, Mwanaccm hivi unajisikiaje katika sehemu unayofanyia kazi usikie kuna mtu analipwa msharaha mkubwa alafu na nyeti vya kughushi?

Haiingii akilini kwanini wanaCCM wanang'ang'ania watu wenye vyeti feki(mfano DAUDI) wawepo serikalini kwakuwatetea kwa kivuli cha madawa ya kulevya.

Kama kweli DAUDI ana vyeti halali ajitokeze kujibu tuhumu hizi. Mfano kaka NCHEMBA japokuwa maelezo yake yalikuwa yanaukakasi sana juu ya elimu yake.

Hapa wanaCCM tujenge tabia ya UTHUBUTU kwa maslahi ya taifa. Na kutoa kauli kama "CCM BILA VYETI FEKI INAWEZEKANA" kama ilivyo kauli ya HAPA KAZI TU.

Ndugu zangu wanaccm kuhalalisha vyeti feki ni kuzalilisha chuo kikuu cha dar es salaam, kwasababu ndugu DAUDI alisoma hapo so tusije tukaonekana kuwa wote ni walewale yani VYETI FEKI.

Kimsingi naomba kutoka sasa tubadilike, matangazo ndio kama haya.

View attachment 477235

Mr mkiki.
 
Askofu Gwajima aliahidi jana atamleta mtu kutoka koromije kuja kuthibitisha madai yake..na aliahidi kuweka hadharani vyeti halisi vya makonda..je alifanya hivyo?
 
mtoto wa kiume kulialia mbele ya kadamnasi ni uchoko huo,mwanume unapopatwa na matatizo macho huwa mekundu kwa hasira,alafu mwanaume analia kama simba ndani yamoyo tena peke yake usiku wa manane
 
6. Mwaka 1997 akajiunga na kidato cha kwanza shule ya sekondari ya Pamba.

7. Mwaka 2000 akahitimu kidato cha 4 na kupata daraja sifuri (division zero).
kwaiyo kutoka form 1 mpaka form 4 kipindi icho ilikua inachukua miaka mitatu badala ya minne?
 
Ccm imeathirika na zidumu fikra za Mwenyekiti
Sasa kama Mwenyekiti katia pamba sikioni anajidai hajui kinachoendelea mitandaoni na magazetini

Juzi anadai yeye asomagi mambo ya mitandaoni huku nyuma alishasema anatamani malaika washukie mitandao ya kijamii

Nikikumbuka Ile hotuba yake bandarini juu ya vyeti feki na hii pamba sijui kijiti alichotia masikioni juu ya ili la Daud nashindwa kumuelewa kabisa
 
Kutetea jambo utatumia nguvu kubwa sana.. Lakini kuweka vyeti mezani ni jambo jepesi saba
 
Mpaka Leo mitandao mingi sana imejadili suala la elimu ya Mh Paul Makonda yangu atangaze hadharani operation maalumu kuhusu janga la madawa ya kulevya ktk mkoa wake.

Lakini cha ajabu wote tumekuwa tukidakia tu hoja kuhusu Mh Makonda mara anapoongea Mch Gwajima au watanzania nje ya nchi.

Cha ajabu mpaka muda huu hakuna aliyetuwekea ushahidi wa shutuma hizi zaidi ya kumshinikiza tu Mh Makonda aweke vyeti vyake hadharani au ajiuzuru au Rais amvue madaraka ya ukuu wa mkoa.

Nadhani si rahisi sana maafisa wa Ikulu toka Dr Kikwete mpaka Dr Magufuli kuwa hawako sahihi ktk kufanya vetting ya viongozi.

Naamini Maafisa wa Ikulu wako makini na teuzi za viongozi mbalimbali kwa kuangalia historia zao za nyuma kielimu, kimaisha na kimahusiano na jamii.
 
Tatizo hakuna ushahidi juu ya hayo mnayotulazimisha tuyaamini,kama haujui siasa ni mchezo mchafu sana,ili tuamini hayo madai yenu tuleteeni huyo aliyemuuzia vyeti kuthibitisha vinginevyo ni hila tu na chuki zisizo za msingi.
 
Back
Top Bottom