Baada kuona mjadala tena mrefu humu ndani leo na mimi naona nitoe uzi wangu ili tupate kujadili wote na ikiwezekana kila mmoja awe amepata jibu sahihi.
Hii ni kutokana na swala linaloendelea ambapo mimi siwezei kukubaliana nalo wala kulikataa ila naweza kulikubali endapo tu itakuja evidence itakayoonyesha hii ni kweli, si jambo lingine nalozungumzia hapa ni swala la kusema RC wa Dar amechukua jina ambalo si la kwake, hebu tujiulize maswali yafuatayo ili tupate kujiridhisha na kuweza kumaliza utata wa swala hili.
1: Mmiliki halali wa hicho cheti yuko wapi na anajihusisha na nini?, na je ni kwanini asijitokeze au asichukuliwe ili kumaliza mzizi wa fitna badala ya kumsubiri huyo mtu anayedhaniwa amechukua jina la mtu na kulitumia ndo afanye hivyo?.
2: Endapo akijitokeza huyo mhusika (mmiliki halali wa hicho cheti) anapaswa kuulizwa maswali kadhaa
A) ni kwann alikubali jina lake litumiwe na mtu mwingine na kupelekea huyo mtu kujiendeleza kielimu na si yeye binafsi
B) kwann alisubiri watu wajitokeze na si yeye binafsi asiende kwenye vyombo vya sheria ili kuchukua hatua juu ya swala hilo?.
C) atatuthibitishiaje umma tupate kuamini kuwa yeye ndo mmiliki halali wa hilo jina?
3: kama kuna mtu mwenye ushahidi mbali na mhusika kamili ambaye bado hajatoka mbele ya kadamnasi kuthibitisha kuwa bwana Daudi Bashite alibadilisha jina na baadae akaitwa Paul Makonda ni kwanini asijitokeze na kuweka mambo hadharani ili watu wajue ukweli badala ya kupiga kelele kwenye mitandao ya kijamii.
4) familia ya mtu ambaye cheti chake kilichukuliwa either kwa kununuliwa au kwa kukitoa kawaida iko wapi? na kwanini hawataki kujitokeza hadharani ili kuwafungua watanzania wengi wanaoamini au wasiamini hii sinema kama ni kweli au la?
5) Walimu, wanafunzi wenzake na Daudi Bashite pamoja na Paul Makonda wako wapi? Na kwanini wasijitokeze na kutoa ushahidi kamili licha ya huu unaosadikika?
6) na je ni kwanini wasifatwe ndugu wa karibu wa familia ya paul makonda na kuhojiwa juu ya hili swala ili kupata jibu sahihi mbali na kuendelea kupiga kelele kwenye mitandao ya kijamii?
NB: kuna kipindi kulikuwa na maswala kama haya ya bwana Daud Bashite na ikapelekea kuandikwa kwa kitabu cha "MAFISADI WA ELIMU" kuna baadhi ya viongozi ambao mpaka leo wapo madarakani, na watu wamekosa ushahidi wa kusema kwamba wamechukua vyeti vya watu na kujiendeleza kielimu au la.
Mtazamo wangu kama ni kweli huyu jamaa alichukua vyeti ni heli yakatumiwa hayo maswali kama njia mojawapo ya kusema ukweli kuliko kusema, kuandika sana haya mambo kila siku kwenye mitandao ya kijamii na hata kwenye baadhi ya vyombo vya habari bila ya kuwa na ushahidi yakinifu na kuwafanya watanzania kuacha kufanya mambo mengine na kujadili hili jambo kila siku.
[HASHTAG]#huu[/HASHTAG] ni mtazamo wangu tu ambao utatusaidia kumaliza huu utata wa bwana Daud Bashite/Paul Makonda.