beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Mbunge wa Mbogwe, Nicodemus Maganga amemtaka Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi kutofuata mambo ya kwenye makaratasi, na kufuatana naye ili akamuoneshe visima 26 ambavyo amesema vipo.
Katika swali lake, Mbunge huyo alihoji Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo hilo kwa ajili ya matumizi ya wananchi.
Akimjibu, Naibu Waziri alisema hali ya upatikanaji maji ni wastani wa 55% na huduma inapatikana kupitia miradi minne ya skimu, visima virefu 26, visima vifupi 460 na matenki 50 ya kuvuna maji ya mvua nk.
Hata hivyo, Mbunge huyo hakuridhishwa na majibu yake akisema, "Tuongozane naye akanionyeshe pale vilipo. Mimi ni Mbunge wa Mbogwe na ninaishi Mbogwe, kuna tabu sana katika sekta ya maji".
Katika swali lake, Mbunge huyo alihoji Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo hilo kwa ajili ya matumizi ya wananchi.
Akimjibu, Naibu Waziri alisema hali ya upatikanaji maji ni wastani wa 55% na huduma inapatikana kupitia miradi minne ya skimu, visima virefu 26, visima vifupi 460 na matenki 50 ya kuvuna maji ya mvua nk.
Hata hivyo, Mbunge huyo hakuridhishwa na majibu yake akisema, "Tuongozane naye akanionyeshe pale vilipo. Mimi ni Mbunge wa Mbogwe na ninaishi Mbogwe, kuna tabu sana katika sekta ya maji".