Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 945
MBUNGE JULIANA SHONZA AFYA MKUTANO WA HADHARA KATA YA IFWEKENYA WILAYA YA SONGWE KUELEZEA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe, Mhe. Juliana Daniel Shonza ameendelea na ziara katika Kata mbalimbali za Mkoa wa Songwe huku alitembelea Wajasiriamali wa vikundi mbalimbali alivyovianzisha na kuvipa mitaji ya Shilingi 300,000 kila kikundi.
Mhe. Juliana Daniel Shonza amefanya mikutano ya hadhara Kata kwa Kata na kuelezea utekelezaji wa Ilani ya CCM 2020-2025 na utendaji wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan
Vikundi vya wanawake wajasiriamali katika Kata ya Ifwekenya vinajishughulisha na Ufugaji wa Kuku, Biashara za Vitenge & Kilimo cha Ufuta na Karanga ambavyo vimewezeshwa na Mbunge Juliana Shonza