Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,580
Naamka asubuhi saa moja majira ya huku (takribani saa nane za mchana Tanzania). Kama ilivyo ada kila nikiwa nje ya TZ nikiamka cha kwanza huwa ni kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ya nyumbani ili kujua kinachojiri. Sikuamini nilichokiona kwenye ukurasa wa facebook na kwenye mtandao maarufu wa Jamii forums, eti ya kuwa Mh. Jeremiah Solomon Sumari, Mbunge wangu wa Arumeru Mashariki amefariki dunia.
Ilinilazimu kumpigia rafiki yangu wa karibu Mh. Godbless Lema (mb) ili anithibitishie habari hizi kwa kuwa na yeye ni mbunge na nafahamu yupo Darkwa ajili ya vikao vya kamati za bunge. Ndipo alipoithibitishia kuwa Spika wa Bunge amewatangazia wabunge kuondeka kwa mwenzao. Kwa kweli ni majonzi makubwa, pamoja na kwamba tulitofautiana kiitikadi lakini still tulikuwa marafiki na mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa nilimpa hongera though siku-sign matokeo. Mara ya mwisho tulikutana Dodoma hotel, akiwa amepumzika akijisomea kitabu. Kwakweli afya yake haikuwa nzuri sana na aliniambia "Nassari afya yangu ikitengemaa nitakupigia simu, kuna mambo ya kuzungumza" hayo ndio maneno ya mwisho niliyoyasikia kutoka kwake.
Hon. Sumari, umefanya mengi kiasi cha uwezo wako kwa wana-Meru na Taifa hili na kwa ujumla wake. Yale ambayo hukuweza kwa sababu moja ama nyingine, atakayekupokea kijiti ataendeleza mbio. Nimelazimika kubadilisha tiketi yangu, nilipaswa kurudi nyumbani TZ wiki mbili zijazo lakini imenipasa kurudi sasa kukusindikiza. Hii ni kwa kuuthamini mchango wako mkubwa kwa Jimbo langu la Armeru Mashariki na Taifa langu la Tanzania.
Natoa pole nyingi kwa Wanafamilia, na Wananchi wote wa Meru. Mungu awape subira katika kipindi hiki kigumu. Upumzike kwa Amani Mh. Sumari.
Joshua S. Nassari
Ilinilazimu kumpigia rafiki yangu wa karibu Mh. Godbless Lema (mb) ili anithibitishie habari hizi kwa kuwa na yeye ni mbunge na nafahamu yupo Darkwa ajili ya vikao vya kamati za bunge. Ndipo alipoithibitishia kuwa Spika wa Bunge amewatangazia wabunge kuondeka kwa mwenzao. Kwa kweli ni majonzi makubwa, pamoja na kwamba tulitofautiana kiitikadi lakini still tulikuwa marafiki na mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa nilimpa hongera though siku-sign matokeo. Mara ya mwisho tulikutana Dodoma hotel, akiwa amepumzika akijisomea kitabu. Kwakweli afya yake haikuwa nzuri sana na aliniambia "Nassari afya yangu ikitengemaa nitakupigia simu, kuna mambo ya kuzungumza" hayo ndio maneno ya mwisho niliyoyasikia kutoka kwake.
Hon. Sumari, umefanya mengi kiasi cha uwezo wako kwa wana-Meru na Taifa hili na kwa ujumla wake. Yale ambayo hukuweza kwa sababu moja ama nyingine, atakayekupokea kijiti ataendeleza mbio. Nimelazimika kubadilisha tiketi yangu, nilipaswa kurudi nyumbani TZ wiki mbili zijazo lakini imenipasa kurudi sasa kukusindikiza. Hii ni kwa kuuthamini mchango wako mkubwa kwa Jimbo langu la Armeru Mashariki na Taifa langu la Tanzania.
Natoa pole nyingi kwa Wanafamilia, na Wananchi wote wa Meru. Mungu awape subira katika kipindi hiki kigumu. Upumzike kwa Amani Mh. Sumari.
Joshua S. Nassari