Mzee ES: Hapo sijakupata, labda uelewa wangu mdogo!
Mwanagenzi:Jibu ni hapana. Hakuna uhusiano. Muhonga aligombea kama wanachama wengi na akapitishwa na vikao na wala hakupitishwa na Zitto.
Kuhusu tukiwa na wabunge 50 au 75 itakuwaje? Labda ni-qualify statement yangu. Kuna kipengele cha uwakilishi wa wabunge katika katiba (nafikiri ni section 7.7.14) ambapo wabunge watano na wawakilishi watatu kutoka baraza la wawakilishi ndio wanaingia. Kwa sasa wabunge wote ni wanachama kwa sifa tofauti. Kwa mfano, Zitto yeye ni mjumbe kwa kuchaguliwa, ila Mhonga ameingia kuwakilisha bunge. Ahsante kwa angalizo maana limenipa nafasi ya kuweka sawa hili.
Ieleweke tu ndugu zangu hapa kuwa mimi sipo hapa kujitetea katika mapungufu yaliopo katika CHADEMA. Najaribu kuweka mambo sawa kwa kadri ninavyojua. Ninaomba sana watu wasichukue mawazo yangu kama ndio msimamo wa CHADEMA. Haya ni mawazo yangu kwa kadri niijuavyo CHADEMA. Mimi wala sina cheo katika CHADEMA kwa hivyo siwezi kutoa msimamo wa chama hiki hata kidogo. Kama kuna sehemu nimepitiliza nikaonekana kutetea bila hoja za msingi hiyo itakuwa inatokana na mapenzi na imani yangu kwa hiki chama na wala sio makusudi, na ninatanguliza kuomba msamaha kwa hilo.
Kama kuna sehemu majibu yangu yameonekana nusu nusu ni pale nitapokuwa sina facts, hapo inabidi nipapite nikitarajia mwenzangu Mnyika atateremka siku moja kuweka vitu sawa maana yeye yuko jikoni na ni kiongozi. Hoja kwamba mimi na Mnyika tukae pamoja tujadiliane haina nguvu kwa sababu hii forum tunatoa maoni binafsi na wala sio taasisi. Wala Mnyika mwenyewe hanijui mimi ni nani, ila nafikiri anajua kwamba mwanasiasa ni moja ya wanachama wa CHADEMA waliopo humu katika forum.
Naomba pia nieleweka kuwa mimi sijasema kwamba katika CHADEMA kuna purity. Ninachopinga ni hoja ambazo hazina mshiko na ambazo zimekaa ki-propaganda zaidi kuliko ukweli. Nazo ni hizi za u-family business, n.k. Nimejaribu kufafanua hili tena kwa vielelezo na takwimu hadi mzee wa utafiti (tafiti then jadili) akiingia mitini. Nimekuonesha kabisa kuwa facts hazifanani hata kidogo na ukubwa wa tuhuma zinazoelekezwa kwa CHADEMA kuhusu ukanda, ukabila na ufamilia. Sasa zaidi ya hizo facts mimi nifanye nini tena.
Hakuna kitu kigumu kukitoa akilini mwa mtu kama 'prejudices' (sina neno zuri la kiswahili). Vyama vya upinzani vilianza kwa kupandikiziwa prejudices akilini na mioni mwa watu. Prejudices zilianza na kuonesha kuwa hivi ni vyama vya fujo (vyama vyote vya upinzani), kisha ikaja na udini (CUF), then ukabila (NCCR) na sasa ukabila, ukanda na ufamilia (CHADEMA). Mimi nasema hizi zote ni conspiracy theories. Najua kwa mazingira ya indocrination iliyofanyika Tanzania, kuingia upinzani inaitaji moyo kama ilivyo kuokoka. Sisi tuliokoka (kukubali upinzani) tunajukumu la kuhubiri ukweli tu bila kupotosha. Tutakapojikwaa na kutenda dhambi, tutatubu na kurekebisha ili twende mbele katika kueneza hii injili ya upinzani. Basi ndugu zangu tusiwakatishe tamaa wale waliokwisha kujitoa kwa kuibuka na conspiracy theories.
Naomba watu sasa tugeukia kwenye sera za vyama katika mambo mbalimbali then tujadili hizi sera kama zinaweza kututoa katika matatizo yaliyosababishwa na utawala wa CCM.