Mleta mada hujawa objective. Ningekuona una maana sana kama ungejaribu kuleta bandiko ukifocus kwenye reality. Unaposema Lema amemkosea naibu katibu mkuu bila kusema naibu katibu mkuu amewakosea wanachama wengine akiwamo Lema unaondoa kabisa maana nzuri uliyokusudia kwenye andishi lako hili.
Binafsi tangu mwanzo sijawahi na sitawahi kuja kuunga mkono malumbano ya kipuuzi ya namna hii. Kinachoumia ni chama. Chama hiki kuna watu wamekifia, kuna watu wamekaa rumande/gerezani kwa chama hiki. Kuna watu wametoa fedha zao halali kwa ajili ya chama hiki. Kujivua nguo hadharani kwa style ile ni kudemoralize nguvu kubwa ya sisi tilio baki. Ni ku water down nguvu ya damu iliyomwagika kwa kukipigania chama.
Mshindi katika vita hii atakuwa mi CCM. Chama ambacho wengine hatutaki hata kukisikia japo kwa sekunde hata moja.
Kwa ufupi Zitto na Lema wana 'dhambi' zinazofanana.
Nimefarijika baada ya kuambiwa Uongozi wa juu umeingilia kati. Nadhani hata
Yericko Nyerere atakuwa ametaarifiwa aache mpango wake alionao.