Mbowe na Dr Slaa, natoa saa 24!

Mbowe na Dr Slaa, natoa saa 24!

Status
Not open for further replies.
Tunahitaji kuona LEMA NA WENZIE WAKIFUNDWA SIO KUSEMA UONGOZI UMEINGILIA KATI.

LEMA NDIO ATAIZAMISHA CHADEMA.
 
Hawa waheshimiwa Mbowe na Dr.Slaa mbali ya kuwa viongozi wakuu kwenye chama chao bali pia ni misingi na kanuni ya chama.

Kwa maana hiyo kanuni zingine na misingi ya CDM ndani ya chama azina ulazima, si wameshasema wakifanya uchaguzi ndani ya chama CDM kitazoofika. Ndio maana matusi kwa wengine kwao sawa kwakuwa they know how to handle wapiga kura na chama chao na ni wao ndio wenye vision ya ukombozi pekee, to think kuna watu wamelewa na porojo zao.

Chama chenye misingi imara utakiona siku zetu kanuni ndio mwongozo wake, hata CCM despite matatizo yake mwisho wa siku ni kanuni za chama ndio utoka kidedea. Zitto amekuwa akitukanwa na watu ambao wadogo kwake kichama na wala hawana impact ya wapiga kura na hawapo kwenye makeke makeke ya kuipa sura ya CDM kama chama mbadala na wala hawakanywi, sasa kweli si ka-saccos binafsi tu hii chadema, wengine tunaomba waache tu kuchukua michango ya maskini kwa maslahi yao.

Chama gani badala ya kupoteza muda kuangaika na kutunga au kuuza sera na kukosoa sera kila kukicha chenyewe kinaongelea personalities, majungu na vikao almost every week.
 
In short nimempigia simu Mnyika na kasema atahakikisha anacontrol situation, Zitto hapokei simu. Dr Slaa na Mbowe sijazoeana nao.

usimusumbue kamanda kwa hoja zako za kimagamba gamba hapa, kwanza kuanzia leo zitto simtambui kama kimgozi wa chama changu, bali kama muuza sura,mtafuta ujiko, mropokaji na asiyejielewa. Huu upuuzi pelekeni mwandiga. Kama na wewe uko upande wa zitto na masalia kuanzia kesho wambieni jamb zenu wa lumumba tumewashitukia.
 
Mzito usimpake mafuta kwa mgongo wa chupa. Hanyooshi chama ila anachochea malumbano... Ofisi za chama hazijui?

Mkuu nimetumia nafasi yangu, kama hii issue ingekuwa haijawekwa public ningeenda ufipa, naiweka huku ili waelewe extent ya hasira za wanachama.
 
Ninachotaka kuona ni maamuzi yasiyo na double standard. Yaani hiki chama kimekuwa cha ajabu sana yani kwa mfano wapo vijana kama Yericko Nyerere anatoa matamko utafikiri chadema ni chama cha shangazi yake (naongea kama wanachama wanavyosema huku mitaani) na haoni madhara ya anayoyaandika humu.
Wewe huoni madhara ya mambo unayoyaandika humu?
 
Tunahitaji kuona LEMA NA WENZIE WAKIFUNDWA SIO KUSEMA UONGOZI UMEINGILIA KATI.

LEMA NDIO ATAIZAMISHA CHADEMA.

Hivi hii ya Lema kuliwa kiboga na baadhi ya vijana wake wa bavicha kutokana na kuwadhulumu ni kweli?maana picha mnato zimezagaa na nasikia video itaepuliwa soon
 
Hiki chama sio cha zitto,mbowe.lema au slaa peke yao. Wanachama tumelalamika huu upuuzi wa kulumbana lakin viongozi hawasikii. Tuendelee tu kulalamika kila siku? Hapana,tuchukue hatua. Tuwekeeni hapa namba za simu za viongoz wote tuwaambie kilio chet
 
We si ndio ulikua unatetea division 5 wewe?! Hilo tu linatosha kujua uwezo wako na kisha kupuuza bandiko lako!!

Eti unatoa masaa 24 la sivyo itatoa tamko na wanachama wa kanda yako?!!? Una kanda wewe?! Hizi ndizo akili kama za Le mutuz hizi! BS!
 
Binafsi nashangazwa sana na chama ambacho nilihisi kipo kwa maslahi yetu (Tz). Lakini sasa kimekua kwa maslahi ya Lema na Mbowe...........kweli baada ya masaa 24 makamanda wa kanda yangu pia tutatoa tamko. Nonsense.....stupid
 
Mkuu nimetumia nafasi yangu, kama hii issue ingekuwa haijawekwa public ningeenda ufipa, naiweka huku ili waelewe extent ya hasira za wanachama.
Sikubaliani na njia uliyotumia na vitisho ulivyotoa.
 
hahaha, kamati kuu ya CCM imetoa masaa 24 kwa Mh. Mbowe na Dr,Slaa, loh, hii kali ya mwaka.

Mkuu mbona unataka nipaliwe hii Kinana baridi ninayoshushia nyama choma yangu? Hapa lazima tamko la Mkuu wa Itikadi na uenezi litatolewa tuu. zumbemkuu, ulishaona wapi mdumange unapigwa Mlalo lakini wanaokatika wako Mazinde? Ndiyo tuliyoyaona humu. Wanachadema wanabishana kwa hoja zao juu ya misimamo yao lakini ukihesabu thread za ushauri na malalamiko kuwa jambo hilo sio jema au kutoa utetezi, 80% ni wale Buku 7 & co
 
Last edited by a moderator:
Hiyo niliyo bold ni kauli ya ZITTO!... Mimi sikulaumu wewe kukosoa ndiyo maana na mimi nakukosoa.. Ila nakupinga kwas kuwa MNAFIKI.. UPINGACHO NDICHO UTENDACHO!

Acha kukariri. Zitto hana haki miliki ya misamiati ya kiswahili mkuu.
 
Najiuliza tu, hivi hiki chama chetu si kina mwenyekiti, na katibu? Haiingii akilini Zitto naibu katibu anashambuliwa na Lema na baadhi ya wanaoitwa makada wa chadema then mwenyekiti na katibu hawasemi lolote. Hivi angekuwa amesemwa John Mnyika, Josephine Mushumbusi ama Slaa si matamko yangetolewa? Mungekaa Kimya?

Binafsi nina matatizo na mwenendo wa Zitto, lakini katika hali ya kawaida uongozi wa chadema mmechemsha, badala ya kujibu hoja mnaleta risiti zinazomhusu Zitto sasa hizo risiti tuzifanyeje?

Ninachotaka kuona ni maamuzi yasiyo na double standard. Yaani hiki chama kimekuwa cha ajabu sana yani kwa mfano wapo vijana kama Yericko Nyerere anatoa matamko utafikiri chadema ni chama cha shangazi yake (naongea kama wanachama wanavyosema huku mitaani) na haoni madhara ya anayoyaandika humu.

Natoa saa 24 Mbowe na Dr Slaa najua mtasoma hii post, mchukue hatua na kuhakikisha Zitto hashambuliwi katika taratibu zisizo sahihi, laa sivyo nitaungana na wanachama wa kanda yangu tutatoa tamko latakalofuatiwa na kujitoa katika shughuli zote za kichama. Tunaweza!

UZURI WOTE WA MAELEZO YAKO YOTE MAZURI YAMEFUTWA Na KAULI YAKO MBOVU YA ' TUTAJITOA KWENYE SHUGHULI ZA CHAMA ' ! UNAMTISHA NANI ? JITOE HATA SASA HIVI .
 
Natoa saa 24 Mbowe na Dr Slaa najua mtasoma hii post, mchukue hatua na kuhakikisha Zitto hashambuliwi katika taratibu zisizo sahihi, laa sivyo nitaungana na wanachama wa kanda yangu tutatoa tamko latakalofuatiwa na kujitoa katika shughuli zote za kichama. Tunaweza!
Kwa vitisho hivi hata wewe ni majanga tu! Jitoe tu!... Mbona vitisho hivi hukutoa wakati ZITTO anawatumia akina MCHANGE, na Mtera kuchafua wenzake?
 
nimetoa saa 24 mkuu.
weka namba za viongozi wote wa chadema plus wabunge wote. Tuwachane waache upuuzi wao. Tuwaambie tumechoka na malumbano na ukimya wao. Tukikaa kimya na kulalamika utakuwa ufala tushachoka.sheeenz
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom