Mbowe: Mazungumzo ya Rais Samia tumeyapokea ‘positive’ na kwa tahadhari kubwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi wa vyama vya siasa leo Januari 3, 2022, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema:

Taifa letu limekuwa na mfumo wa ukandamizaji wa demokrasia kwa muda mrefu, kuanzia ngazi ya taifa hadi vitongozi, lakini tutaangalia kwa macho angavu jambo hio katika ngazi za nchini.

"Rais ameruhusu mikutano ya siasa iendelee, hilo ni jambo muhimu na jema kwa kuwa ni jambo la kikatiba.

"Sisi kama chama kikuu cha upinzani nchini tumelipokea jambo hilo positive, ni hatua muhimu.

"Amezungumza pia kuhusu kukwamua mchakato wa Katiba.

"Suala la Kikatiba siyo la kusubiri, ni suala la sasa na kizuri zaidi ni kuwa Rais amekuja na tamko la kuwa mchakato utaendelea na kutoufanya kuwa wa chama kimoja.

"Jambo zuri pia amezungumzia kuhusu ushirikishwaji katika mabadiliko ya Sheria, zipo nyingi sana zinatakiwa kufanyiwa maboresho.

“Huko nyuma Serikali ilikuwa inafanya mabadiliko ya Sheria, inaleta Bungeni katika Certificate of urgency, zinapitishwa bila kuridhia maoni au mawazo ya wapinzani au makundi mengine ya kijamii.

Kuna Sheria ambazo zinagusa umma kwa ukaribu kama Sheria kama za Vyombo vya Habari, za Uchaguzi, Takwimu na nyingine mbalimbali zinaoongoza taasisi zisizo za Kiserikali.

“Ushirikishwani ni mzuri, kwani kama mnavyojua Bunge letu leo ni la Chama kimoja, hivyo unavyopeleka Sheria ya Serikali ya chama hichohicho ni Sheria ya CCM na siyo ya Kitaifa.

"Kwa ujumla tumepokea tamko lake positive na kwa tahadhari kubwa, muhimu pia tutashirikiana na kutoa presha ili kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba ya Taifa ambalo italiunganisha Taifa.

“Sisi kama chama tutaenda kujadiliana katika vikao vyetu vya chama kwa kile ambacho kimejili Ikulu siku ya leo.”
 
Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi wa vyama vya siasa leo Januari 3, 2022, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema:

"Rais ameruhusu mikutano ya siasa iendelee, hilo ni jambo muhimu na zuri kwa kuwa ni jambo la kikatiba.

"Sisi kama chama kikuu cha upinzani nchini tumelipokea jambo hilo positive, ni hatua muhimu.

"Suala la Kikatiba siyo la kusubiri, ni suala la sasa na kizuri zaidi ni kuwa Rais amekuja na tamko la kuwa mchakato utaendelea na kutoufanya kuwa wa chama kimoja.

"Jambo zuri pia amezungumzia kuhusu ushirikishwaji katika mabadiliko ya Sheria, ni jambo la msingi Sheria kama za Vyombo vya Habari, Takwimu n.k

"Kwa ujumla tumepokea tamko lake positive na kwa tahadhari kubwa, muhimu pia tutashirikiana na kutoa presha ili kupatikana kw aTume Huru ya Uchaguzi.
Kwani LEMA anasemaje?
 
Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi wa vyama vya siasa leo Januari 3, 2022, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema:

"Rais ameruhusu mikutano ya siasa iendelee, hilo ni jambo muhimu na zuri kwa kuwa ni jambo la kikatiba.

"Sisi kama chama kikuu cha upinzani nchini tumelipokea jambo hilo positive, ni hatua muhimu.

"Suala la Kikatiba siyo la kusubiri, ni suala la sasa na kizuri zaidi ni kuwa Rais amekuja na tamko la kuwa mchakato utaendelea na kutoufanya kuwa wa chama kimoja.

"Jambo zuri pia amezungumzia kuhusu ushirikishwaji katika mabadiliko ya Sheria, ni jambo la msingi Sheria kama za Vyombo vya Habari, Takwimu n.k

"Kwa ujumla tumepokea tamko lake positive na kwa tahadhari kubwa, muhimu pia tutashirikiana na kutoa presha ili kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi.
Presha gani tena kwa jambo la kimantiki, nia njema na utashi wa kweli vitoshe kufanya yote kwa maana si Kwa faida ya mtu au kikundi cha watu bali ni kwa taifa zima kwa vizazi na vizazi
 
Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzungumza na viongozi wa vyama vya siasa leo Januari 3, 2022, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema:

"Rais ameruhusu mikutano ya siasa iendelee, hilo ni jambo muhimu na zuri kwa kuwa ni jambo la kikatiba.

"Sisi kama chama kikuu cha upinzani nchini tumelipokea jambo hilo positive, ni hatua muhimu.

"Suala la Kikatiba siyo la kusubiri, ni suala la sasa na kizuri zaidi ni kuwa Rais amekuja na tamko la kuwa mchakato utaendelea na kutoufanya kuwa wa chama kimoja.

"Jambo zuri pia amezungumzia kuhusu ushirikishwaji katika mabadiliko ya Sheria, ni jambo la msingi Sheria kama za Vyombo vya Habari, Takwimu n.k

"Kwa ujumla tumepokea tamko lake positive na kwa tahadhari kubwa, muhimu pia tutashirikiana na kutoa presha ili kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi.
Mwamba kama Mwamba

Tutamtoa_Mkoloni_Mweusi_Soon_on_Instagram%3A_%E2%80%9CMwenyekiti_wa_Chadema_Taifa_akisalimiana...jpg
 
Nchi Za Afrika Demokrasi Imejaa Ukakasi Muda Wote
Sheria Iko Wazi Kufanya Mikutano Na Imevunjwa Na Viongozi Walioapa Kuilinda
 
Hotuba ya mama bana. Was like...."tumewaruhusu wapinzani wapige kelele zao, hizo kelele wont bother me, nitazichukulia kama njia ya kuniboresha, na chama changu nshawapanga wamekubaliana nami"

Good luck maza!

Pengine hata wapinzani watakuwa wameshajifunza kucheza na k aliyeshikilia mpini bila kumtia kidole jichoni.
 
Nawashauri wapinzani waungane ili wawe na nguvu haina haja ya kuwa na vyama lukuki vya upinzani. Ikiwa wataunguna wananchi watakuwa na iman kubwa sana nao.
Wazo lako ni zuri, lakini unasahau kwamba hivyo unavyoviita vyama vya upinzani, na kuvishauri viungane ili viwe na nguvu zaidi, baadhi ya vyama hivyo havitofautiani sana na chama kilicho madarakani.

Kwa hiyo, wazo lako lingeleta maana zaidi kama ungeshauri vyama kama hivyo viungane na chama tawala, wanachokubaliana nacho zaidi kuliko hao wenzao walioko kwenye upinzani.

Maana ya ushauri wako huu ni kwamba unataka vyama vya upinzani viungane bila kujali ni wapi waliko na ushirikiano nako zaidi? Mbona kufanya hivyo itakuwa ni kuua upinzani moja kwa moja!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom