shansarie
JF-Expert Member
- May 25, 2013
- 5,690
- 3,370
jamani ikiwekwa nyingine tujizane MziziMkavu
Last edited by a moderator:
[h=1]Majangaaa Mbona Majangaaa! - 23[/h]
Alipomaliza kuufungua hakusimama tena mlangoni, moja kwa moja akarudi kitandani kwake na kujitupa juu yake.
Rehema naye alipofika, wala hakujibalaguza, akausukuma mlango na kuingia chumbani humo.
Ni wakati alipokuwa akiingia ndipo, kuna mtu aliyekuwa akitokea barazani akiingia ndani, akamuona Rehema akiishia chumbani kwa Eddy.
Mtu huyo akashangaa! Akajiuliza kama Eddy alikuwa amerudi au la. Alipokosa jibu akadhani labda Rehema alikuwa ameachiwa ufunguo.
Rehema alipohakikisha kwamba ameishaingia chumbani humo wala hakutaka kungoja, moja kwa moja alimfuata Eddy pale kitandani alipokuwa amelala na kuanza kumkumbatia.
Eddy hakuwa na ujanja wa kukataa kumpokea Rehema pamoja na kwamba hakutegemea kufanyiwa kitu kama hicho, yeye alihisi kesi kuhusiana na mambo yaliyotokea jana yake usiku ingeanza kisha mambo hayo yangefuata baadaye.
Bila ya kujivunga mtoto wa kike akaanza kumshushia mabusu ya nguvu Eddy, akawa anampandisha morali wake kwa kumshika kila kona ya mwili wake.
Wakati alipokuwa akiyafanya hayo, Rehema alikuwa akisindikiza vitendo hivyo na sauti ya kilio, alikuwa akilia kwa sauti ndogo yenye kusisimua.
Kilio chake kiliongeza hamasa ya kumpagawisha Eddy aliyekuwa amelala na kumwachia msichana huyo afanye anachotaka.
Awali Eddy hakuwa akisikia kile Rehema alichotaka akisikie lakini kadiri muda ulivyoenda ndivyo msichana huyo alivyokuwa akiongeza majonjo ya kumpagawisha.
Ilifika hatua, Eddy alisalimu amri, akaanza kujibu mashambulizi ya Rehema, ilipofika hatua hiyo sasa ikawa kama fujo, wakawa kama wanamichezo wa miereka, wakawa wanazungushana juu ya uwanja ule wa sita kwa sita, mmoja akiwa juu mwingine anakuwa chini, kila mmoja alikuwa akifanya kile anachokijua katika kumpagawisha mwenzake.
Waliendelea hivyo kwa muda mrefu na hatimaye wakawa kama wanaishiwa pumzi, kila mmoja akawa anavuta pumzi za ziada, hamasa ikiwa imewapanda kwa asilimia mia moja.
Bado kilio cha Rehema kilikuwa palepale, alikuwa akilia kwa sauti ndogo kuonesha manunguniko aliyonayo juu ya Eddy.
Kwa nini unanifanya hivi?
aliuliza Rehema huku akisaula viwalo vya mwenzake huyo.
Eddy hakujibu kitu, alikuwa kimya muda wote ingawaje pombe ilikuwa ikianza kumtoka kichwani mwake.
Rehema alipoona kimya wala hakukata tamaa, akaiondoa t- shirt aliyokuwa ameivaa Eddy na kuitupa pembeni.
Akawa anatafuta sehemu ambazo zingeweza kumpagawisha zaidi mvulana huyo.
Baada ya muda akaona kama vile alikuwa akichelewa kufikia lengo lake, akaifungua njia ya kuingia ikulu kwa kuivuta chini zipu iliyokuwa imeziba njia hiyo.
Kwa nini unanifanyia hivi? alirudia tena Rehema huku akimshika askari wa Eddy na kumwingiza katika njia ya kupitishia chakula.
Eddy alizidi kupagawa, kijasho chembamba kikaanza kumvuja.
Unataka nikufanyie nini ? bado Rehema aliendelea na maswali lukuki ambayo yalikuwa hayajibiwi na mwenza wake.
Rehema akaona kama vile hatosheki na kile alichokuwa akikifanya, akamwondoa Eddy kiwalo kingine muhimu katika maungo yake.
Akaendelea na zoezi lake hadi pale alipomuona Eddy akiwa mtupu kama alivyotoka katika tumbo la mama yake , naye akainuka na kuondoa vya kwake.
Mechi ilikuwa ikitaka kuanza, ndipo mlango ulipofunguliwa, mtu aliyefungua mlango aliingia na kuwaona wawili hao kwa msaada wa taa ya ukumbini kwa kuwa mlango aliuacha wazi.
Wote wakatahamaki na kujiuliza nini kilikuwa kikiendelea. Rehema ndiye aliyekumbuka kuwa wakati alipokuwa akiingia mle ndani hakuwa ameufunga mlango.
Eddy, sauti ya kike iliita na wote wawili wakaifahamu ni sauti ya nani.
Kama vile haitoshi aliyewaita akageuka na kwenda kuwasha taa na kuwashuhudia wawili hao wakiwa wamejilaza kitandani tayari kwa kuendelea na ngwe ya kupeana burudani.
Eddy hiki ni nini? alisema mwanamke huyo ambaye hakuwa mwingine zaidi ya Queen.
Queen alikuwa amesimama mbele yao akiwakodolea macho kama vile askari aliyekuwa amewakuta wahalifu wake.
Kwa nini unaingilia starehe za watu? hatimaye Rehema aliweza kupata maneno ya kuonge huku akimwangalia Queen.
Starehe za watu? Wewe una starehe gani hapa mjini zaidi ya umalaya ?
Ndiyo miye ni malaya na wewe ni nini kilichokuleta humu ndani?
Kauli hiyo ilimkera Queen aliyetoka mzimamzima na kumvaa Rehema pale kitandani, Rehema naye hakukubali akakunjua makucha yake na kumshika Queen kisawasawa.
Wawili hao wakaanza kushika huku wakipigizana kelele, hali iliyowashtua watu wengine waliokuwa katika vyumba vyao.
Watu hao wakaanza kuamka na kutafuta kelele zinapotokea, wakagundua kuwa zilikuwa zikitokea chumbani kwa Eddy.
Waliposikiliza vizuri wakagundua kuwa sauti za wanawake wawili zilikuwa zikijibishana, sauti hizo hazikuwa ngeni masikioni mwao, wakaamua kuvamia chumba hicho.
Je, nini kilifuatia chumbani humo? Usikose kufuatilia
Eddy ameamua kuondoka nyumbani kwa wazazi wake na kwenda kupanga, kwa bahati nzuri anapata chumba katika nyumba moja yenye vyumba sita maeneo ya Mwananyamala kwa Kopa.
Nyumba hiyo imekaa Kiswahiliswahili kutokana na wapangaji wanaoishi ndani ya nyumba hiyo.
Kila chumba kimoja kilikuwa na mpangaji mmoja aliyekuwa akiishi na familia yake.
Pia katika nyumba hiyo iliyokuwa na mabanda ya uani, waliishi wapangaji ambao hawakuwa na wake wala waume.
Kati yao walikuwepo wasichana wazuri wenye maumbile ya kupigiwa methali, ambao wengi wao hawakuwa na shughuli maalumu za kuwapatia kipato.
Baba na mama mwenye nyumba nao walikuwa wakiishi ndani ya nyumba hiyohiyo.
Siku ya kwanza Eddy alipokuwa akihamia hakuwa na vitu vingi zaidi ya kitanda kidogo, kabati la nguo na vikombe sita vya chai.
Pia alikuwa na sahani mbili za chakula na jiko moja la Mchina. Kijana huyo aliamua kuanza maisha hayo ya usela japokuwa wazazi wake walikuwa na uwezo mkubwa sana.
Baba na mama yake walimsihi sana kuendelea kukaa nao maeneo ya Kinondoni lakini wala hakutaka kusikiliza ushawishi huo.
Kikubwa alichokuwa akikitaka Eddy ni uhuru, kwani alijiona ameshakua mkubwa, hakutaka kufanya mambo ya uhuni ndani ya nyumba ya wazazi wake.
Mbali na hivyo wazazi wake walikuwa wakimdhibiti sana kijana wao kuingia katika maisha ya kupenda wanawake, hawakutaka ajiingize huko mapema.
Eddy alivumilia ucha Mungu wa wazazi wake kwa kipindi kirefu lakini alipomaliza shule tu hata kabla majibu ya kidato cha nne hayajatoka, akaamua kuhama.
Ushawishi huo aliupata kwa marafiki zake, Salim Raha na John Tupatupa ambao walikuwa na uhuru mkubwa wa kuingiza vyumbani mwao kila aina ya warembo.
Naye alitamani uhuru huo, akaamua kuwaaga wazazi wake na kuondoka katika nyumba ya familia.
Lakini kabla ya kuhama, mara kadhaa kijana huyo alikoswakoswa kunaswa na wazazi wake pale alipoingiza msichana chumbani kwake.
Siku ya kwanza alipoingia katika makazi mapya alikutana na Rehema, msichana wa Kizaramo aliyekuwa ameumbika vyema.
Eddy alishtuka kiasi hata Rehema mwenyewe kuhisi mgeni huyo alikuwa amepagawa kisawasawa. Siku hiyo mrembo huyo alikuwa akisugua miguu yake katika jiwe maalumu lililopo karibu na mlango wa kuingilia msalani.
Rehema alikua ametoka kuoga, akiwa amevaa kanga moja tu iliyokuwa imelowana na maji na kumfanya maungo yake ya ndani yaonekane.
Ndiyo, kanga ilikuwa imeshikana na mwili na kila Rehema alipokuwa akisugua kisigino chake, ndivyo alivyokuwa akimpagawisha Eddy kutokana na kuzalisha mtetemeko wa haja katika mlima aliokuwa ameufungashia nyuma ya mgongo wake.
Kijana huyo alibaki ameduwaa kwa kitambo kirefu akimwangalia Rehema huku akiwa ameshika sahani mikononi mwake lakini Rehema ndiyo kwanza akajifanya kama vile hakuwa amemuona.
Binti huyo akaendelea kufanya kile alichokuwa akikifanya, mara alishtuka aliposikia mlio wa vyombo vikipasuka.
Ndiyo, Eddy alikuwa ameziachia sahani alizokuwa amezishika mikononi mwake bila ya kutarajia.
Kufuatia mlio uliotokana na sahani kuvunjika, Rehema alimgeukia Eddy na kumuuliza kulikoni ndipo kijana huyo alimwambia zilimteleza kwa bahati mbaya.
Ndiyo kwanza mchezo unaanza, unataka kujua zaidi? Weka Like chini ndio nitajuwa munaipenda hii hadithi pasipo weka like sitoweza kuendelea na Hadithi Mpya mnasemaje kuhus hadithi mpya?
Majangaaa Mbona Majangaaa! - 3-
ILIPOISHIA
MAJANGAAA, jamani mbona Majangaaa! alisema Eddy kimoyomoyo wakati alipotoka nje na kukutana na wasichana hao kibao wakiwa wamejipanga uwani kwa ajili ya kusubiri kwenda kuoga.
Samahani kaka naomba sabuni alisema yule msichana wa kwanza aliyewawahi wenzake kwenda msalani akimwambia Eddy.
Bila wasiwasi, Eddy alisema na kumkabidhi binti huyo sabuni yake ya kuogea.
Daa! Unaanza kujipendekeza kwa mgeni, alisema msichana mwingine na kuwafanya wengine nao waongeze maneno yao kedekede ambayo hata hivyo binti yule hakuyajali.
NINI KILIENDELEA? POROMOKA NAYO
Baada ya muda binti yule alitoka bafuni na kwenda moja kwa moja kumrudishia Eddy sabuni yake, alipofika usawa wa chumba cha kijana huyo, Irene alikuwa na kusudio moja tu, kutaka kumshawishi ili awe wake hata kabla msichana yeyote anayeishi ndani ya nyumba hiyo hajamnasa.
Alitaka kutumia ushawishi wake kumnasa mwanaume huyo ambaye alikuwa amemvutia kutokana na urefu wake na umbile lake la kimazoezi.
Aliamini kabisa kwamba yeye ndiye aliyekuwa akiendana na mwanaume huyo tofauti na msichana mwingine aliyepanga pamoja na watoto wa baba mwenye nyumba.
Tangu akiwa anamuomba sabuni, msichana huyo alikuwa ameshajua jinsi alivyoutega mtego wake wa kumnasa kijana huyo.
Alitoka msalani akiwa amevaa kanga moja iliyokuwa ameilowanisha maji na kujaribu kujitingisha kwa mwendo wake wa madaha, moja kwa moja akawapita wasichana wengine waliokuwa wakigombea nafasi ya kwenda kuoga baada ya yeye kutoka.
Alitembea kwa mwendo huo uliojaa uchokozi na kisha kuusogelea mlango wa chumba cha Eddy, bila ya kubisha hodi akaufungua kidogo na kuchungulia, wakati huo macho yake alikuwa ameyaachia kwa kuyalegeza na kuyafanya kama yatake kudondoka.
Kaka samahani sabuni yako hii alisema akiwa ameuingiza uso wake ndani ya chumba cha Eddy aliyekuwa akivaa kwa ajili ya kujiandaa kutoka.
Eddy alishtuka na kumfanya binti huyo naye kujidai kumuomba radhi kwa kitendo alichokuwa amekifanya lakini wakati akifanya hivyo, tayari mwili wake wote ulishakuwa ndani ya chumba cha kijana huyo.
Naitwa Irene alisema huku akionekana kukikagua chumba kile kama vile alikuwa ametumwa kwa ajili ya kufanya kazi ya ukaguzi.
Eddy alikohoa kidogo kutoa kikohozi kikavu kisha akamjibu:
Miye naitwa Eddy au Eddyson Manyara, wakati huo kijana huyo alikuwa akichomekea shati lake.
Oooh oooh jina zuri sana naona ndiyo unaanza maisha? alisema Irene akiwa anamwangalia Eddy baada ya kukagua chumba hicho na kukiona kila kilichokuwemo ndani yake.
Eeehe, nimeamua kuondoka kwa wazazi na kuishi peke yangu ili kujipanga zaidi, Eddy alisema kwa aibu.
Kwa hiyo umekuja kwa walimu tukufunze maisha?
Sijakuelewa ? alihoji Eddy.
Siku zote Waswahili husema anayeshindwa na wazazi hufunzwa na walimwengu, siye ndiyo walimwengu wenyewe karibu sana na jisikie kama uko nyumbani kwa wazazi wako.
Aaah aaah Eddy alicheka na kuendelea kuvaa shati lake tayari kwa kutoka nje ya chumba chake na kwenda kwenye mihangaiko yake.
Unafanya kazi? Irene alimuuliza Eddy.
Yaa, nafanya kazi
Sawasawa karibu sana alisema Irene huku akifungua mlango na kutoka nje kwa madaha, akijitahidi kuutingisha mwili wake.
Wakati Irene akitoa mguu wake nje ya chumba hicho ghafla alipoinua uso wake kuangalia mbele akakutana uso kwa uso na Rehema akiwa anapita kwa ajili ya kwenda uwani.
Rehema hakuonekana kumchangamkia Irene ambaye ndiyo kwanza walikuwa wakionana tangu kulipopambazuka siku hiyo.
Za asubuhi dada? alisema Irene kumwamkia Rehema kwa haraka huku akichekacheka lakini salamu yake haikuitikiwa, akabaki ameduwaa.
Rehema alimpiga jicho kali Irene kwa kumshusha na kumpandisha kisha akaenda zake uwani hali iliyomfanya Irene kufadhaika, moja kwa moja akajua kuwa ameingia kwenye vita na malkia wa nyumba hiyo.
Irene alijaribu kufikiria ni nini kimetokea kati yake na Rehema lakini hakuambua kitu. Alifikiria labda jana yake alikuwa amemkosea, pia hakukumbuka kutokea kitu kama hicho.
Hivi huyu brother men anaweza kuwa chanzo? alijiuliza akimfikiria Eddy.
Nini kitaendelea? Usikose kufuatilia Jumapili ijayo ............
duuuu hii kweli majanga hiyo sehemu ya rehema kuloanisha makalio yake huku amevaa kanga mmoja na kusababisha kanga kunasa mmoja kwa mmoja kwenye makalio ni hatari lazima hapo mtu mzima uingie kwenye mtegoMajangaaa Mbona Majangaaa! - 4-
Rehema alimpiga jicho kali Irene kwa kumshusha na kumpanisha kisha akaenda zake kuelekea
uwani hali iliyomfanya Irene kufadhaika, moja kwa moja akajua kuwa ameingia kwenye vita na
malkia wa nyumba hiyo.
Irene alijaribu kufikiria ni nini kimetokea kati yake na Rehema lakini hakuambua kitu. Alifikiria
labda jana yake alikuwa amemkosea, pia hakukumbuka kutokea kitu kama hicho.
Hivi huyu brother men anaweza kuwa chanzo? alijiuliza akimfikiria Eddy.
NINI KILIENDELEA? POROMOKA NAYO
Irene akiwa katika mawazo hayo akasema kama kweli chanzo ni huyo kijana, basi atahakikisha kwamba anakula naye sahani moja ili kuzidi kumvimbisha mashavu Rehema.
Malkia malkia wala sitajali kama ni malkia wa nini, watu tumewaona mamalkia wa maana atakuwa yeye malkia wa vichochoroni, alisema Irene na kisha akaachia msonyo wa nguvu uliosikika hadi nyumba ya pili.
Wakati huo alikuwa ameshaingia chumbani kwake na kuanza kujikwatua kwa kuupara uso wake kwa mapambo ya kila aina ambayo yalipaswa kuingia usoni pake.
Wakati akiendelea kujipamba kila dakika ilivyokatika ndivyo alivyokuwa akikikumbuka kitendo alichofanyiwa na Rehema.
Alikasirika sana kuona anamsalimia halafu anamvimbishia mashavu bila ya kujua sababu, kila alivyokumbuka kitendo hicho aliachia msonyo na kuendelea na shughuli zake.
Asubuhi asubuhi mtu anakuharibia siku, alijisemea peke yake Irene wakati akijiangalia kwenye kioo kisha akaachia msonyo mwingine.
****
Kwa upande wake, Rehema roho yake ilikuwa imemchafuka, ikimchonyota kwa kumuona Irene akitoka chumbani kwa Eddy, moja kwa moja akajua kuwa wawili hao watakuwa wamelimenya tunda la mwituni asubuhiasubuhi.
Haiwezekani lazima watakuwa wamepeana kile kitu roho inapenda, iweje atoke chumbani kwake asubuhi yote hii? alijihoji na kukosa jibu la uhakika.
Rehema alikuwa amechukia kwelikweli na moyo wake ulimuuma kwa kuona kwamba Irene anaanza kuwa na uhusiano na mwanamme huyo mgeni kabla yake.
Atakuwa ameingia asubuhi ileile au atakuwa amelala chumbani kwake? alijiuliza tena Rehema huku donge likiwa limemnasa rohoni mwake.
Yaani atakuwa ameshanizidi kete? aliwaza Rehema ambaye aliamini kabisa kwamba mitego aliyomtega Eddy siku ya kwanza ilikuwa ni lazima amnase kwanza kabla ya kinyangaratika kingine ndani ya nyumba yao.
****
Kwa upande wake Eddy ambaye alitoka baada ya kujipulizia utuli uliouteka ukumbi wa nyumba hiyo, alikwenda moja kwa moja kwenye shughuli zake kubaingiza, kwa kuwa bado hakuwa na kazi ya kufanya.
Alikuwa akifanya kazi yoyote ambayo aliamini kuwa ingeweza kumwingizia kipato.
Siku hiyo alikwenda moja kwa moja hadi kijiweni kwake maeneo ya Kariakoo ambako vijana wengi hukutana na kuuza maneno kwa watu wengine ili wapate chochote kitu.
Moyoni mwake Eddy hakuwa salama hata kidogo, kwa kuwa vitendo viwili vilikuwa vikimchanganya akili yake kwani moyo wake ulikuwa ukiripuka kila alipokuwa akikumbuka jinsi alivyomuona Rehema akisugua kisigino chake ilhali amevaa khanga moja iliyokuwa imelowana sehemu za makalioni.
Moyo ukitulia unaripuka tena kwa kitendo cha Irene kuingia chumbani kwake akiwa na khanga moja ambayo nayo ikiwa imelowana, Eddy alivuta taswira za mabinti hao wawili na kubaki akiwa hana la kufanya.
Kila mmoja ana uzuri wake Eddy aliambia nafsi yake na kubaki na dukuduku moyoni mwake. Mpaka wakati huo hakuwa akijua kama amesababisha songombingo kati ya wasichana wawili hao.
Hilo hakulijua kwa kuwa hakuliona wakati likitokea, kwa sababu alikuwa chumbani kwake, laiti kama angeliona angejua cha kufanya, asingekuwa na budi kuchagua upande mmoja.
Lakini moyo wa Eddy ni kama wa wanaume wengine, haukulidhika na mmoja, unataka kumi na moja kwa kutaka kuonja kila sehemu ili kujua radha yake.
Eddy alikuwa akitaka kujua utamu wa Rehema lakini pia alikuwa akitaka kujua utamu wa Irene kwa kuwa damu yake ilikuwa ikichemka, kikubwa alikuwa akijiuliza itawezekanaje ndani ya nyumba moja!
Hilo ndilo lililokuwa likimitia mashaka, vinginevyo alikuwa akiwataka mpaka wengine waliokuwa wakiishi ndani ya nyumba ile kwani aliamini kuwa kila mti una tunda lake na kila tunda lina utamu wake.
Eddy alikwenda mjini na kuzugazuga kwa jamaa zake maeneo ya Shule ya Uhuru Karikooo, huko alikutana na marafiki zake Spider au Raha na John Tupatupa na kuongea nao kile kilichomkuta katika nyumba ile aliyohamia.
Hapo lazima ucheze kama Pele lakini kwa jinsi unavyonihadithia kitu hapo ni Rehema alisema Raha.
Mmmh mwana usipepese macho wala kuuma meno, hapo kitu ni Irene aliongeza John Tupatupa ambaye alimlaumu Eddy kwa nini hakumaliza mchezo wakati mzigo ulipoingia chumbani.
Washikaji sasa mnanichanganya niacheni nitumie akili yangu, Eddy aliwaambia baada ya kuona kila mmoja akiwa na mtazamo wake kuhusiana na mabinti hao.
****
Rehema hakuwa ameridhika, alipofika uwani alipishwa kwenda msalani na mabinti waliokuwa katika foleni kwa kuwa yeye ni malkia wa nyumba hiyo.
Akaoga na kumaliza haja zake muhimu, kama kawaida alipotoka alisugua miguu yake huku akiwa na hamu ya kutaka kujua Irene aliingiaje chumbani kwa Eddy.
Alipomaliza shughuli zake akamchukua mmoja wa mabinti waliokuwa wakisubiri kwenda kuoga na kumwambia amfuate chumbani kwake.
Binti akajua labda ametafutiwa mtu wa kuduu naye, akawa na wasiwasi wakati alipokuwa akiambiwa kuingia chumbani kwa malkia.
Usiogope kaa hapo kwenye sofa alisema na binti akiwa na wasiwasi akaketi.
Ulimuona Irene leo?
Ndi ndi- yoooo, nilimuona dada
Ulimuona wakati gani?
Alipokuwa akitoka kuoga
Hukumuona alipoingia chumbani kwa yule mgeni ?
Wala sikumuona lakini kama aliingia atakuwa alikwenda kumrudishia sabuni yake
Kwani alichukua sabuni kwake?
Eeeh wakati akiwa anatoka kuoga yule mkaka, dada Irene akamuomba sabuni ya kuogea alisema binti yule na kuifanya roho ya Rehema kuanza kupona kidonda cha wivu kilichokuwa kikimkereketa.
Oke nenda, usimwambie yeyote nilichokuuliza.
Sawa.
Baada ya binti yule kutoka nje, Rehema alifurahi sana, akajua kuwa Irene hakuwa ameambulia kitu. Akafurahi na kujitupa kitandani na kukumbatia mito.
Je nini kiliendelea? Usikose kufuatilia Alkhamisi ijayo...................
Oya vipi
Mi nge mwambia queen vua nguo uje kitandan asiyeridhika mlango upo wazi
mbwiga tuu huyu kanichefua kweli yani natamani nimtapikiehuyo mshikaji hapo juu mshamba tu anaweka kiwingu badala ajisomee kwa faida yake anatukopia vitu vya longtime sijui katokea wapi sijui labda sitimbi
duuuu hii kweli majanga hiyo sehemu ya rehema kuloanisha makalio yake huku amevaa kanga mmoja na kusababisha kanga kunasa mmoja kwa mmoja kwenye makalio ni hatari lazima hapo mtu mzima uingie kwenye mtego
wa wapi wewee? Unatuzengua bana...kama vipi copy ukawaelimishe dada zako bana
kuna haja gani ya wewe kuchangia sio lazima kila kitu uchangie unaweza ukakaa kimya