[h=1]Majangaaa Mbona Majangaaa! - 27-[/h]
ILIPOISHIA …
Eddy alitoka zake huku akimwacha Pat pale ukumbini akiendelea kumwangalia kwa udadisi. Moyoni mwake Pat aliamini kwamba kijana huyo alikuwa na kitu cha ziada kwa wasichana.
"Kwanza mchangamfu halafu amekaa vizuri…" aliwaza huku akiwa anasumbuka kutaka kujua kama kweli Tabu alikuwa amegonga naye shoo.
Baada ya kutafakari kwa muda, Pat aliamua kumfuata tena Tabu chumbani ili kumuuliza kama kweli alikuwa amevunja amri ya uzinzi na Eddy.
SASA POROMOKA NAYO…
Alipoingia chumbani akamkuta Tabu akiwa bado amelala, akaanza kumwamsha kwa upole tofauti na mwanzo alivyoingia chumbani humo kwa mara ya kwanza na kumwamsha kwa ukali.
Mbali na kufanya hivyo, awali alikuwa akimlazimisha Tabu kuhusu ishu ya kugonga shoo na Eddy, safari hii ilikuwa tofauti.
Tabu alipoamka, Pat akaanza kumuuliza kwa upole ili aweze kujua ukweli, moyoni wivu ulikuwa ukimtafuna kwa kuhisi kuwa amepigwa bao na msichana mwenzake.
"Shoga hebu tuache utani mimi na wewe ni marafiki wa muda mrefu, hebu niambie kile ulichokifanya na Eddy chumbani kwake…" alianza kwa kumbembeleza.
"Wee si umesema unaenda kuwaambia dada Rehema na Queen? Nenda tu miye wala sina wasiwasi…"
"Hebu tuachane na hayo, miye na wewe ni damu damu, yale yamepita shoga'angu maana nimekutana na huyu mwanaume hapo ukumbini, wee acha tu…"
"Unamaanisha nini kwani na wewe unamtaka?"
"Hivi katika akili yako kuna mwanamke ambaye anaweza kukataa kuwa na mwanaume kama yule?" Pat alijibu kwa kuuliza swali.
"Mh! Makubwa."
"Madogo yana nafuu shoga, hebu niambie basi kama mwenzangu umeshawahi?" alichombeza Tabu.
Tabu hakuweza kumjibu Pat akabaki akicheka na kumfanya Pat kuendelea kuhisi kwamba kulikuwa na ukweli kwa kile alichokuwa akikifikiria ndani ya nafsi yake, hata hivyo hakutaka kujiridhisha kwa hisia tu, akataka kuambiwa ukweli na mhusika.
Akaendelea kumuuliza Tabu ili amwambie kwa mdomo wake kile kilichojiri.
Baada ya kutafakari kwa kina, Tabu akaona hakukuwa na haja ya kumficha, akaamua kumwambia Pat kile kilichojiri chumbani kwa Eddy.
"Yaani shoga wee acha tu," akaanza kusema huku akijiinua kutoka kitandani na kukaa.
"Mh! Lete habari…" Pat alichombeza huku naye akijiweka sawa kwa ajili ya kupata ukweli kamili.
"Yule mwanamme sijui hata ana nini… maana ghafla tu nilijikuta nikimtamani… lakini alifanya kosa moja tu, alianza kunidharau… pale aliponiambia kwamba miye ni mtoto mpaka nilipomhakikishia kwamba miye ni mkubwa mwenziwe…"
"Kweli…?" alihoji Pat na kumfanya Tabu kuendelea kuhadithia kile kilichotokea kati yake ya Eddy…
"Nilipomhakikishia hivyo, akanifuata pale nilipokuwa nimesimama, ilikuwa ni katikati ya chumba na kunipeleka kwenye uwanja wa fundi seremala.
"Hapo akapitisha mikono yake kwenye nywele zangu na kuzichambua kwa vidole vyake, kisha akachora ramani mwilini mwangu kwa kutumia mikono yake na kunisisimua vya kutosha.
"Kisha akaanza kutumia silaha ya nyoka…" Tabu alisema na kukatishwa na Pat.
"Silaha ya nyoka ndiyo nini Tabu mbona unaniacha kama kishada kinachokwenda halijojo…?"
"Aaah aaah kumbe nilikuwa nakuacha…, pole shoga'angu si unajua inanibidi nitumie lugha ya tafsida, basi namaanisha ile silaha anayoitumia nyoka akitaka kutema sumu yake.""
"Hapo nimekupata ni ulimi…" alisema Pat.
"Yesii, ulimi wake ulipita nyuma kidogo ya shingo yangu na kuzidi kunipandishwa wazimu… nilikuwa nasikia raha kama vile natambaliwa na sisimizi shingoni," aliendelea Tabu na kumfanya Pat kukaa vizuri ili kupata uhondo zaidi.
"Baada ya hapo akawa anasafiri na ulimi wake kwa kupita kila sehemu aliyoiona inafaa, sehemu ya kuweka kituo kwa muda aliweka na kuendeleza utundu wake.
"Kisha akahamia kwenye embe sindano zangu, akawa anazivuta kwa ndani na kisha kuzitoa nje kwa kutumia njia yake ya kupitishia chakula, weee acha tu… wazimu si wazimu raha si raha, sijui hata nikwambieje…"
"Mh!"
"Alipotoka hapo alipitisha silaha ya nyoka katika maeneo mengine nyeti kwenye maungo yangu na kunifanya nizidi kumchemka kwa hisia kali, akafika hadi kwenye kile kitu ambacho mara baada ya mtoto kuzaliwa baada ya muda huwa kinakatika chenyewe…"
"Nini hicho?"
"Kwani wee hujawahi kusikia kuanguka kwa kitovu cha mtoto…?"
"Aaah nimewahi kusikia shoga…" aliitikia Pat.
"Basi alipofika hapo, mashetani yalitaka kunipanda… nilitamani hata kupiga kelele ili anichie au nipate msaada wa kusaidiwa maana aliniweza kwelikweli…"
"Wee acha utani…" Pat alihoji.
"Kweli vile…" alisisitiza Tabu.
"Mh! Basi makubwa," Pat aliguna.
Mwili ulinitoka vipele kama vile nilikuwa nikitambaliwa na sisimizi au nilikuwa nikitaka kuugua ugonjwa wa malaria. Alipotosheka akapitiliza hadi kwenye bastola zangu…"
"Halafu… ikawaje…" Pat alijawa na udadisi wa kina wa kutaka kujua kile kilichoendelea.
"Hapo kwenye bastola zangu hakukaa sana, akaenda moja kwa moja kumsalimia bibi kule shambani."
"Acha utani…?"
"Kweli vile, yule kijana ana heshima kwelikweli… kwani alipofika kwa bibi aliamua kumwamkia kwa heshima zote, alipiga magoti na kumsalimia kwa kuzungumza naye kwa kinywa chake… huku silaha yake ikiwa ni ileile anayoitumia nyoka."
"Aiseee…" Pat aliropoka bila ya kujijua na kumfanya Tabu ageuke na kumwangalia.
" Hapo ndipo nilipoanza kusikia kizunguzungu kama siyo kichinachina… nilisi kama vile nataka kukata roho, kuna wakati nilifikiria kama vile sikuwa duniani… kweli dada Rehema na Queen walikuwa wanafaidi…
"Mh! Endelea basi akawa anafanyaje…? Pat alikuwa akitaka kujua uhondo huo aliokuwa akisimuliwa na Tabu jinsi ulivyonoga.
"Wee acha mwanaume pale yupo, alipomaliza kumsalimia bibi wakati huo miye nusu nilikuwa duniani na nusu nilikuwa peponi, nilikuwa kama vile niko ndotoni…"
"Aisee ulifaidi…" Pat alisema.
"Si kidogo, lakini mchezo kamili ulikuwa kwenye shoo yenyewe maana hiyo yote ilikuwa ni kama rasharasha vile vumbi lenyewe lilitimka pale alipoingiza kisu kwenye ala ndipo nilipochoka… kweli nilijiona ni mtoto…," alisema Tabu.
"Kwa nini," Pat aliendelea kuhoji.
"Kisu chake kilipoingia kwenye ala nilisikia kama vile mawimbi ya maji yakipiga kisimani, kali mawimbi yenyewe yalikuwa yanafanana na yale ya baharini lakini hayo yalikuwa kama yana mvutano wa umeme, aah Pat wee acha nilipiga kelele," alisema Tabu.
"Kwa hiyo umemvulia kofia…?"
"Si kidogo hapa unaponiona niko hoi, ulipokuwa ukinisemesha muda ule nilikuwa nakuona kama vile ulikuwa unanizungua tu…" alisema Tabu.
"Kumbe?"
"Eeeh wee acha tu, Eddy anajua kuizungusha funguo katika kufuli kwelikweli…" alisisitiza Tabu na kumfanya Pat kuanza kupatwa na hamu ya kile alichokuwa akifanyiwa mwenzake.
Nini kiliendelea? Usikose kufuatilia siku ya Alkhamisi ijayo.....