Majangaaa Mbona Majangaaa! - 14-
Moyoni mwake Eddy alikiri kwamba Queen alikuwa mzuri sana lakini hata ungemuuliza kati ya msichana huyo na Rehema nani alikuwa zaidi, asingeweza kutoa jibu mwafaka.
Alikuwa amebaki katikati na kuwa na kisebusebu na kiroho papo, huku anataka na kule anataka.
"Tafadhali usiniite jina la Mala… wako."
"Samahani… nilighafirika."
"Kwa hiyo utaniita jina gani?"
"Queen," alisema Eddy huku akionekana kuwa mnyonge. Jina hilo lilimfurahisha sana Irene akatabasamu na kufungua matuta yaliyokuwa yametanda kwenye sura yake.
"Asante baby…" alisema na kurudia zoezi alilokuwa amelianza.
POROMOKA NAYO…
Queen kama alivyomwita Eddy aliporudia safari hii alikuwa na mzuka mpya, akahakikisha kuwa anampagawisha Eddy kwa ujanja wake wote.
Kweli hali hiyo ilizidisha mzuka wa Eddy akawa anahamasika na kupandwa na munkari kwa askari wake kuonesha dalili zote za kutaka kuingia vitani.
Eddy hakujua hata nguvu alizipata wapi, akamgeuzia kibao Queen na kuanza kumshambulia kwa kufanya kujibu mashambulizi ya nguvu… akahakikisha haonekani ----- mbele ya Queen.
Akapitisha ulimi wake katika kila kiungo cha Queen. Akaanzia shingoni kisha akapanda hadi kwenye mdomo hapo wakabadilishana ‘kinywaji' na Queen.
Eddy alipotosheka akarudi kwenye viwambo vya kusikilizia sauti, yote hiyo ilikuwa ni kumsaka shetani wa Queen. Kila kipengele ambacho Eddy alichokigusa kilikuwa kikimtia wazimu Queen.
Alipotosheka kumpagawisha sehemu moja akahamia nyingine hata pale alipoona viwalo vya Queen vinamwondoa mchezoni alihakikisha anaviondoa.
Baada ya kuviondoa vyote akawa anashuka chini kwa kupitia shingoni na kuuacha ulimi wake utalii katika maungo ya ‘bintani' huyo.
Akawa anashuka chini hadi kwenye embe sindano za Queen, akawa anazinyonya embe hizo na kumpandisha mori kiasi cha kumfanya akose uvumilivu na kuanza kulia.
Hata hivyo, kilio chake kilikuwa ni tofauti na kile kilio cha kawaida, alikuwa akilia kwa furaha, kilio adimu kutokea kwa binadamu.
Kilio chake kilikuwa kikiongeza hamasa moyoni mwa Eddy ambaye alimini kuwa alikuwa amemuweza. Aliamini kuwa kiwango chake cha kupagawisha kilikuwa kimeongezeka.
Pamoja na kilio hicho cha Queen, Eddy hakuacha kufanya kile alichokuwa akikifanya, ndiyo kwanza akawa anazidisha majonjo, alipoona amempatia vyema msichana huyo, akazidisha makeke kwa kuweka vikorombwezo vingine vingi tu.
Alipotosheka akashuka tena chini, akafikia kwenye tumbo jembamba la Queen, tumbo ambalo lilikuwa vigumu kwa mtu kujua kama msichana huyo alikuwa ameshiba au alikuwa na njaa.
Hapo hakuchukua muda mrefu sana kupiga deki kama siyo kupiga msasa kwa kutumia ulimi wake, akashuka tena chini, akafika kwenye kiuno, hata hapo hakuchukua muda mrefu.
Akashuka chini zaidi, zaidi na zaidi, akafika sehemu adimu kufikika, sehemu yenye ulinzi mkali lakini Eddy aliweza kuwapangua walinzi wote na kuweka ulimi wake.
Queen alichanganyikiwa, akajihisi kama alikuwa yuko katika pepo ya Firdausi akiwa amezungukwa na malaika kibao.
Sauti yake ilibadilika na kuwa ndogo, macho yake yakabonyea na kuingia ndani na kuwa madogo kama ya Mchina, akawa anapumua juu kwa juu.
Pamoja na hivyo, akahisi kama vile alikuwa akitaka kukata roho. Kabla ya kufikia hatua hiyo alijihisi kama alikuwa akiishiwa nguvu, kisha akahisi kama alikuwa akitaka kuzimia.
Maskini Queen hakuwahi kushuhudia kile alichokuwa akikishuhudia kwa wakati huo, raha zilikuwa zimemzidia, ilikuwa ni mara yake ya kwanza kufanyiwa alichokuwa akifanyiwa, akachanganyikiwa mara elfu moja.
Wazimu ukampanda, akawa anajikuta anaingiza mipira golini kwake mfululizo bila ya kutegemea, akahisi raha kupita kiasi, raha ambazo kamwe hakuweza kuzielezea ladha yake.
Kila goli alilojifunga alikuwa akipiga kelele za kushangilia.
****
Ni wakati huo ndipo Rehema alipokuwa akitoka chumbani kwake na kwenda msalani. Nyumba ilikuwa imetulia kwa ukimya huku sauti pekee zilizosikika zikiwa ni zile za watu waliokuwa wakikoroma ambazo zilitokana na watu kulala vibaya au kutokana na uchovu wa mihangaiko yao ya mchana kutwa.
Kelele nyingine zilikuwa ni zile za mlango na miguu yake wakati akitoka chumbani kwake.
Rehema alishika uelekeo wa kwenda uwani.
Alipofika kwenye mlango wa mwisho, alihisi kusikia kitu kisichokuwa cha kawaida, kitu adimu katika masikio ya watu wengi lakini akapuuza.
Kupuuza kwake kulitokana na kutoka kwenye usingizi ambao bado ulikuwa ukimwelemea, akaendelea na safari yake hadi akafika msalani lakini wakati akiwa huko akameza mate ya akili na kutafakari kile alichokuwa amekisikia.
Akajiuliza kilikuwa ni kitu gani, sauti ile ikajirudia katika akili yake, akahisi ni sauti ya msichana aliyekuwa amechanganywa na mtu anayejua mambo.
Je, Rehema atagundua kama aliyekuwa chumbani kwa Eddy ni Queen? Akigundua atafanyeje?