Majangaa mbona majangaa-31-
Pamoja na kuona michakato ya kugonga shoo ikiendelea lakini hakuweza kuwajua ni akina nani waliokuwa wakifanya vile.
Aliamini kabisa kwamba watu wale walikuwa wanaishi mle ndani akadhamiria kuwaingilia mle bafuni ili aweze kuwaumbua.
Akasogea hadi katika mlango wa bafuni, hakuwa na shaka kabisa kwamba walikuwa ni watu wawili wakila uroda kwa raha zao.
Mshawawasha kama siyo kilarularu kikaanza kumsumbua naye wazimu ukampanda kabisa, ukataka kujumuika katika gemu lile bila ya kuwajua wachezaji ni akina nani.
POROMOKA NAYO…
Mtu aliyekuwa akifuatilia sauti hizo hakuwa mwingine zaidi ya Mwamvita ambaye alikuwa amehaha kutaka kujua mahali alipokuwa Eddy kwa wakati huo.
Alichungulia chumbani kwake, akaona taa ilikuwa ikiwaka lakini hakukuwa na dalili za uwepo wake, aliporidhika akaendelea na uchunguzi wake katika chumba cha Rehema nako akaambulia patupu.
Kwa kuwa alikuwa na uhakika kwamba Eddy alikuwa amerudi akasogea hadi katika chumba cha Queen ili kuhakikisha kama alikuwemo humo.
Alipopata jibu kwamba hakuwemo, akatoka hadi uwani ambako aliingia hadi msalani ili kuhakikisha kama Eddy alikuwa huko.
Akiwa msalani ndipo alipoweza kusikia mtu akimwaga maji bafuni, hapo akaamini kwamba mwanaume huyo alikuwa akioga.
Aliporidhika akawa hataki kutoka uwani, akawa anarandaranda ili aweze kumnasa Eddy kwa kuongea naye papohapo lakini alikaa kwa muda mrefu bila ya kuona dalili ya mtu kutoka bafuni.
"Kwa nini hatoki, mbona amechukua kitambo kirefu sana," aliwaza.
Akiwa anamfikiria mwanaume huyo ndipo alianza kupatwa na wasiwasi kama kule bafuni kulikuwa na usalama wa kutosha, akasogea na ghafla akasikia sauti za watu wakiwa wanapiga shoo.
Hakuweza kuamini mara moja, akaamini kuwa labda kulikuwa na mtu ambaye alikuwa akijichua peke yake lakini hilo lililkuwa gumu kuliamini kadiri alivyokuwa akisogea na kuzifuatilia sauti zilizokuwa zikitoka bafuni.
Akaamini kabisa kwamba kulikuwa na watu wawili, tena wenye jinsia tofauti.
***
Stimu zilikuwa zimewapanda, Eddy na Pat walikuwa katika harakati za kutafuta kilele cha mlima na kila mmoja alikuwa ameongeza spidi zake ili kuwahi kufika kwenye kilele hicho.
Kelele zao zikazidi kuongezeka, walikuwa hawana habari kama kulikuwa na mtu aliyekuwa akikaribia kuwaharibia zoezi lao hilo.
***
Ndipo Mwamvita alipoanza kunyata na kuzifuata kelele hizo ili aweze kubaini kama kweli zilikuwa zikitoka bafuni mle.
Akaufikia mlango wa bafu. Jinsi ya kuufungua mlango wa bafuni kwa mtu aliyekuwa akiujua vyema haikuwa ngumu hata kama mtu huyo alikuwa nje ya bafu hilo.
Ilikuwa ni kazi rahisi sana kwa Mwamvita, kwa kuwa bafu hilo halikuwa limeezekwa kwa juu, hivyo aliingiza mkono wake usawa wa mlango na kuupachua msumari uliokuwa umeuzuia mlango.
Kwa kuwa alikuwa ni mzoefu wa bafu hilo, alijua sehemu ya msumari huo ulipokuwa, hivyo akaupachua na kisha kujitoma ndani.
Alipoingia tu, aliwaona Eddy na Pat wakiwa katika raha zao, kwa msaada wa mwangaza wa mbalamwezi iliyokuwa ikiwaka wakati huo.
Hamadi! Eddy na Pat walishtuka mtu akiingia bafuni humo wakati wakiwa katikati ya starehe.
Mwamvita hakusema kitu alibaki akiwaangalia wawili hao kwa muda huku nao wakisitisha kile walichokuwa wakikifanya.
"Ahiii jamaniiii…" alisema Mwamvita katika hali ya kupagawa na kutawaliwa na kilaruralu.
Pat alijibaraguza na kumwangalia Mwamvita, akawa anajiweka sawa huku uso wake ukionekana kusawajika kwa aibu kutokana na kufanyiwa fumanizi lisilotarajiwa.
"Mnafanya nini huku?" Mwamvita alizungumza kwa sauti ndogo akijifanya kama vile hakuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea.
Hakuna aliyempa jibu, wote walikuwa kimya wakiangaliana kwa staili ya kila mmoja akimtaka mwenzake ndiye azungumze kile walichokuwa wakikifanya.
Kwa upande wake, Eddy alichanganyikiwa zaidi akaona bwawa limeshaingia ruba, akahisi aibu kwa vile alijua tukio lile lingezua gumzo lingine katika nyumba ile.
Akakumbuka makubaliano yake na Queen kwamba asishiriki tendo la ngono na mwanamke mwingine ndani ya nyumba, akajisikia vibaya kwa kuwa safari hii stori itakuwa kubwa kwa kuwa amenaswa bafuni.
"Mnafanya nini?" Mwamvita alirudia kuuliza huku akiwasogelea na kuwaangalia kwa zamu.
Hofu kubwa haikuwa kwa kuwa wamekutwa wakifanya tendo hilo tu lakini kukutwa na mtoto wa mwenye nyumba ilikuwa ni soo kubwa zaidi.
"Mi nilikuwa naogaa… ndiyo…… Eddy akaingia…" aliongopa Pat kwa aibu huku akitaka kutafuta nguo zake ili aweze kujistiri.
"Hapana … haikuwa hivyo…," Eddy naye alisema.
"Sikieni, sitaki kusikia utetezi wenu, nataka muendelee kufanya kile mlichokuwa mkikifanya la sivyo nitawajazia watu…" Mwamvita aliwapiga mkwara na kumzuia Pat kuvaa nguo zake.
Eddy na Pat waliangaliana tena na kuona kwamba itakuwa ni vigumu kuendelea na zoezi hilo mbele ya mtu mwingine ambaye hakuwepo wakati walipokuwa wakianza kupiga shoo yao.
Mwamvita alishayasoma mawazo yao na kukazia wazo lake la kuwataka wawili hao waendelee pale walipoishia.
"Itakuwa vigumu…" alisema Eddy.
"Hakuna ugumu wowote… sasa hivi nawataka muendelee na miye nitakuwa mwamuzi wa pambano lenu ninawahakikishia kwamba sitamwambia mtu," alisema.
"Haya…" Pat alikubali.
"Tafadhali sitaki ujanja wowote na kama mtashindwa kufanya hivyo, nitapiga kelele na kuwaita watu…" Mwamvita alizidi kuwatisha.
Eddy na Pat hawakuwa na ujanja, ikawabidi kurudia kile walichokuwa wakikifanya awali ingawaje hawakuwa katika hisia zilezile za mwanzo.
Wazimu wao ulikuwa umeshakatika, hawakuwa na wazimu kama ule wa mwanzo kabisa, ikawabidi wafanya ili mradi kama alivyokuwa akitaka Mwamvita.
Wakajaribu kurudia mtindo uleule, lakini nyoka wa Eddy aligoma kabisa, hakuwa na nguvu, alikuwa ameshalala doro na kukosa nguvu yake.
Mwamvita akawataka waaanzie kwa kupashana miili yao moto ili kuweza kuvuta msisimko upya kwa shingo upande wakafanya hivyo.
Bado, nyoka wa Eddy hakuwa na nguvu, ndipo msichana huyo aliyekuwa amesimama kando yao akachukua jukumu la kumsaidia Pat ili aweze kufanikiwa kumshtua Eddy aweze kurudi sawasawa.
Mwamvita aliishika ‘maiki' ya Eddy na kuanza kurap kama mwimbaji wa nyimbo za kufokafoka. Kwa mbali hisia za Eddy zikaanza kurejea.
Nyoka wake akaanza kusisimka na kurudia katika hali yake ya kawaida baada ya hofu kumtoka akilini mwake, akaona kuwa mtu aliyewakuta wakiduu alikuwa upande wao.
Hata Pat, akarejea katika hali ya kawaida, akamwomba Mwamvita ampishe ili aendelee kutoka pale alipoishia, ndipo walipoweza kufanya kile walichokuwa wakikifanya mwanzo huku Mwamvita akishuhudia.
Nini kiliendelea? Usikose kufuatilia Alkhamisi ijayo.............