Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Ni Long story Ndugu yangu lakin kwa ufupi baada ya jaribio la Mapinduzi kushindwa 1983 Baadhi ya Watuhumiwa walitoroshwa Gerezani Ukonga na kupelekwa Kenya Kupitia Mpaka wa Horohoro na lilitumika Gari la Kubebea Mkaa kuwabeba kina Kapten Maganga

Mwl Baada ya kugundua Mpango huo ndipo akatengeneza Revenge

Baada ya Arap Moi kutikiswa ikabidi wafanye Mazungumzo na Mwl Nyerere na wakakubaliana wabadilishane Wale Wahaini ndipo kina Maganga wakadanganywa na Utawala wa Kenya kuwa wanawapeleka kuwaficha Ethiopia kwa kuwa kuna Vijana wa Nyerere Wapo mitaa ya Nairobi wanaweza kuwadaka Kumbe ni Mpango wa kwenda kuwakabidhi Dodoma si Dsm
Nyerere nae aka swap kwa kukabidhi Wahaini feki kwa Moi wakat huo tayari kina Odinga ( Wahaini halisi ) wameenda kufichwa Canada Kama wakimbiziwa Kisiasa kishawasafirisha, Moi baada ya kugundua alipoteza kabisa Interest na Tanzania na Mwl kabisa kwa kuingizwa Chaka

Tanzania haitokuja kupata Rais Mwenye akili Nyingi sana Kama Julius Kambarage Nyerere never never!
ni KWELI kabisa mwalimu alikuwa habari ingine..kwa sasa tuimbee Tz amani tu ila..
 
kwahiyo mkuu inamaana kwamba intelijensia ya wale waliohudhuria kuapishwa kwa rais kule kenya ilikua dhaifu kwa kushindwa kubaini yaliyotokea kipindi cha uchaguzi kenya?
aliapishwa lini huyo Rais wa KENYA?
 
Alifukuzwa na Mwalimu Nyerere kwenye Ukurugenzi wa Usalama wa Taifa kwa kosa la Kununua Mercedez Benz bila ya kumjulisha Mwalimu

Akaja Tena kupoteza Uwaziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala bora wa Mzee Benjamin Mkapa kwa kosa la kughushi Malipo ya Matibabu ya Mkewe Nchini Marekani

Alipoongea na Media nyumban kwake Upanga alikanusha tuhuma za kughushi akamtaja PM wa wakati huo ambae kwa sasa ni Mwenyekt wa Chama Fulani kanda ya Pwani kuwa ndie anamchafua kwa kuwa wote wanautaka Urais japo mwishowe wote wakaukosa

kwa hiyo huyo PM, alikuwa Sumaye du kumbe naye ni mzee wa fitna toka kitambo tu, sasa leo analia lia nini, hajui kuwa muosha naye huoshwa ha ha haaaa
 
Mahiga hajawahi kuwa mkuu wa usalama wa taifa, ila aliwahi kuwa mkuu wa usalama wa Rais ikulu

Mkuu hiko Cheo cha ' Mkuu wa Usalama wa Rais Ikulu ' kilikuwepo Tanzania hii hii au? Kwakuwa Wewe unaonekana ni ' Mbobezi ' sana wa haya masuala ya ' Ujasusi ' Mkuu naomba unipe tofauti kati ya Mkurugenzi Mkuu wa TISS / Usalama wa Taifa na Mkuu wa Usalama wa Rais Ikulu. Nitashukuru ukinijibu ' fasta ' sasa hivi ili utumalizie ' Ubishi ' wetu hapa Kijiweni.
 
Wewe mwana eagle unawauliza waathirika wa bomoabomoa,vipi mjomba.

Habeeb Marhan
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Back
Top Bottom