Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Thank you umenigusa sana baada ya kutambua utulivu mkubwa alionao Mzee Mahiga.Kwa mtazamo wangu waziri mahiga ni miongoni mwa mawaziri wachache wenye nidhamu ya hali ya juu na watiifu wa dhati kwa rais wetu.Ameshika nafasi kubwa za kuaminika kimataifa kakini bado anaitumikia nafasi yake ya uwaziri bila majivuno.Huyu ni mfano wa kuigwa na lazima tujivunie kwamba Rais bado ana mawaziri wazuri wakiwemo akina Hussein Mwinyi na Prof. Mubarawa.Kwa kumalizia lille tukio la mke wa Mahiga na yaliyofuatia baada ya pale yangeweza kuleta mtikisiko kwake lakini alitulia kama siyo yeye.
Hawa wazee walifundwa na wakafundika. Sio hawa unawachukua UVCCM tena sio UVCCM yakina Lukuvi, Kikwete nk. Hawana busara za uongozi, akishakuwa kiongozi, lugha za staha kwa watu wanazikosa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alex Furgeson alisifiwa sana akiwa Manchester japo hakuwa anacheza na Wenger analaumiwa sana Arsenal japokuwa Yeye sio Mchezaji nadhan utakuwa umeelewa kwanini Namsifia Mwl Nyerere kwa kuwa Yeye ndio Kiongozi Mkuu aliekuwa anateua Hao unaowataka niwasifie

Labda hujui tu kuwa Mipango Mikubwa yote huwa lazima ipate baraka za Rais kabla ya kutekelezwa na ikitokea Rais ni Fwalaaaa anaweza akaropoka hadharan Kama Fulani alivyoropoka kuhusu Suala la Kibiti na kudukuliwa kwa simu ya Mwanasiasa aliekuwa anafuatiliwa na Usalama kuhusu kuwasiliana na Acacia

Rais Nyerere lazima tumsifu alipokuwa kafanya vizuri Kama ninavyomkosoa anapokuwa alikosea ndio u Great thinker
Ile ya "kudukua sim ya Lisu ni UFWALA WA MUHULA"
Mshkaji hana KIFUA

May Allah bless Me and You
 
Thank you umenigusa sana baada ya kutambua utulivu mkubwa alionao Mzee Mahiga.Kwa mtazamo wangu waziri mahiga ni miongoni mwa mawaziri wachache wenye nidhamu ya hali ya juu na watiifu wa dhati kwa rais wetu.Ameshika nafasi kubwa za kuaminika kimataifa kakini bado anaitumikia nafasi yake ya uwaziri bila majivuno.Huyu ni mfano wa kuigwa na lazima tujivunie kwamba Rais bado ana mawaziri wazuri wakiwemo akina Hussein Mwinyi na Prof. Mubarawa.Kwa kumalizia lille tukio la mke wa Mahiga na yaliyofuatia baada ya pale yangeweza kuleta mtikisiko kwake lakini alitulia kama siyo yeye.
Yeye yuko vizur.
Je bos wake?

May Allah bless Me and You
 
Ni Kweli kabisa na Hata Afande Kimario Mwenyewe alitumia Hati ya kusafiria ya Ghana sio Tanzania

Wale Jamaa haitokuja tokea Sytem strong Kama ile, iliyotibua Mapinduzi na Uhaini Mara 8 ikiwemo kumsaidia Raila Odinga kumtikisa Daniel Arapa Moi 1983 na jaribio liliposhindwa wakamtorosha Raila mpaka Canada Ikiwa ni revenge kwa Kenya kusaidia Uhain wa kina Kapten Maganga na Akina Maghee Upande wa Tz

Kipindi hicho Tanzania ilikuwa Israel ya Maziwa Makuu na Africa Mashariki kwa jumla sio hii ya Leo Kibiti inatutoa jasho
Sasa hivi Rwanda ndio mbabe Wa maziwa makuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huenda Mpaka sasa Tanzania haijapata Mtaalam wa kudungua ( Sniper) wa kiwango cha Mahiga

Kuna Mzee Mmoja Mstaafu wa pale Makumbusho aliwahi kuniambia Mahiga alijifunzia Yugoslavia ya Kijamaa 1970s Makitu kiasi kwamba kWenye Mazoezi Yao walikuwa wanapanda Magari mawili tofauti yanayoenda kwa kasi kwa uelekeo tofauti lakin Balozi alikuwa na uwezo wa kumdungua anaemtaka ndani ya Gari tofauti!
Story za form two unatuletea watu wazima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Story za form two unatuletea watu wazima

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio stori za form two, tatizo kuna watu ukiambiwa uwezo wao akili yako lazima ikatae!

Ukisikia mtu ni jasusi basi tambua kuwa jasusi anao uwezo mkubwa kuliko mwanajeshi na siku zote kazi za ujasusi duniani kote wanafanya watu wenye akili sio ya kawaida na uwezo wa hali ya juu.


Unaweza kushangaa lakini ndio hivyo . Mtu ukisikia ni jasusi wa usalama wa taifa basi muogope!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mahiga hajawahi kuwa mkuu wa usalama wa taifa, ila aliwahi kuwa mkuu wa usalama wa Rais ikulu
Dk Mahiga alipata ufadhili na kuendelea na masomo ya juu nchini Canada katika Chuo Kikuu cha Toronto ambako alihitimu Shahada ya Uzamili. Aliendelea na masomo ya Shahada ya Uzamivu (PhD) katika chuo hichohicho akijikita katika Uhusiano wa Kimataifa na kuhitimu mwaka 1975.

Mwaka huohuo 1975 (akiwa na miaka 30), Dk Mahiga alirejea nchini akiwa daktari wa falsafa kitaaluma na alipangiwa kazi ya kufundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwa mhadhiri katika Idara ya Kimataifa na Ushirikiano wa Kikanda. Alifanya kazi hiyo hadi mwaka 1977 alipohamishiwa katika Ofisi ya Rais kuwa Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo na alidumu hapo akifanya kazi pamoja na Mwalimu Julius Nyerere hadi mwaka 1980.

Kati ya mwaka 1980 hadi 1983, Dk Mahiga alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa. Nafasi hii aliitumikia kwa weledi mkubwa katika historia ya watu waliowahi kuitumikia, aliweza kuifahamu nchi vizuri na mifumo yake kwa mtizamo wa ndani na nje.
 
Sio stori za form two, tatizo kuna watu ukiambiwa uwezo wao akili yako lazima ikatae!

Ukisikia mtu ni jasusi basi tambua kuwa jasusi anao uwezo mkubwa kuliko mwanajeshi na siku zote kazi za ujasusi duniani kote wanafanya watu wenye akili sio ya kawaida na uwezo wa hali ya juu.


Unaweza kushangaa lakini ndio hivyo . Mtu ukisikia ni jasusi wa usalama wa taifa basi muogope!

Sent using Jamii Forums mobile app
Eti Jasusi,my foot

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom