Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Matusi ya nini Ndugu,

huu ni Mjadala wa jumla kuna Vitu tunawaeleza Juniors na kuna Vitu tunapata kutoka kwa Wataalam,

kufoji kwake vyeti vya Matibabu ya Mkewe hakufanyi tusijifunze na kutambua role ya Usalama wa Taifa kumdhoofisha Iddi Amin Kabla ya Vita,

Sifa zote za Ushindi wa Vita vya Kagera huwa tunampa General Twalipo na Makamanda wengine na kusahau role ya Usalama wa Taifa chini ya Dkt Hassy Kitine,

Kama kosa la Mtu linaharamisha kusifiwa kwa Mengine Mazuri aliyofanya Basi Hakuna Binadamu anaepaswa kusifiwa kwa kuwa Hakuna Mkamilifu
Pohamba inaonekana unajua mengi sana.

Napenda kujua usalama wali mdhoofisha vipi Idd amin kabla ya vita

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msimsahau pia mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja tena kwa herufi moja M
Huyu jamaa watu wa miaka ya 64 watamkumbuka vizuri saaana, mtu pekee ambaye hakujulikana wala kuonekana katika muonekano wa kawaida na mtu pekee alie wachagua akina Hassy kipindi hicho. Na aliaminika mnooo na mzee nyerere, mambo yake yalikuwa zaidi ya tunavomjua wengine

Hata hivyo ndie aliekuwa ansaidia kutoa taarifa kutoka kila mahari na kuzifikisha mahali husika kisha vijana kama akina hassy wanazifanyia kazi.

Wengi walimuita masikio ya tembo kwa uwezo wake wa kupata udaku na habari nyeti.
Kila wenzie wakileta habari kwake yeye ilikuwa kama mechi ya marudio iliyochezwa jana.

Cha kushangaza baadae alikuja kutofautiana na wenzake mwaka 86 akidai anataka kupumzika
Nani huyo MKUU
Umetuacha kwenye mataa ya chato
 
Pohamba,

..Mzee Kitine alipata kuelezea kuhusu nini haswa kilitokea ktk "kashfa" anayotuhumiwa kununua benzi.

..kwa ujumla alieleza kwamba Mwalimu hakumtimua ktk nafasi ya mkurugenzi mkuu wa tiss.

..Maelezo ya Kitine yapo ktk mahojiano aliyofanya na gazeti la raia mwema.
 
Mahiga ukimuona juuu juu unaweza kumchukulia kama wanasiasa wengine ila ukifuatilia historia yake unachoka tu. Mzee katulia sana huyu.

Lile tukio la mkewe lilipotokea, alitulia tu. Wangekuwa wanasiasa wengine wa kisasa, wangeanza kutweet mipasho. Vijana tujifunze kwa hawa wazee.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ana busara sana mzee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni Kweli hata Mimi nahisia Kama zako

Mgawanyiko wa CCM Kama Lowassa angebaki CCM ni Mkubwa kuliko alivyohama!, huenda Akina Gwajima walitumika kumsaidia Mzee kuhama bila ya wao kujijua ili CCM iweze kujiandaa vyema na Uchaguzi bila ya kitisho kikubwa cha usaliti tokea ndani

Unadhani Edward Snowden "ameiasi" kweli U.S.A au bado yuko kazini. Nadahani nitavumiliwa na wengina kuuliza swali hili kwenye uzi huu.
CC: Matola et all.https://www.google.com/url?sa=t&rct...nowden&usg=AFQjCNGL4Pz33By1CJC15mULy7PmUlotlA
 
Pleaseee majina ya Mkwere ya Mfukoni ndio Ya usalama wa Taifa
Mi najua/kwa uelewa wangu mdogo Usalama wa Taifa upo kwenye kila nyanja
Uchumi
Utawala bora
Usalama wa mipaka na Ndani pia
BUT kama unaniambia TISS waliona kwa huyu jamàa ambae anavunja katiba daily kuna kitu bora mihimili ya bunge na Mahakama iko uchi ambacho waliona ni tofauti na wengine 4 waliopita walipoiacha hii mihimili atleast iwe hurru walikuwa wapumbavu basi ntashindwa kuwaamini hao Zege la Chips kama unavyowaita.
Ukivunja sheria/katiba jua unaleta uonevu ukileta uonevu jua unahatarisha Usalama wa Taifa.....Labda kuna mbingu hao TISS waliiona kwa huyu jamaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu,dhana ya usalama wa Taifa ni dhana pana sana.Unayoyaona mabaya,kumbe ndivyo yalivyo pangwa yatokee hivyo hivyo,kwa maslahi mapana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sifahamu kabila lake japo nadhan aliwahi kuwa Mbunge wa Makete Kama sijakosea Ila Historia yake inanivutia sana!

Alianza kwa kuwa Mwalimu wa Secondari kule Bukoba baada ya kumaliza Chuo Kikuu

Baadae ikaamriwa wote ambao hawakupita JKT waende Hata Kama Wapo kazini
Hassy akajaribu na wenzie kukwepa Mafunzo ikashindikana mwishowe wakasalim Amri wakaenda na Yeye akapangwa Songea

Baada ya kumaliza Mafunzo ambayo walikuwa hawayapendi kuanzia wanatoka Makazini mpaka wakat wa Mafunzo Hassy akajikuta Miongoni Mwa wanaochaguliwa kubaki kuendelea na JKT rasmi wakat tayari akili yake ilianza kufurahia kurudi kazini na kuanzia hapo ndipo akaanza kuandaliwa na mpaka kufikia Cheo hicho kikubwa cha Ukuu wa Usalama wa Taifa

Mwalimu Nyerere kwny Masuala ya Usalama wa Taifa alikuwa sio Mtu wa Mchezo Mchezo

Aliwahi kupeleka Maafisa 15 Nchini Israel depo la Kina Bregadier Muhidin Kimario kujifunza Mambo ya Usalama bila ya wao wenyewe kujuana kwa kuwa walionekana wana tokea Mataifa ya Nje kwa kuwa Uhusiano wa Isarel na Tanzania haukuwa Mzuri, alitumia hati za kusafiri a za Mataifa Rafiki yenye uhusiano Mzuri na Isarel
[emoji1] [emoji1] duh!! Mwalimu alikuwa kiboko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mr X alisema walijaribu kumkamata lakini akawatoroka kwa kuruka ukuta wa nyumba aliyokuwa akiishi.

Akasema wakati wakimkimbiza Komandoo Tamim alidandia gari moja pick-up iliyokuwa imebeba masanduku ya bia na kuanza kuwarushia risasi wana usalama waliokuwa wakimkimbiza, hivyo akapigwa risasi na kufa.

wapi Mabere Nyaucho Marando..
 
Nime jifunza mengi
Acha tu mkuu, Hapa unganisha doti mwenyewe...

Yaani walioanzisha upinzani nchini ni akina mabere, apson wazee wa system, na mwenzao mzee wa kiraracha ambaye naye anadai alikua mtu wa system, na hawa watu huwa hawastaafu.. Wanapunzika tu..kama anavysema Pohamba

Yaani tunachezeshwa ngoma, mpigaji ni yule yule ila anatubadilishia midundo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom