Mbona CHADEMA mnalalamikia zoezi la usafi wakati RC Chalamila hajalaumu maandamano yenu?

Kindeena

JF-Expert Member
Sep 27, 2017
9,061
15,799
CHADEMA kupitia Mwenyekiti Mbowe wametangaza kufanyika maandamano Dar es Salaam, January 24, 2024.

Lakini pia RC wa Dar es Salaam Bwana Chalamila Albert ametangaza Majeshi ya Ulinzi na Usalama kufanya usafi mkoani kwake tarehe 23-24 January 2024.

CHADEMA kila kona mitandaoni wanamlaumu RC Chalamila kwa tangazo lake la usafi.

Swali langu ni kwamba, kwani CHADEMA wakiandamana na majeshi yakifanya usafi, shida ipo wapi?

Mbona Chalamila hajawalalamikia CHADEMA kutangaza maandamano ila CHADEMA wanamlalamikia Chalamila kufanyia usafi Mkoa wake kwa msaada wa jeshi?

Pale Soko la Mabibo, Chalamila aliwahi kuwapeleka wanajeshi wakafanya usafi huku biashara zikiendelea bila bugudha wala mikwaruzano.

Kwa hiyo CHADEMA ninadhani waandamane tu wasiogope, ila ninahisi wakifanya fujo zoezi la usafi litasitishwa kwa muda.
 
CHADEMA kupitia Mwenyekiti Mbowe wametangaza kufanyika maandamano Dar es Salaam, January 24, 2024.

Lakini pia RC wa Dar es Salaam Bwana Chalamila Albert ametangaza Majeshi ya Ulinzi na Usalama kufanya usafi mkoani kwake tarehe 23-24 January 2024.

CHADEMA kila kona mitandaoni wanamlaumu RC Chalamila kwa tangazo lake la usafi.

Swali langu ni kwamba, kwani CHADEMA wakiandamana na majeshi yakifanya usafi, shida ipo wapi?

Mbona Chalamila hajawalalamikia CHADEMA kutangaza maandamano ila CHADEMA wanamlalamikia Chalamila kufanyia usafi Mkoa wake kwa msaada wa jeshi?

Pale Soko la Mabibo, Chalamila aliwahi kuwapeleka wanajeshi wakafanya usafi huku biashara zikiendelea bila bugudha wala mikwaruzano.

Kwa hiyo CHADEMA ninadhani waandamane tu wasiogope, ila ninahisi wakifanya fujo zoezi la usafi litasitishwa kwa muda.
Wenye akili wanajua dhamira ya Chalamila, wewe chawa huwezi kuyaona ya ndani kutoka higher mental faculties
 
Wenye akili wanajua dhamira ya Chalamila, wewe chawa huwezi kuyaona ya ndani kutoka higher mental faculties
Dhamira yake ni kuwatia hofu na hiyo ni kutokana inajulikana kuwa wabongo sio waandamanaji ni waoga kuandamana, jeshi halipo kwa ajiri ya kuzuia maandamano sasa kama kweli mmekusudia kuandamana kwa maandamano ya amani iweje kulalamika jeshi kufanya usafi Dar siku hiyo?
 
Mi nadhani itakuwa vyema chadema wakiungana na majeshi siku hiyo kufanya usafi... nayo itakuwa ni protest pia yenye nguvu sana..
 
_42dd6c81-3205-4734-9034-3644652d0624.jpeg
 
Back
Top Bottom