Mbeya: Watoto zaidi ya 3,000 wapewa Elimu ya Ukatili wa Kijinsia, utoaji wa taarifa za uhalifu na matumizi ya barabara

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
efa66c23-4244-4da8-8fa7-27f8014aeb18.jpeg
Askofu Mkuu Jimbo Kuu la Mbeya Mhashamu Gervas Nyaisonga ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania akiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Benjamin Kuzaga katika kilele cha Kongamano la Utoto Mtakatifu Jimbo la Mbeya lililofanyika Kanisa la Hija Parokia ya Mwanjelwa Jijini Mbeya Desemba 28, 2024.

Kongamano hilo la siku tatu limeshirikisha Watoto zaidi ya 3000 kutoka Parokia zote za Jimbo Kuu la Mbeya likiwa na lengo la kuwajenga katika maadili ya dini na kuwajengea uwezo wa kutambua haki zao, kujitambua na kujilinda dhidi ya vitendo viovu.

Aidha, katika kongamano hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kupitia Dawati la Jinsia na Watoto na Kikosi cha usalama barabarani kitengo cha elimu kwa umma lilipata nafasi ya kutoa elimu ya ukatili wa kijinsia, utoaji wa taarifa za uhalifu na wahalifu na elimu ya matumizi sahihi ya barabara.
ee55e5ff-a2f8-49c7-a478-ff1bfd2743aa.jpeg

cc31147a-33ae-4169-b12b-03c9d66edc99.jpeg
 
Back
Top Bottom