Mbeya long time kitambo

Mbeya long time kitambo

Mimi naikumbuka Mbeya ya 1975/1977. Reli ya Tazara inazinduliwa 1976 tulipanda train iliyotoka Kapiri Mposhi tukashuka Makambako tukarudi Mbeya kwa gari VW combi. Nilikuwa na viwanja vya golf kabla ya kugeuzwa matumizi ili ujengwe uwanja mkubwa wa michezo. Tulishiriki katika Ujenzi wa Uwanja wa Mapinduzi ( Sokoine) tukitokea Majengo primary school tukishirikiana na wanafunzi wa Sisimba, Mbaya, Azimio hiyo ilikuwa 1976 etc. Mwalimu Mkuu Malengo alikuwa Mwl Mwangomile na Mbaya alikuwa Mwakang'ata.
Nakumbuka kulikuwa na kikundi cha Sanaa kilichoitwa Chamnambe kikiongozwa na Mzee Ryoba. Kulikuwa na shule inaitwa Muungano ilikuwa msituni njia ya Mwanjelwa sijui kama bado ipo. Pia nakumbuka Pareto ya uyole. Those old good days.

Pia nakumbuka 1976 ilitokea ajali kubwa ya basi likiitwa Mwambipile Bus Service ilipinduka huko Mwakaleli ikaua watu wengi sana.
Sijafika Mbeya Tangu Dec. 1977, nasikia imebadilika mno.
Mkuu karibu sana jijini mbeya imebadirika
 
ha ha haaa Kifwamba Rangers .....ilikuwa timu ya tajiri mmoja mnene enzi hizo.....mara moja moja alikuwa akipewa namba tisa aingie kupiga soka .....ilikuwa vituko....nasikia alikufa huyo mwenye kifwamba
Mzee alikuwa kituko sana,ukienda kuomba usajiliwe katika timu yake ukisema unacheza namba tisa biashara imekukata.
 
Ally ni dereva wa mabasi ya mikoani maarufu kama "mwansyu"
 
Kawaida Auto garage walipendezesha sana Mei Mosi kwa magari yao ya ajabu
 
Bujibuji umenikumbusha mbali sana Mkuu umesahau FAT ya isanga ilikua inatengeneza Tiketi feki za uwanjani na Disco nakumbuka kuna siku walitengeneza tiketi za Disco livingstone ikaonekana watu wengi kuliko mauzo ya tiketi zao ikabidi tutolewe wote disco jamaa yule baunsa akawa akimtambua wa isanga,docks au Nonde hata kama ulilipa tiketi harali haurudi ndani..Kambosonic nilimuona mara ya mwisho Cape Town 2003,Rossebank katulia sana huyo Simply nasikia alikua Jozi sijapata kumuona karibuni..isanga kulikua na Brigedia Mwakayugu na ATU JANDE kwa sasa marehemu..maisha ya kibabe utadhani soweto ya south sasa hivi..
Mh...peter kihaka
 
Hivi yule msanii DDG yupo kweli sikuhiz, alikua anachana enzi hizooo miaka ya 2000
 
e3f31d98312ac6ec8ffce54f8d685024.jpg
 
Hivi pale town uhindini naskia soko liliungua sijui watu wakahama? Is it true
 
Samahan mkuu mTC ndo nn
mbeya technical college,chuo kilikuwa kule iyunga kiwanda cha koka kwa juu,jamaa walikuwa wakali sana wa basketball..walikuwa wana uwanja wa mbao wa ndani-indoor marble court
 
Back
Top Bottom