Mimi naikumbuka Mbeya ya 1975/1977. Reli ya Tazara inazinduliwa 1976 tulipanda train iliyotoka Kapiri Mposhi tukashuka Makambako tukarudi Mbeya kwa gari VW combi. Nilikuwa na viwanja vya golf kabla ya kugeuzwa matumizi ili ujengwe uwanja mkubwa wa michezo. Tulishiriki katika Ujenzi wa Uwanja wa Mapinduzi ( Sokoine) tukitokea Majengo primary school tukishirikiana na wanafunzi wa Sisimba, Mbaya, Azimio hiyo ilikuwa 1976 etc. Mwalimu Mkuu Malengo alikuwa Mwl Mwangomile na Mbaya alikuwa Mwakang'ata.
Nakumbuka kulikuwa na kikundi cha Sanaa kilichoitwa Chamnambe kikiongozwa na Mzee Ryoba. Kulikuwa na shule inaitwa Muungano ilikuwa msituni njia ya Mwanjelwa sijui kama bado ipo. Pia nakumbuka Pareto ya uyole. Those old good days.
Pia nakumbuka 1976 ilitokea ajali kubwa ya basi likiitwa Mwambipile Bus Service ilipinduka huko Mwakaleli ikaua watu wengi sana.
Sijafika Mbeya Tangu Dec. 1977, nasikia imebadilika mno.