Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa...

Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa...

Hongera, sana ndg yangu Mbatia ww ndiyo kiongozi,maana kiongozi huongoza kwa vitendo ila mwanasiasa yeye ni kusema tu.Hongera sana Mh Mbatia.

Utafikiria aliye-comment hapa ni kilaza JK mwenyewe
 
Bado nashindwa kuelewa. Jengo la ghorofa 10 zinapandishwa mpaka 16 bila mamlaka yoyote kushtuka, tena katikati ya jiji, wote walihongwa? Hii ni kielelezo cha serikali iliyokubuhu kwa rushwa katika ngazi zote.
 
Wewe una beef binafsi na Meya kwa sababu ya mafanikio yake makubwa ya hivi karibuni. Watu kama nyinyi kwenye jamii hamkosekani...
Mafanikio yake makubwa ndio haya ya kuanguka hili jengo na kuua watu? Jibu hoja hapa, "alikuwa anasubiri report toka mwezi wa 10 mpaka jana", hiyo report ilikuwa Nachingwea ikakosa usafiri? Kama Baba yako angekuwa miongoni mwa waliokufa au kujeruhiwa vibaya, ungekubari hoja hii ya kijinga toka kwa Meya? Acheni utamaduni wa kutukuza watu wengine wanaumia kwa uzembee wao
 
Ndugu wana JF na watanzania nimefuatilia misiba mikubwa km kuzama kwa meli. Pia sijona chama cha CHADEMA; Kipindi cha uokozi ; ushauri wangu CHADEMA tuma mwakilishi katika jengo lilioanguka posta ili imani ya wapenzi wa chama iongezeke;

Mbowe na slaa onyesha mfano kama Mbatia kipindi cha uokoz
 
CHADEMA Sio sela yao kwenda kuuza Sura, Niambie hao waiofika hapo wamesaidia nini? CCM ndo wanatakiwa kuwajibika moja kwa moja make niliwonawale wadindi wakilalamika waliwahi kutoa malalamiko Mara mbili ya kuzia jendo lisiendelee kujengwa lakini hakuna walicho fanikiwa,

Ufisi wa CCM ndo unafikisha nchi hapa tulipo, hao wakina Lipumba ni kuuza Sura tu hapo, inachekesha eti Raisi a Nchi amezuru eneo mara mbili, kusaidia nini?
 
unanikumbusha ule usemi wa mchawi ndiye hulia sana msibani.Teh,teh,tehhh
 
Kwako wewe kuanguka kwa gorofa kwa sababu ya uzembe wa serikali ya magamba ndo unataka viongozi wa chadema wawepo?ina maana kwako huo ndio uzalendo zaidi ya kazi ya elimu ya uraia wanayoifanya?Wewe ni mmojawapo ya wanaotakiwa kukamatwa na kushtakiwa kwa mauaji hayo yaliyosababishwa na magamba wenzako kwa rushwa walizopokea.
 
Sijui nisemeje kwani yote haya yametufika kwa sababu ya kukosa maadili (ethics). Kama magazeti yalivyoandika jengo lilikuwa liwe la ghorofa kumi aliyeruhusu ghorofa kumi na sita ni nani? Manispaa wamekanusha kuhusika sasa ni nani mwenye mamlaka zaidi ya manispaa? Sasa jambo limeshatokea je serikali si ina kitengo cha maafa? Kimejipangaje ktk shughuli kama hii? Kusema mbatia kajitolea haina mshiko kwani hata rais kufika ktk eneo la tukio ni mchango muhimu na wale wote waliosaidia uokoaji wote ni wa kuwapa pongezi kwani walikuwa ktk mazingira hatarishi. Ktk jambo kama hili tuweke siasa pembeni tupambane na wenye taaluma ktk fani ya ujenzi lengo likiwa matukio kama haya yanazuilika kabisa kama wataalamu watafuata maadili.
 
Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi mh. James Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa katika kusaidia shughuli ya uokoaji wa waathirika wa jengo lililoanguka jijini Dar es Salaam tarehe 29.32013. Hayo yameelezwa na walioshuhudia jinsi kiongozi huyo wa upinzani alivyokuwa hodari katika kutumia ujuzi wake kulinufaisha taifa katika janga hili.

Hatua hii ni tofauti na mwenyeti wa chadema Freeman Mbowe ambaye alichokifanya ni kwenda kwenye mitandao ya kijamii kulifanyia kejeli janga hili kubwa kwa taifa.

Kamera za waandishi wa habari zilifanikiwa kupata picha kadhaa za jinsi mh. Mbatia alivyoonyesha umuhimu wa kuweka siasa pembeni katika majanga na kutoa kipaumbele kwenye kuisaidia jamii kuwa salama kwanza.

Hongera mh. Mbatia, hongera NCCR kwa kuwa na mwenyekiti shupavu.


View attachment 88608
Mh. Mbatia akitoa maelekezo ya hatua muhimu za kuchukua kuokoa waathirika.



View attachment 88607
Rais Kikwete akimshukuru na kumpongeza mh. Mbatia kwa mchango wake mkubwa kwenye kuokoa waathirika.



View attachment 88609
Wananchi wakimshukuru mh. Mbatia kwa msaada mkubwa alioutoa kuokoa waathirika.

Acha unafiki! uchungu wa tukio haupimwi kwa kwenda eneo la tukio kama unavyodhani ili watu wakuone kuwa upo eneo la tukio. Hivi kwa akili zako timamu na ukizingatia staili ya teknolojia inayotakiwa katika uokoaji mchango wa Mbatia katika hili zoezi unapimika? Ni shughuli gani ambayo ameifanya ambayo bila yeye kuwepo pengo lake lisingezibika?
Kwa upande mwingine umejiridhisha sababu za Mbowe kutokuwepo eneo la tukio si za msingi na ilimpasa kuja hapo kuonyesha sympathy?

Umri ndio unaenda hivyo inakupasa akili yako ikomae kadri umri wako unavyokua na hii inadhihirika pale unapopambanua mambo kiukomavu.
 
Watanzania tutaendelea kuwa wapumbavu mpaka mwisho wa hii dunia kama upo. Watu wanashauriwa namna ya kufanya mambo yawe vizuri makusudi wanapuuza sasa haya ni majanga? Ajali za meli za kujitakia? Kwani wakienda pale watasaidia nini zaidi ya kuongeza foleni ya wapuuzi wanaoshangaa?
 
Kama Mv spice baada ya kurud wakaendeleza Taarab! Majanga wanazembea wao unataka Cdm waje kutoa pole..! Wakisema ukweli kuwa n uzembe wa Maccm mtakubali?
 
Hii ajali ni matokeo ya rushwa. Wahindi wamelia sana kuelezea walivyopuuzwa na serikali. Jengo la ghorofa 10 litapandishwa vipi hadi 16 bila mamlaka yoyote kushtuka?
 
kinachotakiwa ni kuwa na vifaa vya kisasa vya uokoaji,na waokoaji wenye taaluma ya uokoaji siyo wanasiasa kwenda kushangaashangaa tu.na vilevile tuwe na mikakati ya kuzuia majanga kabla hayajatokea.
 
CDM si kama CCM, hawa jamaa wa magamba wamekaa standby kusuburi misiba na majanga ili kujionesha wanajali sana wananchi kumbe wanafiki tu!
 
Wauza sura tu hao,wangeenda kuzuia ujenzi
 
hivi huyo diwani mwenye hiyo kampuni inayojenga hilo jengo ni wa chama gani?
 
Mbona wanahani sana kwenye majanga na yanazidi kila uchao!! Wanafiki hao ma CCM ....gamba we!
 
Yaani upuuzi wa serikali ya ccm wa kutofanya ukaguzi wa majengo uigwe na chadema. Kwa kwenda kuokoa watu...

Utakuja kushauri wawe ma fastjet mda si mrefu
 
Back
Top Bottom