Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa...

Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa...

ZeMarcopolo

Platinum Member
Joined
May 11, 2008
Posts
14,279
Reaction score
7,685
Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi mh. James Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa katika kusaidia shughuli ya uokoaji wa waathirika wa jengo lililoanguka jijini Dar es Salaam tarehe 29.32013. Hayo yameelezwa na walioshuhudia jinsi kiongozi huyo wa upinzani alivyokuwa hodari katika kutumia ujuzi wake kulinufaisha taifa katika janga hili.

Hatua hii ni tofauti na mwenyeti wa chadema Freeman Mbowe ambaye alichokifanya ni kwenda kwenye mitandao ya kijamii kulifanyia kejeli janga hili kubwa kwa taifa.

Kamera za waandishi wa habari zilifanikiwa kupata picha kadhaa za jinsi mh. Mbatia alivyoonyesha umuhimu wa kuweka siasa pembeni katika majanga na kutoa kipaumbele kwenye kuisaidia jamii kuwa salama kwanza.

Hongera mh. Mbatia, hongera NCCR kwa kuwa na mwenyekiti shupavu.

attachment.php


Mh. Mbatia akitoa maelekezo ya hatua muhimu za kuchukua kuokoa waathirika.
attachment.php

Rais Kikwete akimshukuru na kumpongeza mh. Mbatia kwa mchango wake mkubwa kwenye kuokoa waathirika.
attachment.php

Wananchi wakimshukuru mh. Mbatia kwa msaada mkubwa alioutoa kuokoa waathirika

=============== michango zaidi ===============

Serena Hotel wamejitolea chakula kwa wanaosaidia shughuli ya uokoaji...
attachment.php


attachment.php

Asante sana Serena Hotel kwa kuonyesha mfano wa uzalendo kwa vitendo...
 
Mbatia amekomaa kisiasa na ndio maana kama kiongozi wa chama alifika kwenye tukio kuungana na wananchi .
Wengine wamekaa nyumbani wanasubiri kesho watoe TAMKO na kuitisha maandamano nchi nzima.
Wao ni kama kufa kufaana, yaani wengine wakipatwa na majanga wanatumia kama mtaji wa kujipatia umaarufu wa kisiasa
Viongozi wa kweli ni wale waliofika kwenye eneo la tukio, sio kurusha comments kwenye face book
When you are good , You are good! No wonder why Mheshimiwa Rais alimteua mbunge wa viti maalum, ni kwa sababu aliona kipaji cha huyu bwana
Upinzani sio kupinga kila kitu kinachofanywa na serikali, upinzani ni kuwaonyesha wananchi kuwa utawafanyia zaidi ya yanayofanywa na serikali ya sasa au kuyaboresha.
 
mbona naona anashikana mikono na waheshimiwa tu..... nilitarajia uweke picha akiwa field na mbinu alizotumia kuokoa.... hapo ningekupa LIKE kubwa balaa

Hizi picha ni baada ya kazi. Kwenye kazi alikuwa katikati ya vumbi kubwa, ilishindikana kupata picha live kutokana na angle aliyokaa mpiga picha wetu...
 
ZeMarcopolo,

..inasemekana James Mbatia alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho UDSM kitivo cha Uhandisi.

..sasa kutokana na siasa za migomo Mzee Mwinyi na CCM yake wakamfukuza shule.

..juhudi zote za kujaribu kumuombea aruhusiwe kumaliza shahada yake zikakwama.

..kwa hiyo mpaka tunavyozungumza Mbatia hajapata shahada yake ya Uhandisi wa Ujenzi.

..leo hii jengo limeporomoka yule aliyenyimwa na CCM shahada yake ya Uhandisi, ndiyo amekuwa mfano wa kusaidia majeruhi.

cc: Chris Lukosi
 
Last edited by a moderator:
Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi mh. James Mbatia ameonyesha mfano wa kuigwa katika kusaidia shughuli ya uokoaji wa waathirika wa jengo lililoanguka jijini Dar es Salaam tarehe 29.32013. Hayo yameelezwa na walioshuhudia jinsi kiongozi huyo wa upinzani alivyokuwa hodari katika kutumia ujuzi wake kulinufaisha taifa katika janga hili.

Hatua hii ni tofauti na mwenyeti wa chadema Freeman Mbowe ambaye alichokifanya ni kwenda kwenye mitandao ya kijamii kulifanyia kejeli janga hili kubwa kwa taifa.

Kamera za waandishi wa habari zilifanikiwa kupata picha kadhaa za jinsi mh. Mbatia alivyoonyesha umuhimu wa kuweka siasa pembeni katika majanga na kutoa kipaumbele kwenye kuisaidia jamii kuwa salama kwanza.

Hongera mh. Mbatia, hongera NCCR kwa kuwa na mwenyekiti shupavu.


View attachment 88608
Mh. Mbatia akitoa maelekezo ya hatua muhimu za kuchukua kuokoa waathirika.



View attachment 88607
Rais Kikwete akimshukuru na kumpongeza mh. Mbatia kwa mchango wake mkubwa kwenye kuokoa waathirika.



View attachment 88609
Wananchi wakimshukuru mh. Mbatia kwa msaada mkubwa alioutoa kuokoa waathirika.

Hata MIMI ningefanya HIVYO free SHANGINGI free PAYCHECK Free DIPLOMATIC PASSPORT; Ningeenda kwa MIGUU wa kwanza
 
ZeMarcopolo,

..inasemekana James Mbatia alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho UDSM kitivo cha Uhandisi.

..sasa kutokana na siasa za migomo Mzee Mwinyi na CCM yake wakamfukuza shule.

..juhudi zote za kujaribu kumuombea aruhusiwe kumaliza shahada yake zikakwama.

..kwa hiyo mpaka tunavyozungumza Mbatia hajapata shahada yake ya Uhandisi wa Ujenzi.

..leo hii jengo limeporomoka yule aliyenyimwa na CCM shahada yake ya Uhandisi, ndiyo amekuwa mfano wa kusaidia majeruhi.

cc: Chris Lukosi

JokaKuu,

Je unajaribu kusema kuwa wale wahandisi wote waliohitimu wamepewa fursa hiyo na CCM?
 
I think we are missing the big picture here. Mwenye jukumu la kushughulikia maafa nchini ni serikali. Yalipotokea mafuriko ya Katrina New Orleans ni serikali ya Bush ndiyo ilikuwa na dhamana ya kushughulikia maafa hayo, na ililaumiwa ipasavyo kwa kushindwa kuokoa maisha ya watu katika muda muafaka. Mafuriko yaliyotokea New York na New Jersey wiki mbili kabla ya uchaguzi wa mwaka jana Obama aliwajibika ipasavyo. Akishirikiana na gavana wa New Jersey alitoa ahadi kuwa serikali itahakikisha kuwa wahanga wanapewa msaada haraka. Hivyo ndivyo wenzetu wanavyofanya. Wanayo system in place na si kutegemea msaada wa mtu mmoja mmoja kama Mbatia na kumwona shujaa wakati system yetu ni a total failure. Hii si mara ya kwanza kwa jengo kuporomoka Dar-es- Salaam na ninaamini haitakuwa ya mwisho. Tumejifunza nini kutokana na jengo lililoanguka Chang'ombe? Nothing. Tumeweka in place utaratibu gani wa kushughulikia maafa kama hayo? Nothing. Kwa hiyo hii ya kumsifia Mbatia ni kutaka kupotosha lengo kuwa hatuna utaratibu wowote wa kushughulikia au kuzuia maafa kama haya nchini mwetu.
 
Mnyonge mnyongen lakin haki yake mpeni! No matter what alichokifanya mh mbatia ni sawa kama mtanzania mbunge ndugu jamaa na rafiki ana haki ya kuwasaidia waliopatwa na matatizo bila kuangalia SI-HASA! Napita tu

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Mbowe anapewa vyote hivyo lakini kaishia kwenye ukurasa wa facebook...

Uh Nilidhani alimshinda MBUNGE wa CCM Machame hakupewa kama MBATIA... hembu tujaribu kuangalia tena UCHAGUZI 2010 inaonyesha CHUKI imetujaa
 
Uh Nilidhani alimshinda MBUNGE wa CCM Machame hakupewa kama MBATIA... hembu tujaribu kuangalia tena UCHAGUZI 2010 inaonyesha CHUKI imetujaa

Kwahiyo Mbunge wa Hai hapaswi kusaidia watu wa Ilala?

Kweli elimu ya uraia inahitajika sana!!!
 
I think we are missing the big picture here. Mwenye jukumu la kushughulikia maafa nchini ni serikali. Yalipotokea mafuriko ya Katrina New Orleans ni serikali ya Bush ndiyo ilikuwa na dhamana ya kushughulikia maafa hayo, na ililaumiwa ipasavyo kwa kushindwa kuokoa maisha ya watu katika muda muafaka. Mafuriko yaliyotokea New York na New Jersey wiki mbili kabla ya uchaguzi wa mwaka jana Obama aliwajibika ipasavyo. Akishirikiana na gavana wa New Jersey alitoa ahadi kuwa serikali itahakikisha kuwa wahanga wanapewa msaada haraka. Hivyo ndivyo wenzetu wanavyofanya. Wanayo system in place na si kutegemea msaada wa mtu mmoja mmoja kama Mbatia na kumwona shujaa wakati system yetu ni a total failure. Hii si mara ya kwanza kwa jengo kuporomoka Dar-es- Salaam na ninaamini haitakuwa ya mwisho. Tumejifunza nini kutokana na jengo lililoanguka Chang'ombe? Nothing. Tumeweka in place utaratibu gani wa kushughulikia maafa kama hayo? Nothing. Kwa hiyo hii ya kumsifia Mbatia ni kutaka kupotosha lengo kuwa hatuna utaratibu wowote wa kushughulikia au kuzuia maafa kama haya nchini mwetu.
mkuu kuna watu wa ajabu sana, ripoti za majengo, mabovu wanazo, mamlaka za usimamizi wa ujenzi zipo chini yao, idara za uokoaji zipo chini yao, afu mtu anaibuka na thread kama hii! Wakati wengine tunajiuliza, kwa nini magorofa yanajengwa kwa 'wire mesh' ilhali kuna vyo vya usimamizi, yeye anajiuliza flani atashiriki vipi pale wire mesh za jengo zinavo jikunja!
 
mkuu kuna watu wa ajabu sana, ripoti za majengo, mabovu wanazo, mamlaka za usimamizi wa ujenzi zipo chini yao, idara za uokoaji zipo chini yao, afu mtu anaibuka na thread kama hii! Wakati wengine tunajiuliza, kwa nini magorofa yanajengwa kwa 'wire mesh' ilhali kuna vyo vya usimamizi, yeye anajiuliza flani atashiriki vipi pale wire mesh za jengo zinavo jikunja!

Kwahiyo wewe unajiuliza kuhusu wire mesh wakati kuna binadamu wako chini ya kifusi. Halafu unaamini kuwa kujiuliza kwako kuna thamani kuliko waliojitoa kuokoa waathirika!!!

Haya endelea kujiuliza...
 
Back
Top Bottom