ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
- Thread starter
- #61
Mbatia anasaidia kitu gani? Hakuna hata mwenye kujua cha kufanya japo kuna zaidi ya majengo matatu yameanguka hapo Dar. Acheni porojo zenu, Meya wa Ilala lazima awajibike kwa uzembe, Waziri wa Ujenzi na Naibu wake, waziri wa ardhi na naibu wake, Mkuu wa mkoa na wa wilaya. Waliobakia washitakiwe, ili iwe fundisho kwa uzembe huu
Mwache Maya wa Ilala. Ni kijana anayechapa kazi kwa weledi.
Alishasema hilo jengo lisiendelee kujengwa na alikuwa anaongoja ripoti ya mhandisi.
Tukipata vijana kadhaa kama Meya wa Ilala nchi itaendelea faster faster...
In his own words Mustahiki Meya anasema "Jengo hili lililoanguka binafsi nililisimamisha mwezi wa kumi mwaka jana na sasa nangoja taarifa toka kwa mhandisi wa halmashauri nini kiliendelea. Naendelea kutoa pole kwa wahanga na familia zao na naomba tuwe na moyo wa uvumilivu kipindi hiki."16