Biashara ya utumwa ilifanywa na babu zako, kumbuka hilo. Unafikiri watumwa walikamatwa kwa nguvu bila babau zako na machifu wao kuwauza? Waliwauza kwa vioo vya kujitazamaia, kwa kaniki na shuka za kujifunika, na shanga za kujipamba. Biashara ya utumwa ilikuwa ni kawaida sana enzi hizo kama inavyokuwa kawaida leo kwa majina mengine. Unaweza kunambia maana ya "manpower agency". Usidanganywe na aliyekufundisha historia ya kijinga kuwa Utumwa ulifanywa na "Mwarabu tu. Huyo alikudanganya ili akugawe na watetezi wako. Uislam na Waislam ndio watetezi wako wa kukutoa kizani kukuingiza kwenye Nuru ya maisha na kama ulikuwa huelewi.
Elewa kuwa Uarabu sio kabila au rangi kama ulivyojazwa ujinga na aliyekujaza ujinga. Jiulize ni nani huyo? Ni yule aliyewagawa akawatawala mababu zako kwa ukabila na dini. Kabla ya ujio wake.
Labda huelewi kuwa Waarabu wengi wapo Afrika kuliko kontinenti lingine lolote lile.
Labda huelewi kuwa kontinenti lenye watu weusi wengi nje ya Afrika leo hii ni Amerika, jiulize walifikaje huko, ni nani aliwapeleka huko> Ukipata majibu utakuwa umenielewa, labda ni ujinga tu ukufanye usielewe.