Huduma zinazotolewa na makanisa zimewasaidia sana waislamu. Kama unafikiri ni uongo mwulize jk amepata wapi elimu iliyomwezesha kuongoza taifa akiwa mwislamu. Mahospitali ya ngazi zote ya kanisa yanawasaidia wakristo na waislamu bila ubaguzi.
Ni ukweli kuwa ukimpa mkristo akufundishie mwislamu habari ya imani atamweleza uislamu kwa perspective ya kikristo. Hii ni common sense. Nina watoto wakristo ambao kutokana na kusoma shule za waislamu wanaimba kaswida na wanajua adhana. Mimi mwenyewe wajomba zangu wengi ni waislamu na wakati wa Idd sote tulienda huko kula siku kuu. Hivyo tungeimba nao kaswida na kufuatana nao misikitini.
Huu ndio ukweli.
Siku hizi kuna vituo vingi vya watoto yatima vinaendeshwa na taasisi za kiislamu. angalia vizuri hata katika luniga wote wanavalishwa hijabb.
huu utumbo wa eti makanisa yanawasomesha waislamu bila ya ubaguzi sipendi kuusikia, hizo ni hadithi za abunuasi, Serikali inyochukua kodi kwa waislamu na wakristo na kuyapa makanisa kuendesha shule halafu makanisa yakatoza ada kubwa na muislamu akasoma huko je muislamu kasomeshwa na kanisa , msifikiri wote tuna akili za kushikiwa acheni kuendelea na utumbo huu