Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Matajiri wa Moshi miaka ya 90 hadi 2000's

Nawafahamu hao Kisinane mkuu. Actually nadhani amekuwa underestimated. Huyu alikuwa na pesa kabla hata ya hao kina Mengi.

BTW Reginald Mengi pia ana mdogo wake anaitwa Benjamin Mengi nayeye pia ana miradi kadhaa na ana pesa. Hata kule Shanty town ana hotel moja siyo mbaya pametulia kiaina.

Benjamin Mengi alikuwa na kiwanda cha dawa. Kipo hapo chini ya ile chuo cha Northern kilichojengwa chini ya kiwango.
Sasa alikuwa anaagiza dawa ulaya kisha akija anazipack kisha anauza. Sasa walikuwa wanakula na mzungu sasa mzungu alipovujisha siri kwamba hakuna kiwanda ni usanii tu anaufanya Ben Mengi ikabidi TRA wampige deni la kukwepa kodi mpaka akakifilisi kiwanda.

Ila sisi wachagga ni shida mpaka huyu RC Mgwhira anasema tuna hela lakini viwanda hatutaki kuwekeza. Hela tamu kuliko demu wangu
 
Yap Mzee Hugo ni Don kitambo sana,gari yake ni Range Rover tuu tangu miaka ya 80s mpaka leo. Kwake ni kule Uru Njari.

Namfahamu huyo mzee. Mwaka 2016 nilipomaliza chuo nikuwaga naendaga pale Kuringe hall kwa nyuma kule sehemu wanapotupa takataka. Siku hizo mzee yule alipotoka akanikuta nipo na simu yangu maana eneo lile lina shika mtandao sijui kwa sababu ya makaburi. ALiponikuta akanichimba kwamba wewe utakuwa mwizi, akita walinzi wakaja na magobore kule kwa nyuma. Wakanichimbaa weee mwisho nikaondoka zangu.

Siku moja tulienda pale Kuringe mwak 2018 mwanzoni tulikuwa na mkutano wa ULGSP. Nimetoka kwenye semina maana nilikuwa nashuka point. Kuniona mzee akastuka nikamchimba na mimi kwamba nitamfungia hall yke kwa sababu haijakizi vigezo. Kuanzia hapo tukawa marafiki. Chezea nishakuwa serikali sasa
 
Kuna Kipindi nadhani Mwezi Julai 2012, tulikuwa tunacheza uwanja wa shule mida ya saa 10, Bob alipitisha Ndege yake mita chache saana juu ya uwanja, Kila Mtu alitawanyika, ilionekana Bob ni mtu asiyejali hata kidogo, wanasema pale soweto alikuwa anakodisha ndege zake yaani ukae nayo hewani nususaa/Lisaa.. ila watu hawakutaka yeye awe Pilot..kwa maana anavofly sio kawaida.. Pia ikumbukwe inadaiwa Bob hajawahi kusomea Urubani

Mtoto wake tulisoma naye Majengo secondary. Ikifika saa flani anaruka trench anakwenda kiwanja cha ndege anairusha ndege, kisha anapita nayo hapo juu ya shule mita chache sawa na mti. Ila hela bana aliyezigundua sijui aligundua nini. Mimi mwenyewe nikisikiaga pesa na ubinadamu nautupa kandooo sijali chochote maana maisha bila pesa hayanogi
 
Kumbe babu sambeke ndio huyo Billionaire Erasto Msuya ............ duh ndio nimejua leo

Unachanganya ma-file Msuya alikuwa mfanyabiashara wa madini na alipigwa risasi kule KIA. Sambeke yeye alikuwa mtu wa mandege ambayo alipata ajali kile kiwanja cha Arusha
 
Wajapan hawazitengenezi tena ila ukienda moshi hasa vijijini bado zipo japo chache sana

Nazionaga huku Kibosho inajazwa ndizi mpaka unaona gari inataka kukatika. Ukute limebeba majani yaani ni kama ghorofa inayotembea. Sasa naona Canter nazo wanazijaza kinoma mpaka inasukumwa. Ila wabongo gari la kubebea bidhaa za mjini sisi tunafanya la kijijini tunalishonesha mzigo mpaka linashindwa kuwaka
 
Na disco la Kilimanjaro hotel je? Mweeh
Saivi wameweka nakumat pale
Lilikuwa tamu sana
Nakumbuka kiingilio kilikuwa soda
Moshi nitarudi jamen
Hahahahah

Duhh wewe ulikuwa ni usalama wa taifa hadi Nakumat. Ila nakumat ilipofunguliw walipasua nazi na mayai wale wahindi.
 
Enzi hizo niko mdogo sana
Siku za sikukuu ndo tunaruhusiwa kutoka
Basi hausigel wetu namkumbuka hadija akawa anatupeleka pale na bwana ake
Tukiingia ndani hana time na sisi tena
Yeye bize na bwana ake
Akinunuliwa soda anamwaga kwenye Rasta kichwan tukawa tunazitaman mimi na kaka yangu ila hatuna jinsi lol
Inapigwa hidayaaa nitarudiii hahah maisha haya mweehhh

Ila wewe nimekugawa inaelekea watu wa kusini mna chembe chembe za u-changudoa kwa kweli. Ila Hidaya alifariki mwaka jana kama sikosei.
 
Msarikie alikuja kudharau mila wakamuokota kwenye vichaka huko hakujui hata anachofanya na kanzu yake,sijui ulikuwa ni ugonjwa sijui ndo mila zenyewe,Askofu wangu aliyenipatia kipaimara

Ata mimi alinipa KIPAIMARA KANISA LA KORONGONI. Kabla mauti hayajamkuta nilienda Saint Jose nikabusu pete yake akatubariki.

Mungu amrehemu askofu wangu
 
Nauliza wakuu kuna somebody lekule alikuwa na nyumba ya kupanga dsm street,zile za mfumo wa L,dah huyu jamaa tukiwa tumepanga pale miaka ya 1993,alikuja asubuhi akangoa milango na madirisha watu tupo ndani ili tuhame.kuna maneno wanasema alikuwa jambazi wa magari
 
Kwa uzi tujuane wandugu.mm sio mchaga ila nilikaa moshi dsm street.kwenye nyumba ya lekule.majirani zangu alikuwepo akina malik baada ya wazazi wao kufariki akawa mwizi walikuwa na nyumba.akina chale walikuwa wanachezea kipigo kutoka kwa baba yao kila siku.akina keffa sijui yuko wap?akina nassoro na wile watu wa mbeya sijui wako wap.ila enzi hizo kulikuwa na vibaka si mchezo
 
Back
Top Bottom