Maswali ya mwisho juu ya Escrow

Maswali ya mwisho juu ya Escrow

Ziliwekwa kule kwa muda kwa kuwa kulikuwa na kesi kati wanahisa wa IPTL.Zikawekwa kwenye akaunti ya ESCROW ambayo hakuna mwenye hisa yeyote angeweza kuchukua hadi kesi imalizike.Zingewekwa akaunti ya IPTL mwanahisa yeyote angeweza amka asubuhi na kuzitoa pesa zote ndio maana zikawekwa kwenye ESCROW ACCOUNT.

wewe ni ----- kweli hujui hata unachojibu ni kitu gani. rudi darasani kwanza dada...acha kukariri mambo usiyoyajua mbugila mkubwa!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mimi sijui kwanini hata mlimani TV walikuajili mbugila kama wewe halafu huku unataka ukagombee ubunge pwani yani ulivyokichwa maji sijui nani atakuchagua.


Ni kama Asumpta Mshana miaka yote aliheshimika,
Pale alioonesha utupu wa kichwa chake kila mmoja alimdharau kwa jinsi utupu wa kichwa ulivyo mkubwa!
mjepo ni bora ungekaa kimya kusitiri utupu wa kichwa chako kuliko kuonesha utupu wa kichwa chako ulivyo mkubwa,

Ni ushauri pia kwa wenzako wengine
 
Last edited by a moderator:
Mgogoro ulikuwa ni kati ya Tanesco na IPTL, waliolipana ni Tanesco na IPTL, maana yake waliafikiana kumaliza mgogoro, wakati wakifungua Escrow Tanesco na IPTL hawakuomba kibali cha bunge, so wakati wa kumaliza Escrow hawakupaswa kuomba kibali cha bunge, hii issue tumeipoliticize bila sababu

Kumbuka TANESCO ni Shirika la Umma na Pesa za Tanesco ni pesa za Wananchi kwa hiyo wananchi wana kila sababu ya kuelewa jinsi Tanesco ilivyofikia makubaliano ya kusitisha Mgogoro na IPTL.Bodi ya Tanesco ilitoa uamuzi unaoashiria uwepo wa Rushwa ndio maana uamuzi wake hauna maslahi kwa watanzania na wametakiwa kuwajibishwa.
 
Ziliwekwa kule kwa muda kwa kuwa kulikuwa na kesi kati wanahisa wa IPTL.Zikawekwa kwenye akaunti ya ESCROW ambayo hakuna mwenye hisa yeyote angeweza kuchukua hadi kesi imalizike.Zingewekwa akaunti ya IPTL mwanahisa yeyote angeweza amka asubuhi na kuzitoa pesa zote ndio maana zikawekwa kwenye ESCROW ACCOUNT.

Ww acha uongo kama hujui kitu bora ukae kimya , hata Jk RAIS wako hakusema hayo.
 
Mkuu wala usiwaze,sisi tulishauri vizuri sana,umiliki wa pesa hizo haukuwa certain,hivyo tukashauri badala ya kurepoti kama Assets on the face of financial statements,wai-disclose kama contigent assets kwa maana ownership yake ilikuwa bado na utata,hakuna mahali tukiposhauri ifutwe bali ihamishwe,nashangaa JK anapotosha kiasi hiki.
Aksante mkuu-huyu mpangaji wetu alikuwa anatapatapa tu,hana lolote
 
Mzee Tupa tupa, Ninachofikiri tukubali ile hela yote ni ya IPTL. Na IPTL wana haki kutumia hela yao kama wanavyopenda wao wenyewe. Lakini hili la kampuni ya kimataifa iliyokuwa inatupatia umeme kwa gharama na imenunua mitambo yake kihalali kabisa kwa gharama kubwa leo wamekuja Tanzania wakaingia katika mgogoro na Tanesco. Hela yao ikanasa katika akaunti ya Escrow kwa miaka yote hiyo badala ya kuingia katika mzunguko wa uzalishaji; fikiri ni hasara kiasi gani wamepata IPTL maskini!!!! Hatimaye taratibu zakuafatwa ipasavyo wakalipwa hela yao halali napata shida kupima IQ yao kwanini waliamua kusambaza ile hela kama karanga sokoni, na kuirusha juu katika mchezo wa sandakarawe wakaacha ipeperushwe na upepo ili kila anayetaka aokote. Wapita njia wasiohusika kabisa wakaokota!! hivi huyu CEO wa IPTL n nani? Alisomea wapi? Na lengo la kampuni hii kuingia katika biashara lilikuwa ni nini?? Imenipa maswali mengi mapya Bw Vuta Nikuvute.
 
Mzee TupaTupa ukweli yale malipo ni Mali ya IPTL lakini,Viongozi wakubwa Serlikalini waliuhujumu mfumo wa malipo hayo,ili waweze kuiba Fedha iliyokuwa kwenye Account ya Escrows- Mfumo wa Serikali ya chama cha mapinduzi Rais ni mwenye mamlaka yote,
Hata wahusika wanaonyesha dalili zote kwamba walipewa Amri Fanyeni.Bila Hilo hakuna mfanyakazi yeyote anaye weza kutoa Benk hata cent moja .Sasa wananchi mtu tuliyempa madaraka yote haya ni mheshimiwa Rais,kasema hakusema hakuna combo chochote cha kumuhoji. Mwisho Katiba Ya Jaji Warioba ndiyo Mkombozi Wetu,Bila hivyo mtashangaa
Sana tena Sana
Poleni Wanyonge
 
Pole,kazi unayo,acha mimi nibaki muongo kwa muda kwa kutoleta link ili ujionee.
Imefahamika kwamba Werema kajiuzulu(sijui kama na hili utataka link)
kwa nini Werema kajiuzulu?( naamini labda hili utaelewa na kunijibu

Werema kasema kajiudhuru kwa kuwa hajafahamika maamuzi yake na amesisitiza kuwa hakuna kosa alilofanya na hangependa yeyote awajibke kwa maamuzi yake.

Huyo ndiyo namna ya viongozi wanaotakiwa, anabeba majukumu yake, uchunguzi sasa utaonesha kama ana makosa au hana.

Rais wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi aliwahi kujiudhuru uwaziri wakati wa awamu ya Nyerere kwa makosa ambayo yalibainika si yake lakini kwa kuwa yeye ndiye alikuwa waziri wa wizara hiyo akaamuwa awajibike bila kushinikizwa.

Huo ndiyo ujasiri.

Upo hapo ulipo?
 
Hatutumii umeme wa bure tunalipia lakini si kwa namna hii mnayojalibu kutuaminisha.Mkuu ni saidie swali hili dogo.Tageta Escrow account ilifunguliwa na nani specifically?Tanesco na IPTL au Serikali

= mnayojaribu

Sasa wewe tuaminishe huo umeme kama hujamlipa aliyewekeza kwenye mitambo umlipe nani? Au Tanzania ndiyo mmekuwa paka wenye tasbihi ya dagaa? chembelecho kisemeo cha Kikwete.
 
Hakuna mahala katika maazimio ya bunge ambapo imesema kuwa hizo ni pesa za umma. Kumbuka hilo. Kama wewe umepaona tuoneshe na sisi. La sivyo unaweza kuwa na maoni yako lakini yasiyo kweli.

Mpaka CAG aliamrsha TANESCO wafute kwenye vitabu vyao kwani hizo pesa hawana haki ya kusema zao.

Mlitaka umeme wa bure?

Rejea hapa:
"KWA KUWA, kwa sababu ya kuhusika kwa watu hao na miamala iliyofanyika kwenye Akaunti ya Escrow imeliingizia Taifa hasara ya mabilioni ya fedha za umma zinazotokana na kutokulipwa kwa kodi mbali mbali za Serikali na kushindwa kwa TANESCO kukokotoa upya kiwango cha malipo ya gharama za uwekezaji (‘capacity charges') wa IPTL"

Hiyo ni para ya pili ya Azimio la kwanza la Bunge kuhusu sakata la Escrow. tafsiri ya azimio la bunge ni kwamba kuna kiasi kikubwa tu katika ile fedha ambacho kilikuwa ni fedha ya umma. na hiyo ndio statement ya CAG alipohojiwa na gazeti la Raia Mwema. hata akili za kawaida tu zitaonesha hivyo. kwa hiyo si sawa kusema moja kwa moja kwamba zote zile zilikuwa za Umma - granted. Lakini pia SI SAWA KUSEMA KWAMBA ZILE PESA SIYO ZA UMMA. hapo Rais kadanganya taifa, na hiyo imepunguza MORAL AUTHORITY ya Rais.

Lakini la msingi zaidi, rejea para ya tatu ya Azimio la Bunge:

"KWA KUWA, mabilioni ya fedha yaliyotolewa kwenye Akaunti ya Escrow yametumika kuwapa kile kinachoonekana kuwa ni rushwa baadhi ya viongozi na maafisa wa serikali kama vile Mawaziri, Majaji, Wabunge, Wenyeviti wa Kamati za Bunge, wakuu wa taasisi za umma, viongozi wa dini, mawakili wa kujitegemea na watu binafsi.

NA KWA KUWA, vitendo vilivyofanywa na watu hawa vinaashiria makosa mbali mbali ya jinai kama vile uzembe, wizi, ubadhirifu, kutakatisha fedha haramu, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa na kupokea mali ya wizi;"

La msingi zaidi, ni kwamba hii fedha inayoitwa kuwa ni ya IPTL, iliyogawanywa kama vile haina mwenyewe, watu wakabeba kwenye Lumbesa, jamani, hata ile 10 pasenti huwa haiwi hivyo. na imegawanywa kwa watu wenye madaraka na wenye dhamana ya kutoa haki kwa mujibu wa sheria. hii kwa watu ambao siyo wavivu wa kufikiri, lazima watahoji hata hilo povu la wengi wanaoshadidia kwamba hiyo si fedha ya Umma. na ndio maana wanatumia rungu kwamba eti kwa kuwa rais kasema basi maswali zaidi yasiulizwe. ni shida sana kuficha samaki waliochina. utauficha mfuko usionekane lakini harufu unaifichaje??
 
Siyo kajiudhuru ni kajiuzulu. Siyo kujiudhuru ni kujiuzulu na siyo akaamuwa ni akaamua.

Werema kasema kajiudhuru kwa kuwa hajafahamika maamuzi yake na amesisitiza kuwa hakuna kosa alilofanya na hangependa yeyote awajibke kwa maamuzi yake.

Huyo ndiyo namna ya viongozi wanaotakiwa, anabeba majukumu yake, uchunguzi sasa utaonesha kama ana makosa au hana.

Rais wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi aliwahi kujiudhuru uwaziri wakati wa awamu ya Nyerere kwa makosa ambayo yalibainika si yake lakini kwa kuwa yeye ndiye alikuwa waziri wa wizara hiyo akaamuwa awajibike bila kushinikizwa.

Huo ndiyo ujasiri.

Upo hapo ulipo?
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
ni za IPTL kwa hukumu ipi? account ilifungiwa pesa ziwekwe wakati ikisubiriwa muafaka kwenye mgogoro baina ya IPTL na TANESCO mgogoro umeisha?? acha kutumia akili za pongo wewe?!
Osokoni mgogoro uliisha na ndo maana pesa ilitoka.
labda unaweza kuuliza uliishi mahakama gani,ukweli ni kuwa huo mgogoro wa pili baada ya ule uliotatuliwa kwanza na ISCID,haukuwahi kwenda mahakamani,ulimalizwa nje ya mahakama kwa tanesco na iptl kufanya recalculation,kukubaliana na hatimae kuifunga account ya escrow.
 
Siyo kajiudhuru ni kajiuzulu. Siyo kujiudhuru ni kujiuzulu na siyo akaamuwa ni akaamua.


mkuu huwa mnanifurahisha huyo faiza forxy anae jifanya anajua kiswahili anarekebisha na katikati ya sentensi yake ya marekebisho na yeye anakosea sasa sijuianakijua nn...big up kwa mnao mfatilia mfatiliaji.
 
Kumbuka TANESCO ni Shirika la Umma na Pesa za Tanesco ni pesa za Wananchi kwa hiyo wananchi wana kila sababu ya kuelewa jinsi Tanesco ilivyofikia makubaliano ya kusitisha Mgogoro na IPTL.Bodi ya Tanesco ilitoa uamuzi unaoashiria uwepo wa Rushwa ndio maana uamuzi wake hauna maslahi kwa watanzania na wametakiwa kuwajibishwa.
Kwamba walitoa uamzi unaoashiria rushwa,weka sasa hivyo viashiria vya rushwa tuone.
ukweli ni kuwa mgogoro wa tanesco na iptl kuhusu capacity charge uliisha na ndo maana pesa ikatoka.
ila kina mkono na wahepele wake kwa kuona watu wengi hawana uelewa mpana wa ishu hii wakaja na santuri eti kuna bilioni 321 zimeporwa escrow,wakisaidiana na mengi mwenye uhasama na mulongo akatumia vyombo vyake vya habari kulikoleza jambo hili,nao wabunge vilaza na wengine wakishawishia na rushwa toka kwa kina mengi na mkono,wakaunga tela na kulishikia bango.
 
Osokoni mgogoro uliisha na ndo maana pesa ilitoka.
labda unaweza kuuliza uliishi mahakama gani,ukweli ni kuwa huo mgogoro wa pili baada ya ule uliotatuliwa kwanza na ISCID,haukuwahi kwenda mahakamani,ulimalizwa nje ya mahakama kwa tanesco na iptl kufanya recalculation,kukubaliana na hatimae kuifunga account ya escrow.

du!!! walikubali kuwa kiwango kinachatozwa ni sawa?
 
Shukrani Mkuu 🙂🙂

mkuu huwa mnanifurahisha huyo faiza forxy anae jifanya anajua kiswahili anarekebisha na katikati ya sentensi yake ya marekebisho na yeye anakosea sasa sijuianakijua nn...big up kwa mnao mfatilia mfatiliaji.
 
Kinachoitwa kwamba ni kashfa ya akaunti ya Escrow ni ngoma ambayo wanaoichezesha wanafanya hivyo kwa matumaini kwamba wakiivutia kwao basi hatimaye watafaidika ipasavyo. Miongoni mwa wanaoishangilia ngoma hii ni baadhi ya mawakili waliokuwa wakiitetea Tanesco na Benki ya Standard Chartered.
Benki ya Standard Chartered inataka kuhakikisha kwamba kunakuwapo na sintofahamu kuhusu akaunti hiyo ya Escrow na kulazimisha imilikiwe ama na Serikali ya Tanzania au Tanesco kwa sababu hiyo inaweza kuisaidia katika lengo lake kuu la kupata fedha isizostahili. Ni wazi kwamba fedha zilizohifadhiwa katika akaunti hiyo ya Escrow si za Serikali wala si za Tanesco kama ambavyo Standard Chartered na wapambe wao wanavyolazimisha iwe. Fedha hizo ni za IPTL.
Migogoro kati ya TANESCO na IPTL ilianza mwaka 1998 baada ya IPTL kukamilisha kwa kiasi kikubwa ujenzi wa mtambo wa 100MW Tegeta Mjini Dar es Salaam. IPTL walitaka Tanesco inunue umeme kwa bei kubwa kuliko ilivyo kuwa halali lakini Tanesco walikataa kwa madai kwamba gharama zilizoainishwa na IPTL zilikuwa kubwa mno kuliko gharama halisi za uwekezaji.
Tanesco katika jitihada za kujinasua iliajiri kampuni ya uwakili ya Mkono & Co. Advocates ili kutoa huduma za kisheria kwa kushirikiana na Huntons & Williams ya Marekani.
Kutokana na tofauti za mitazamo ya gharama za uwekezaji, mawakili hawa waliishauri Tanesco ifungue kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji {ICSID} nchini Uingereza dhidi ya IPTL ili kupinga gharama hizo.
Katika uamuzi wa Julai 2001 uliotolewa na ICSID kwenye kesi iliyofunguliwa na Tanesco dhidi ya IPTL mwaka 1998, mahakama hiyo ilitoa uamuzi kwamba, gharama za uwekezaji zishuke kutoka dola za Marekani milioni 163.53 hadi milioni 121.83.
Uamuzi huo wa mwaka 2001 uliridhia mfumo wa kifedha {financial model} iliyokuwa imekubalika katika kukokotoa viwango {tariff calculation} kati ya Tanesco na IPTL ambayo inaipa IPTL marejesho ya uwekezaji {internal rate of return - IRR} ya asilimia 22.31 badala ya asilimia 23.1 iliyodaiwa na IPTL. Mawakili wa Tanesco Mkono & Co Advocates walishauri kwamba Tanesco itekeleze mfumo huo.
Mwaka 2004, mawakili hao hao wa Tanesco wakiongozwa na Mkono & Co. Advocates waliishauri Tanesco isitekeleze ulipaji wa tozo ya uwezo wa kuzalisha umeme {Capacity Charges} kwa kutumia mfumo wa kifedha uliokubalika mwaka 2001. Kutokana na ushauri huo, Tanesco kwa kuamini ushauri wa mawakili wao mwaka 2006 kwa kupinga thamani ya invoices zilizowasilishwa na IPTL kwa kutumia mfumo wa fedha {financial model} iliyotolewa na ICSID. Kitendo hicho kiliifanya IPTL kuupinga uamuzi huo wa Tanesco wa kutofuata ulipaji wa tariff kwa kutumia mfumo wa fedha wa mwaka 2001.
Baada ya Tanesco kupokea ushauri wa Mkono & Advocates iliutilia mashaka na hivyo kuamua kuomba ushauri kwa kampuni ya Huntons & Williams iliyokuwa ikiishauri Serikali katika mashauri ya nje ya nchi.
Kampuni ya Huntons & Williams ilisisitiza kuwa unaosemekana kuwa ni ugunduzi uliofanywa na kampuni ya Mkono & Co. Advocates ulikosa hoja ya msingi yakuifanya Tanesco ipinge kulipa tozo ya uzalishaji umeme {capacity charge} kama ilivyokubalika mwaka 2001.
Ni wazi kwamba ushauri wa kampuni ya Mkono & Advocates ulikuwa ni wa kuipotosha Serikali na Tanesco kwa manufaa binafsi na kwa mantiki hiyo basi kampuni ya Mkono & Co Advocates ilikusudia kesi kati ya Tanesco na IPTL iendelee ili waendelee kulipwa gharama za kuendelea na kesi.
Ushahidi wa upotoshaji ni mwaka 2012 Mkono & Co. Advocates kuitaka Tanesco kukubali usuluhishi nje ya mahakama katika shauri la Tanesco kukataa kuilipa IPTL capacity charges kwa kigezo kwamba uwezekano wa Tanesco kushinda katika kesi ya kupinga kiwango cha tozo ulikuwa mdogo na unaashiria kuendela kuuiingiza Tanesco kwenye hasara kubwa na kesi zisizokuwa na ukomo.
Aidha, moja ya kesi ambazo zinathibitisha kuwapo kwa mgongano wa kimaslahi wa mawakili ni shauri kati ya Tanesco na Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong {SCB-HK} lililoko ICSID.
Shauri hilo linawakilishwa na mawakili wenye asili na historia ya pamoja na kampuni ya Mkono & Co. Advocates. Mkono & Co. Advocates anaiwakilisha Tanesco na kwa upande mwingine Bw. Charles Morison mwenye mahusiano makubwa na kampuni ya Mkono & Advocates kwa kuwa alikwa mwanasheria wake ndiye anaiwakilisha SCB-HK.
Mahusiano haya ya kikazi kati ya mawakili hawa yanaashiria mgongano mkubwa wa kimaslahi na kuifanya Serikali na Tanesco wasinufaike na huduma yao kwa kuwa huduma za mawakili hao zilikuwa zimegubikwa na maslahi binafsi na kuwatwisha Watanzania mzigo mkubwa.
Ukiachilia mbali kizungumkuti hicho cha mgongano wa maslahi tangu kampuni ya Mkono & Co. Advocates kwa pamoja na Huntons & Williams wapewe kazi hiyo ya uwakili na Tanesco mwaka 1998, jumla ya shilingi bilioni 62.9 zimelipwa kwa kampuni ya Mkono & Advocates.
 
Back
Top Bottom