Kwa hili sakata la ESCROW Rais ametoa funzo kubwa sana kwa waliomtangulia na watakaokuja:
-Kwanza ni somo la utawala bora unaofuata misingi ya sheria, kanuni tulizojiwekea kwenye utumishi na mamlaka mbalimbali;
-Pili ni mgawanyo wa madaraka kikatiba na kisheria juu ya mihimili yetu mitatu ambayo ni Dola, Mahakama na Bunge;
-Tatu ni juu ya dhana nzima ya uwajibikaji pale inapolazimu kufanya hivo na
-Nne ni ITIFAKI na nidhamu.
Kwa kweli ambao hamtaki kumwelewa Rais wetu ni kwa kuwa tu mliamua kwa pupa, kwa jazba, kwa visasi na mihemuko ya kisiasa. Kwa mfano, ilikuwaje Bunge zima likashindwa kuelewa taratibu za kuwawajibisha Majaji? Ilikuwaje Bunge zima likashindwa kuelewa kuwa Katibu Mkuu ni Mtumishi wa UMMA na ziko taratibu za kufuatwa ili kumwondoa madarakani?