Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Mbona aliyekuwa nae ndani ya gari kwenye ajali kaelezea vizuri tu ajali ilivyotokea,mtoa post hukuangalia habari ya jana Star tv? Tusipende kuraise vitu ambavyo hata habari hatutafuti kwa kina kujua ukweli wa jambo.
 
wamekufa kina daud mwangosi itakua mtikila!!
 
Natoa ushauri kwenye kila Mikutano ya UKAWA , viandaliwe VIPEPERUSHI vya kueleza jinsi ya kupiga kura ,maana naona kuna uwezekano wa kura nyingi kuharibika kutokana na ufahamu mdogo na hasira walizokuwa nazo wapiga kura
 
Mbona aliyekuwa nae ndani ya gari kwenye ajali kaelezea vizuri tu ajali ilivyotokea,mtoa post hukuangalia habari ya jana Star tv? Tusipende kuraise vitu ambavyo hata habari hatutafuti kwa kina kujua ukweli wa jambo.

Hapo wanamtafuta mchawi sijui watampataje. Kuna mahali nimesoma wengine wanamhusisha Lowassa kwenye hii ajali. Jamani jaman tunazidi kumpa mungu hasira azidi kutuadhibu. Tuwe na hofu ya mungu usimnene mtu mabaya yatakurudia wewe.
 
Hivi ile breafcase hawa policcm si walisha isachi kila mahali.
 
Mstutoe kwenye mada ya muhimu,tarehe 25 sio mbali kabisa tutumie vikatio vyetu vizuri haya mengine yatafuata.ETI MTIKILA auwawe????FOR WHAT!!!! ana kipi cha muhiiiiiimu cha kusababisha auwawe,CCM msilete za kuleta,MTOI alivyokufa mbona hatukusema ni JM
 
Ahahaaha acha kulazimisha unachotaka kiwe ndio kiwe, eti sounds interesting. Hapo ulipo taarifa unazozitumia ni hizi zilizoenea kwenye mitandao ya jamii amabazo ni chache na unreliable kuweka conclusion. Wakati mwingine give yourself time to gather data and information before you speak out
Wazalendo husikiliza watu wote..kujaribu kudodosa... ni dodoso tu..Haki yangu!!!
 
CCM Wameishiwa hoja na sera mananiliiii yamewashuka magotini.
 
Gari imeacha njia ikapinduka, mbona ajali aliyopata awali haizungumzwi?
 
conspiracy!! mtu unaona picha moja na hear says tayari unajifanya crime scene officer. wabongo bana
 
Mmeanza Swine! Watanzania Fanyeni Mambo Yenu Na Iacheni Rwanda Na Maisha Yake. IKIGUSWA Tu Nchi Ya Rwanda Gentamycine SITANYAMAZA Na Hali Ya Hewa ITACHAFUKA Humu. Mtuache WANYARWANDA TUPAMBANE NA MAISHA YETU KWANI GENOCIDE Ya 1994 IMETURUDISHA MNO NYUMA ILA Tunashukuru Mwenyezi Mungu SASA KIONGOZI Wetu Mwenye HAIBA Kama Za Dr. Magufuli KIPENZI Changu His Excellency President Paul Kagame ANAIRUDISHA Rwanda Ktk Economic and Development Map. I Love Rwanda, I Love Paul Kagame, I Love Tutsi Tribe And I Love Dr. John Pombe Joseph Magufuli.

Umejielewa ulichosema. ... kwamba watanzania tufanye yetu tuwaache nyie wanyarwanda. .! Mbona we ya kwetu Tanzania unayaongelea?? Tena unayashobokea haswa! eti utachafua hali ya hewa humu JF kisa Rwanda imetajwa.. . Hovyo! Na vitisho vyako vya kitoto. Hopeless
 
conspiracy!! mtu unaona picha moja na hear says tayari unajifanya crime scene officer. wabongo bana

kwa akili yako mtu arushwe nje ya gari akandamizwe na gari bado asichubuke! Bado ashikilie pochi yake! Basi ilikuwa na madini ya thamani sana.
 
huu ni upuuzi kuanza kuwahusisha watu kwa kuwataja majina kwenye ajali kama hii.
Kama una jambo la msingi nenda na ushahidi/dukuduku lako kituo cha polisi uwasadie ili ukweli ujulkane badala ya
kuanza kusambaza habari za kipuuzi kama hizi....tena zaidi kumhusisha rais wa nchi jirani.
 
Historia ipo ili watu wajifunze kwayo, kila tukio linalotekea ni funzo kwa mwenye akili…

Mwaka 1985 tarehe 7 April, Afisa mstaafu, Mwanasheria na Mwanaharakati maarufu nchini Uingereza mwenye asili ya usikochi Willie MacRae ambaye alikuwa Makamu mwenyekiti wa SNP, aliyekuwa akipambana na Unyonyaji wa waskochi masikini na makundi ya mafia yenye kumiliki makampuni makubwa nchini humo alipata ajali ya gari na kufariki katika milima ya Scot.

Ajali yake ilizua mjadala mkubwa kuwahi kutokea nchini humo kutokana na mambo yafuatayo;

1.Wajihi wa Willie na vita yake dhidi ya MAFISADI.
2.Utata wa Ajali yake.
3.Ripoti ya Polisi.

WAJIHI WA WILLIE NA VITA YA UFISADI.

Willie kama walivyo wanaharakati wengi duniani alikuwa ni sauti ya wasio na sauti, wanyonge wa nchi ambae alitangaza wazi wazi vita dhidi ya Wanyonyaji na Mafisadi nchini mwake, akiwa kama Mpinzani ambaye aliweza kuwashambulia na hata kufungua kesi mara kadhaa mahakamani kupinga operation za makampuni makubwa ya Nuclear yanayomilikiwa na Mafia wenye mikono mirefu Serikalini ambao walinunua vyama vya siasa ambavyo vilikuwa vikipambana kwenye kampeni ili kuchukua Serikali.

Willie akiwa mstari wa mbele kupinga Kitendo cha Kampuni ya Dounrey Nuclear Power Development kumwaga takataka baharini, alifungua kesi na kuandaa vidhibiti vya kisheria kuthibitisha kuwa jambo hilo lina athari kubwa kwa wananchi, na kutokana na vitisho na sensitivity ya vidhibiti hivyo ilimbidi awe anatembea navyo kila wakati na kila anapokwenda hakuwahi kuziacha sehemu hata ofisini kwake ingawa baada ya kifo chake haikujulikana Document hizo zilipotelea wapi.


UTATA WA AJALI.

Watalii wawili watalii wa Ki-australia waliona gari aina ya Volvo katika bonde la Glenmoriston, na watalii wale walisogelea na kukuta mwili wa mtu kwenye gari hiyo ukiwa umejaa damu kuanzia kichwani na mwili mzima, mikono ikiwa imeshika usukani wa gari, kichwa kimelalia bega moja na hakuwa amevaa mkanda wa gari (seatbelt)
Wakasogea barabarani na kusimamisha gari ambayo ndani yake kulikuwa na Diwani wa Chama Cha SNP ambaye alimtambua WILLIE na kutambua pia kuwa alikuwa HAJAFA bado, wakamuwaisha Hospitali Aberdeen Royal infirmary ambapo alifariki na hospitali hapo iligundulika alipigwa risasi kichwani, kabla ya gari yake kutumbukia kwenye korongo hilo.


RIPOTI ZA POLISI

Ilikuwa kitendawili kikubwa kwa kuwa ripoti ya kwanza ilisema kuwa alitumbukia bondeni kwa kukosa kulimiliki gari kutokana na spidi, lakini ripoti ya hospitali inasema alipigwa risasi ya kichwa kabla ya kutumbukia kwenye korongo na kwa kuwa kioo cha gari hiyo hakikuwa na tundu la risasi ikabainika kuwa mpigaji wa risasi hiyo alikuwa ndani ya Gari hiyo kisha akashuka na kulisukuma gari kwenye Korongo.

Uchunguzi pia ulibaini kuwa bastola aina ya Wesson 45 Calibre ilipatikana mita chache kutoka ilipookotwa gari ya Willie, lakini hakukuwa na alama zozote za vidole kwenye bastola hiyo jambo lililofanya isitumike kama ushahidi katika upelelezi wa kesi hiyo.

TUKIO SIKU YA KIFO CHA WILLIE.

Siku ya Kifo cha Willie ambacho kilikuwa ni gumzo kilifuatiwa na tukio la Wanasiasa wawili maarufu na wabunge wa Chama Cha Ulster Unionist kujiuzulu, Ulster ni Chama ambacho kilikuwa kinapingana na harakati za WILLIE. Kitendo hicho kilitafsiriwa kuwa ni Decoy..,kuwaondoa wananchi katika mjadala wa kifo cha WILLIE.

‘’NCHI zingine Duniani Serikali zina Mafia lakini TANZANIA mafia wana Serikali..” Dr Slaa Nov,2009 on response to Richmond Scandal’s.

R.I.P Mtanganyika Rev. Christopher Mtikila…Hivyo ndivyo ulivyo mwisho wa wanaharakati wa kweli duniani.
Namna hii ndio ulikuwa mwisho wa;
@ Kassi Manlan wa Burundi – 2001
@ Clement Oumarou wa Burkinafaso – 1991
@ Abdelkader Hachani wa Algeria – 1999
@ Rev. Emile Biayenda wa Congo – 1977
@ John Kaiser wa Kenya – 2000
@ Carlos Cardoso wa Msumbiji – 2000
@ Dian Fossey wa Rwanda – 1985

Na pia ulitanguliwa na Rev Janani Luwum wa Uganda mwaka 1977...na hakika wapo watakaofuata baada yao…
 
Back
Top Bottom