Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila

Kwahiyo mnataka tuamini kuwa hao waliopanga kumuuwa walikuwa na akili fupi kihasi cha kushindwa kufikiria kuwa wakimuacha bila majerahaa itazua maswali? mnataka kutuaminisha kuwa hawakufikiria kumjeruhi kwanza mtikila kama walivyowajeruhi hao madereva na mchungaji Mgaya? yani mmewaita kuwa ni majasusi wa hal ya juu wenye uwezo wa kuingia popote lakini katika hii ajali ya Mch Mtikila wamekuwa ni mambumbu wasiojua kutengeza ajali itakayoshinda kuzua maswali kwenye vichwa vya wapumbavuk


katika ku engineer ajali kuna majeraha wataalamu mara moja wanaweza gundua kuwa mtu ameinflict na si ajali,kwahiyo hawawezi kumkata mapamnga eti ionekane ajali imemuumiza

Hao majeruhi wengine wamewajeruhi vipi? wakashindwa kumjeruhi na Mtikila kama hao majeruhi wengine? au tayari imethibitishwa kuwa majerahaa yao sio ya ajali ya gali
 
Maswali yako yanaonekana yana tija, nadhani wewe unafaa kulisaidia jeshi la polisi.
 
Gazeti la UHURU limeandika gari alilopanda marehemu liliacha njia ili kukwepa gari iliyotekea mbele yao kwa ghafla, baada ya kuacha njia na kuingia pembeni mwa barabara, kwa kuwa dereva alikuwa kasi gari lilikita kwenye shimo na kupinduka, Marehemu alitokea kioo cha mbele(bila shaka hakufunga mkanda), na kisha gari ilimlalia upande wake wa kushoto kifuani. hakuwa na jeraha lolote zaidi ya kutokwa damu mdomoni.
HILO NI GAZETI LA UHURU (05-10-2015) UK. 4
 
Mmeanza Swine! Watanzania Fanyeni Mambo Yenu Na Iacheni Rwanda Na Maisha Yake. IKIGUSWA Tu Nchi Ya Rwanda Gentamycine SITANYAMAZA Na Hali Ya Hewa ITACHAFUKA Humu. Mtuache WANYARWANDA TUPAMBANE NA MAISHA YETU KWANI GENOCIDE Ya 1994 IMETURUDISHA MNO NYUMA ILA Tunashukuru Mwenyezi Mungu SASA KIONGOZI Wetu Mwenye HAIBA Kama Za Dr. Magufuli KIPENZI Changu His Excellency President Paul Kagame ANAIRUDISHA Rwanda Ktk Economic and Development Map. I Love Rwanda, I Love Paul Kagame, I Love Tutsi Tribe And I Love Dr. John Pombe Joseph Magufuli.

Mhhhhhh wewe
 
Kifo cha Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila jana alfajiri kwa ajali ya gari kimetajwa kuwa ni mwendelezo wa vifo vya aina hiyo vilivyowakumba wanasiasa wa Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni.

"Aliondoka hapa Ijumaa kwenda Njombe kumnadi mgombea wetu wa ubunge , Nicodemus Atoswege na walipata ajali katika kijiji cha Msolwa, Chalinze. Ndani ya gari hilo pia alikuwa Mchungaji Mgaya, Ni huyu ndiye aliyetoa taarifa za awali za ajali na kifo hiki" Alisema Katibu Mwenezi wa DP Mwambichoka Ferous.

Wanasiasa na vifo vya ajali:
Julai 27, 2008, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Chacha Wangwe, alifariki dunia kwa ajali ya gari liliyozua utata mkubwa katika maeneo ya Panda mbili mkoani Dodoma. Kabla ya kifo kile , Wangwe aliyekuwa akielekea Dar es salaam kuhudhuria mazishi ya mwanasiasa mkongwe, Bhoke Mnanka alikuwa kwenye malumbano na uongozi wa CHADEMA, wakati huohuo alikuwa amepania nafasi ya juu ya uongozi ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani. Katika ajali hiyo , alifariki yeye huku mtu mwingine aliyekuwa naye, Deus Malya akinusurika , hivyo kuzua maswali mengi.

Oktoba 24, 2007 , kada na Mbunge wa CCM, Salome Mbatia , alifariki kwa ajali ya gari akiwa njiani kwenda Songea kusaka kura za ujumbe wa NEC ya CCM. Utata katika ajali hiyo ya Salome uliibuka kwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA wa wakati huo, Zitto Kabwe, naye alikuwa njiani kwenda Songea kwa shughuli za kikazi. Wakati huo Zitto aliyekuwa kwenye mgogoro wa ndani na CHADEMA, alisimama kwa muda Njombe na kuliona gari lake, likipita hapo na muda mfupi baadaye alikuta limepata ajali.

Mbunge mwingine wa CHADEMA aliyefariki kwa ajali za namna hiyo ni Regia Mtema huku mwezi uliopita , mgombea ubunge wa CHADEMA huko Lushoto, Mohamed Mtoi , naye alifariki dunia kw ajali ya gari. Marehemu Mtoi anatajwa kuwa, alikuwa na misimamo ndani ya CHADEMA kama waliyokuwa nayo Zitto Kabwe na Chacha Wangwe.

Chanzo: Raia Tanzania

Tafakuri: Tutakumbuka kuwa siku za hivi Karibuni, marehemu Mtikila alijitokeza waziwazi kwenye vyombo vya habari na kusema, mgombea urais kwa tiketi ya Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa Katiba ya Wananchi(UKAWA), Edward Ngoyai Lowassa ni fisadi na hafai kuwa rais wa nchi hii. Marehemu Mtikila alienda mbali na kusema nchi za wengine kama CHINA, LOWASSA angeshanyongwa kwa sababu ya kujihusisha na ufisadi.

20151005_090154.jpg
 
Gazeti la Mwananchi wameandika mahojiano na majeruhi,mmojawapo ni mchungaji Mgaya ambaye ni NDUGU WA MTIKILA.Wewe Moringe unasema walikutana mwezi mmoja tu uliopita!

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani amesema uchunguzi wa awali unaonyesha chanzo cha ajali ni mwendokasi wa gari ambapo Mtikila ambaye hakufunga mkanda alitupwa nje ya gari kupitia kioo cha mbele halafu ikamlalia upande wa kushoto wa gari.

Alama za gari tangu ilipotoka barabarani zinaonyesha ilitembea nje ya barabara kwa takriban mita 100 halafu ikakuta kibonde,ikapaa na kugonga mti,na kupinduka(nadhani ndio hapa Mtikila alipotokea kioo cha mbele kutokana na impact ya mti,ndio sababu alitua karibu na ilipotua gari ikamlalia na ndio sababu gari imechakaa zaidi mbele kuliko pembeni).

Kamanda Mohamed amesema pia licha ya mwendokasi,upo uwezekano dereva alizidiwa na usingizi na wanaendelea kumhoji.

Jamani tuache vyombo vya dola vifanye kazi yake.
 
maskini watu wa kijani,mbona mmepanic sana??? Mohamed mtoi alipopata ajali na
kufariki tuliamini ni mapenzi ya mungu na tulilipokea jambo hilo na
kulikubali. Iweje leo afariki binadamu kama alivyokuwa aliyetangulia
watu waanze kutuletea hadithi za kifo cha kupangwa???
Kumbukeni ndugu zangu, mungu hadhihakiwi. Akiamua jambo,hutenda kwa wakati
na majira apangayo yeye na si vinginevyo. Period!!!

 
Hao majeruhi wengine wamewajeruhi vipi? wakashindwa kumjeruhi na Mtikila kama hao majeruhi wengine? au tayari imethibitishwa kuwa majerahaa yao sio ya ajali ya gali

nachokiona mtikila kilichomuua sio ajali, kwani inaonekana alitoka mzima na akabeba breaf case yake, ila inaonekana alianza kuzidiwa ndo maana akapewa huduma ya kwanza ikiwa kumfungua mkanda shati na kumvua viatu.

Mtu anayekuua atakupepea na kutoa msaada wote huo? Inawezekana alikuwa na matatizo mengine ambayo wenzie waliyajua pia.
 
Pia kwenye hiyo list wamo
Akukweti
Sokoine
Imran Kombe
Kolimba
Malima
Yule kamanda wa polisi Mwanza
Sengondo Mvungi

Bila kusahau
Amina Chifupa
Karume
Makamu wa raisi wa kwanza kwa Mkapa

Tusiwasahau pia
John Komba
Selina Kombani
Mgimwa
Saidi Bwanamdogo (aliyerithiwa ubunge na Ridhiwani)

R.I.P viongozi wetu
 
Njaa mbaya sana. Shigongo hizi mambo zitakupeleka wapi?
 
nachokiona mtikila kilichomuua sio ajali, kwani inaonekana alitoka mzima na akabeba breaf case yake, ila inaonekana alianza kuzidiwa ndo maana akapewa huduma ya kwanza ikiwa kumfungua mkanda shati na kumvua viatu.

Mtu anayekuua atakupepea na kutoa msaada wote huo? Inawezekana alikuwa na matatizo mengine ambayo wenzie waliyajua pia.

tunaweza kuanzia hapa maana kunapoint.
 
Acheni ushabiki kunguni nyie watanzania wanao kufa kwa ajali pia wameuliwa nyie nyoko nini mnaboa mno tumieni akili kifo cha MTU kikipangwa kimepagwa na hakuna Wa kuzuia
 
Mambo mengine nikujifanya ukomando yoso, gari yenyewe inaonekana mkweche, unasafiri na gari ndogo kutoka njombe hadi dar tena usiku kwa usiku, kama walianguka saa alfajiri walianza safari saa ngapi?

Siku hizi watu wamagari binafsi wanasafiri usiku kukwepa tochi za trafik sasa wakibinuka wanaanza kutafuta wachawi.
 
Back
Top Bottom